mwanakijiji lugusi
Senior Member
- Apr 13, 2016
- 128
- 96
Nateseka sana wadau nina miaka kumi hili tatizo nililonalo la mdomo kuwa mchungu huku viungo vya mwili vikiuma na uchovu uliopindukia, na nimejaribu kwenda hospital kucheki vipimo vyote lakini tatizo halionekani. Nimetumia madawa ya kila aina ya antibiotics lakini hali inazidi kuwa mbaya huku tumbo langu likinguruma sana. Mbaya zaidi nikilala usingizi hata mchana naamka mwili umechoka ukiambatana na maumivu makali na mdomo ladha ni chungu utadhani nimekunywa nyongo. Jamani yaweza kuwa tatizo gan? Mwenye uelewa, kwasababu nateseka sana