Naona sasa tunazalisha Taifa la watetea watenda makosa!

Mkuu twende pamoja hapo pa kuonewa. Rugemalila na Seth wako ndani mpaka leo, je watu walioshirikiana nao toka ccm/ serikalini mbona hawapo ndani kama sio uonevu?
yawezekana wapo waliokula lakini kimaandishi hawaonekani. Km wao waliwagawia pesa Sasa mahakama itathibitishaje hapo
 
Dereva haji kuhojiwa bali anatakiwa ili atishiwe na kulishwa maneno. Lissu yupo hai yuko tayari kuhojiwa, mbona hatakiwi yeye?
Mwanzo kisingizio alikuwa anaumwa saikoloji,Lissu anambwela ni lini alikuja bongo tangu akimbie majukumu na wananchi wake!
 
Mkuu
Naona umelipwa Posho Ya eid elfitr Eeeh

Hivi kucheka picha ya ile suti Ya baba yako ile ya juu pima chini kadiria ni kosa????

Kucheka picha.. Narudi kucheka picha




Sent from my TECNO_W4 using JamiiForums mobile app
 
Pesa ya serikali itoke bila maandishi, unajua unachoongea boss?
Hukumbuki watu walivyobeba pesa kwenye sandarusi. Wewe nafikiri kwasababu wapo waliopata mgao ndo unahisi wanamakosa au la.. lazma uangalie mchakato wa kufanyika hilo dili liliratibiwa na nan. Aliyeratibu ndio tunamtaka
 
Kavunja sheria ipi?

Kacheka picha ya rais unaweza thibitisha ile ni picha ya Rais( mali ya jamhuri) au ni picha ya Magufuli
Mna uhakika wakati anacheka mbele ikiwepo hiyo picha alimaanisha kuidharau?

Mtu kucheka picha ni kosa?
Vipi mtu akiicheka noti ya fedha ya Tz ambayo ni mali ya jamhuri atakuwa amevunja sheria ya usalama wa Taifa 1970?

Mbona hashtakiwi?
 
Tusiwaangalie wakosoaji kama wakosaji pekee, tuangalie HAKI inatendeka vipi kwa wakosaji kwani kila mtu awe amekosea au hajakosea ana haki zake, watuhumiwa wako mahakamani upelelezi miaka na miaka hauishi, hiyo siyo haki lazima watu waseme. Watuhumiwa wako polisi na wamekamatwa na ushahidi lakini hawapelekwi mahakamani lazima watu waseme.

Hii unayofanya hapa wewe ndo mbaya kabisa kwani kwa kukaa kimya hawa watu watazidi kutuendesha watakavyo, ni lazima kila mtu afuate sheria, siyo kwa huyu ni sahihi, ila kwa yule jambo hilohilo siyo sahihi halafu unataka watu wakae kimya. Nasema HAPANA.
 
Naona hii tabia ya kutetea wanaokosea na zikichukuliwa hatua stahili.,
Wapo mapuruzai kibao wanajitokeza kutetea utopolo wa huyo mkosaji.

Tumeshuhudia hapa mafisadi,watakatisha pesa,wauza madawa ,yule mwandishi wote hawa walipata watetezi kwa makusudi kwa makusudi kutaka kuonyesha kama wanamkomoa mtu kumbe wanazidi kuchochea moto,

Hivi sasa kuna mmoja kafanya kosa la kucheka picha ya raisi bado kuna watu badala ya kujaribu kutoa rai kumshauri kijana asirudie makosa, kuna watu wanataka kufanya kama hakufanya kosa,

Kama hakudhamiria kwanini hakuchukua picha ya mzazi wake wa kike au kiume akaanza kucheka. lakini kwa kuchukua picha na kuanza kuidhihaki hapo ametumbukiza mguu wenye kiatu kwenye sufuria la ubwabwa lazima awatambue wenye shughuli ili kesho asirudie tena afunzwe sana!

Mtoto hakanywi akienda hukanywa akisharudi wakati yameshamkuta ya kumkuta!

Bakora haichagui pa kutua kwa mtoto mtukutu!
Hawata weza system iko imara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom