Napata shida ofisini kwangu goba, majirani wameanza kunichukia

Ofisi yako ni ipi pale nije kukuungisha?

Kuna hizi tatu zinazokaribiana ukiwa unatokea Mbezi, moja ya mwanzoni iko kushoto, ya pili kulia na ya tatu kushoto karibia na kituo cha daladala. Au kile kidogo pale pale Senta, au ile ya njia ya Makongo.

Wewe ni yupi hapo?
 
Hongera sana kwa kimiliki duka kubwa la Hardware hapo Goba, ni kawaida ya wafanyabiashara wengi wa ngozi nyeusi hawapendi ushindani nakuhakikishia jiandae kwa fitina na majungu zaidi..

Msisitizo wangu tu kwako ni kumtegemea Mwenyezi Mungu kila siku..
 
Watanzania wenzangu tuwe na huruma, si kila aliyepata alipitia njia ya mkato wapo ambao wamehangaika usiku na mchana kufika walipo.
Nina ofisi ya hardware(vifaa vya ujenzi) kubwa tu hapa goba, nimehangaika nayo hii kuifokisha hapa ilipo kwa jasho.
Nakumbuka nilivyoteseka kuifikisha hapa ilipo, na ni mtaji mkubwa sana umelala hapo.
Hapo mwanzo wakati inaanza tulikuwa tunashirikiana sana Tena nathubutu kusema walinisaidia pia kupata connection kwa baadhi ya viwanda na kwa baadhi ya agents wakubwa wa viwanda.
Urafiki ulikuwa mzuri, Mimi sishindi Sana pale Ila kila nilipoenda lazima nisalimiane nao na kupiga story mbili tatu.
Sasa hivi Hali ni mbaya ni Kama tupo Vitani, Kuna kisa kimoja kilitokea Ila sikuwa najua kama pia inaweza kutufikisha hapa tulipo. Kuna kijana alikuwa kwenye hardware moja ambayo ni kubwa na ya miaka mingi, wakaja kushindana na mwenyewe, yule kijana akaja kuniomba kazi na kiukweli nilikuwa nahitaji kuongeza vijana maana walikuwa wapo wawili hivyo hawakutosha kabisa kutokana na kazi nyingi. Nikampa nafasi, we nilianza kununiwa na yule mzee wa kich......story zikaanza kuisha na kukoma kabisa.
Shughuli kubwa ikaja kwenye mauzo ya cement, Mimi nilipunguza 500 kutoka bei ya kawaida ambayo wengine pale wanauza.
Wakienda kwao hao wakishandana wanakuja kwangu nawauzia kwa kupunguza tena. Mfano; Kama watakuta huko ni 15000, wakija kwangu nawauzia kwa 14500.
Katika kuboresha zaidi biashara nikaona isiwe kesi ni vyema nikanunua gari ili wateja wapate nafuu zaidi kwa kuwa nawatoza bei ndogo kulinganisha na usafiri wa kukodi kwa wengine.
Nikanunua townace(Kaka yake kirikuu), nilinunua mil 11 mkononi lakini bado ilikuwa mpya na katika hali nzuri sana. Kijiweni wakichajiwa 40000, Mimi nawafanyia 30000. Hiyo ndio kazi ya gari, haitumiki kwa shughuli yoyote zaidi ya wateja wa hapa ofisini.
Chuki imekuwa kubwa hadi kwa watu wa kijiweni, eti najifanya mjuaji sana. Na yote hii imepandikizwa na hao wenzangu.
Sio Siri mzunguko wa biashara upo japo bado sijaridhika kwa kuwa eneo la kuhifadhi vitu(store) ni ndogo hivyo labda niwe na pesa nyingi ninunue eneo nijenge store nyingine(sidhani Kama ntaweza kwa kuwa ni ghali sana kumnunua Mtu eneo hilo).
Hakika watu ni wabaya sana, sasa hivi story zimeanza kugeuka kuwa natumia ndumba kijana mdogo, mara mwisho wake sio mzuri.
Hizi naambiwa na vijana wangu, maana wao wanaambiwa na vijana wa hao majirani.
Kuna surprise nimewaandalia hapo ili wateseke zaidi, mteja yoyote kija akanunua vitu kuanzia milioni 1 nampa taa moja ya bure (zile za 5000).
Relax focus on the business,hawa sio wa kuwaanzshia uzi.Ukiona umefanya hivo ujue lengo limefika.Na hao vijana wako waambie Sijawaajiri kwa ajili ya kuniletea maneno ya watu.Nataka mfanye kazi kama kazi imewashinda mnaleta umbeya tutshindwana.

