Naona giza nene maisha ninayopitia pamoja na ajira niliyonayo,ushauri wako ni muhimu.

The black day

Member
Oct 8, 2018
9
16
Miaka 30 ni umri wangu na nipi kwenye hii kazi ya ualimu kwa miaka 9 sasa.Lakini ndoto zangu zote nilizoziwaza za kimaendeleo hata robo hazijatimia zaidi ya kufanikiwa kuanzisha familia ambapo mpaka sasa nina mke na watoto wawili.

Ingawa kuna factors nyingi zinazonivuta nisifikie ndoto zangu mapema kama:-
1:Kuwa tegemeo pekee kwenye familia ya wazazi wangu ambapo tulizaliwa watoto 8 na mimi nikuwa wa 7/8 ingawa sasa tumebaki 6 kwani wengine walishaenda mbele ya haki na wenzangu wote ni wakulima tu wa kile kilimo kisichokuwa na tija na bado kuna mpwa niliyekuwa nikimsomesha aliyehitimu kidato cha 6 mwaka huu.
2:Mazingira duni ya kazi niliyopo ambayo si productive.
3:Mshahara duni.

Hatua nilizozichukua mara kadhaa kupunguza ukali wa maisha ni kukopa mkopo bank na kuanzisha kibiashara cha kioski ambapo mara kadhaa nilianguka na kuamka tena lakini mara ya mwisho nilikuja kuibiwa kila kitu nikabaki mweupe na deni la bank bado bichi kabisa.
Kilichopo sasa my take home salary ni 191,000.

Kutokana na hiki kipato changu cha sasa,ugumu wa kazi ulivyo na mazingira yake,utitiri wa majukumu na madeni naona kabisa itanichukua zaidi ya hata miaka 10 walau kufikia japo nusu ya ndoto zangu.

Ijapo lengo langu tangu mwanzo ilikuwa ualimu utakuwa daraja tu lakini kumbe nimetumbukia.

Zaidi ya ualimu:
1.Ni MC ila mazingira yananifelisha maana nipo kijijini sana na ndoto yangu ni kuwa iwe kazi yangu rasmi.
2.Nimeandika kitabu cha kiingereza ambacho naamini kitakuwa ni muarobaini wa tatizo la ufundishaji wa lugha hii kwa walimu wa shule za msingi na ujifunzaji wa wanafunzi wanaojiandaa na mtihani wa drs la 7 maana kipo full nondo ingawa ndo nimemaliza tu kukiandila,nilifikia hatua ya kuwaza wazo hili pengine kwa uzoefu na ujuzi nilionao katika somo hili ninaweza fanya kitu cha kuniingizia kipato.
3:Ni mtunzi mzuri wa mashairi na nyimbo za kisasa na hata kuimba ingawa sijawa na ujasiri wa kuamua kurekodi nyimbo.

Shida iliyopo naiona kazi ni chungu na ninatamani kuiacha ili nifanye shughuli hizo ila tena nikifikiria kiacha wakati bado sina mtaji nina hofu pengine halu ya maisha inaweza kuwa mbaya zaidi ya hapa maana hata kipato ninachokipata kwa sasa naishia kulipa madeni ya watu binafsi.

Anyway,najua wapo watakaonikejeli lakini kumbuka hili ni tatizo kwangu na ninahitaji msaada wa kipi nifanye au nijilipue wapu ili walau nami siku nufurahie haya maisha.
 
Usikate tamaa. Hujatuambia shemeji yetu anafanya nini. Maisha ni kusaidiana, usiache kazi kwa sasa, kama shem sio muajiriwa, mfungulie hata genge(wengine huita "bao") la bidhaa muhimu za chakula, na wewe fungua bustani ya mbogamboga.
Mwanzo utaona bado shida, but baadae utaona nafuu hasa utakapoanza kuvuna mbogamboga.
Usitake makubwa wakati hali hairuhusu.
Na ule mchepuko wako upunguze dau la kumpa. Tchao
 
Pole kwa yanoyokusibu amini haupo peke yako wapo wengi tu kwenye jamii wengi hawana ujasiri wa kusema hadharani kama wewe.
Nachokushauri kuendelea kushikilia kazi ili hali unazidi kuumia haitakusaidia, jiamini mwenyewe na ufanye maamuzi magumu.
 
Pole mtoa mada.....maisha yetu Walim sana tena yana staajabisha kikubwa endelea kuvumilia na kupambna tena ikiwezekana Fanya figisu zote utoke huko kijijini iwe kwa kuhama au ruhusa ya kwenda masomoni na ukifika kwenye mji hutakosa cha kufanya.... Kinachouma zaidiii Mwl anaeishi kijijini ambako Hakuna fursa anaishi kwa dhiki kuliko wa mjini.
 