Kama ni ndumba na wao wakatumie ndumba kwani shida iko wapi biashara ni ushindani.

Mkuu hakuna biashara RAHISI ili usiendekeze umbea umbea utachoshwa akili.
 
Watanzania wenzangu tuwe na huruma, si kila aliyepata alipitia njia ya mkato wapo ambao wamehangaika usiku na mchana kufika walipo.
Nina ofisi ya hardware(vifaa vya ujenzi) kubwa tu hapa goba, nimehangaika nayo hii kuifokisha hapa ilipo kwa jasho.
Nakumbuka nilivyoteseka kuifikisha hapa ilipo, na ni mtaji mkubwa sana umelala hapo.
Hapo mwanzo wakati inaanza tulikuwa tunashirikiana sana Tena nathubutu kusema walinisaidia pia kupata connection kwa baadhi ya viwanda na kwa baadhi ya agents wakubwa wa viwanda.
Urafiki ulikuwa mzuri, Mimi sishindi Sana pale Ila kila nilipoenda lazima nisalimiane nao na kupiga story mbili tatu.
Sasa hivi Hali ni mbaya ni Kama tupo Vitani, Kuna kisa kimoja kilitokea Ila sikuwa najua kama pia inaweza kutufikisha hapa tulipo. Kuna kijana alikuwa kwenye hardware moja ambayo ni kubwa na ya miaka mingi, wakaja kushindana na mwenyewe, yule kijana akaja kuniomba kazi na kiukweli nilikuwa nahitaji kuongeza vijana maana walikuwa wapo wawili hivyo hawakutosha kabisa kutokana na kazi nyingi. Nikampa nafasi, we nilianza kununiwa na yule mzee wa kich......story zikaanza kuisha na kukoma kabisa.
Shughuli kubwa ikaja kwenye mauzo ya cement, Mimi nilipunguza 500 kutoka bei ya kawaida ambayo wengine pale wanauza.
Wakienda kwao hao wakishandana wanakuja kwangu nawauzia kwa kupunguza tena. Mfano; Kama watakuta huko ni 15000, wakija kwangu nawauzia kwa 14500.
Katika kuboresha zaidi biashara nikaona isiwe kesi ni vyema nikanunua gari ili wateja wapate nafuu zaidi kwa kuwa nawatoza bei ndogo kulinganisha na usafiri wa kukodi kwa wengine.
Nikanunua townace(Kaka yake kirikuu), nilinunua mil 11 mkononi lakini bado ilikuwa mpya na katika hali nzuri sana. Kijiweni wakichajiwa 40000, Mimi nawafanyia 30000. Hiyo ndio kazi ya gari, haitumiki kwa shughuli yoyote zaidi ya wateja wa hapa ofisini.
Chuki imekuwa kubwa hadi kwa watu wa kijiweni, eti najifanya mjuaji sana. Na yote hii imepandikizwa na hao wenzangu.
Sio Siri mzunguko wa biashara upo japo bado sijaridhika kwa kuwa eneo la kuhifadhi vitu(store) ni ndogo hivyo labda niwe na pesa nyingi ninunue eneo nijenge store nyingine(sidhani Kama ntaweza kwa kuwa ni ghali sana kumnunua Mtu eneo hilo).
Hakika watu ni wabaya sana, sasa hivi story zimeanza kugeuka kuwa natumia ndumba kijana mdogo, mara mwisho wake sio mzuri.
Hizi naambiwa na vijana wangu, maana wao wanaambiwa na vijana wa hao majirani.
Kuna surprise nimewaandalia hapo ili wateseke zaidi, mteja yoyote kija akanunua vitu kuanzia milioni 1 nampa taa moja ya bure (zile za 5000).
Tatizo ni wewe mwenyewe, deal na mambo yako usipende kufikiria watu wanakuwazia nn! ''You must learn to ignore their words b'coz it won't degrade you but it degrade them and Forgive them for the love of God''.
 
Back
Top Bottom