Pole mtoa mada.....maisha yetu Walim sana tena yana staajabisha kikubwa endelea kuvumilia na kupambna tena ikiwezekana Fanya figisu zote utoke huko kijijini iwe kwa kuhama au ruhusa ya kwenda masomoni na ukifika kwenye mji hutakosa cha kufanya.... Kinachouma zaidiii Mwl anaeishi kijijini ambako Hakuna fursa anaishi kwa dhiki kuliko wa mjini.
Ni sahihi unachosema mkuu,kuna vijiji vingine kweli si haba unaweza fanya chochote cha kupunguza vitu lakini kiukweli hiki kijiji nilichopo is totally unproductive,ningekuwa mjini hata tuition ningegonga sana.
 
Usikate tamaa. Hujatuambia shemeji yetu anafanya nini. Maisha ni kusaidiana, usiache kazi kwa sasa, kama shem sio muajiriwa, mfungulie hata genge(wengine huita "bao") la bidhaa muhimu za chakula, na wewe fungua bustani ya mbogamboga.
Mwanzo utaona bado shida, but baadae utaona nafuu hasa utakapoanza kuvuna mbogamboga.
Usitake makubwa wakati hali hairuhusu.
Na ule mchepuko wako upunguze dau la kumpa. Tchao
Sheme
Usikate tamaa. Hujatuambia shemeji yetu anafanya nini. Maisha ni kusaidiana, usiache kazi kwa sasa, kama shem sio muajiriwa, mfungulie hata genge(wengine huita "bao") la bidhaa muhimu za chakula, na wewe fungua bustani ya mbogamboga.
Mwanzo utaona bado shida, but baadae utaona nafuu hasa utakapoanza kuvuna mbogamboga.
Usitake makubwa wakati hali hairuhusu.
Na ule mchepuko wako upunguze dau la kumpa. Tchao
Mkuu,shemeji yenu nilimfungulia kiduka lakini walikuja kuiba kila kitu
 
Kwanza kabisa nikupe hongera kwa kukomaa ndugu. Ingawaje sina ushauri ila naomba nikutie moyo tu kuwa kuna siku utatimiza ndoto zako....hold on to them tight and make sure they are SMART Specific Measurable Attainable Relevant Time-bound
 
Walimu wa vijijini niano wajua mimi ambao ndio wamenifundisha miaka ya wana maisha mazuri sana kukiko raia yeyote katika vijiji! Na wamejenga majumba mazuri, wanalima, wanafuga.. Kuwepo kwao kijijini ni fursa. Ukifika kijijini ukioneshwa nyumba ya mwalimu unasema yes ualimu dili.

Lakini nyie walimu wa wa miaka hii ya 2000s sijui mnashida gani?
 
Sheme

Mkuu,shemeji yenu nilimfungulia kiduka lakini walikuja kuiba kila kitu
Uko kijijini fuga kuku wa kienyeji anzia 10 au 20.tumia njia ya kawaida yan wajitafutie chakula, baada ya miezi 8 utaanza biashara ya kuuza mjini kwa gape la miezi 4 mi 4.unaweza usitumie tena mshahara wako kwa mahitaji ya familia, pia uwe na matumizi kulingana na uwezo wako.
 
Pole sana ndugu.

Hayo ndio maisha, mshukuru Mungu kwamba pamoja na changamoto unazoziona walau una kazi ya kukufanya uwe busy kwa muda fulani na kusahau kidogo changamoto zako.

Kuna wengi tunakaangwa huku hata hiyo laki hatujui kama tutakuja kuiona tena toka tutumbuliwe.

Wakati mwingine katika maisha, mambo huenda kombo kiasi kwamba mbele huwa na giza nene la kutisha na kutupotezea matumaini kabisa.

Nini ufanye;

1. Usiache kazi kabla hujapata kazi.

2. Hebu jaribu kubadiri mtazamo katika kazi yako. Anza kuipenda na kujituma kwa nguvu zako zote. Chukulia hilo ndio boya pekee ulilorushiwa majini ujiokoe...kwamba ukiliachia umekwisha.

3. Wakati unatekeleza hayo niliyosema kwenye namba 2. Tanguliza na ongeza upendo kwa walimu wenzio na wafanyakazi, penda wanafunzi, wazazi na hata wanakijiji mnapokutana mtaani baada ya kazi.

4. Wasaidie kwa moyo wote walimu wenzio katika utendaji wa kazi pale wanapokwama kwa kuwaelekeza wafanye nini. Usionyeshe maringo au kujivuna kwa kile unachokijua.

5. Saidiana na walimu wenzio kubuni na kupanga mikakati ya kuongeza ufaulu na kama vipi jitolee kufuatilia kutimiza mikakati yenu.

6. Onyesha ushirikiano wa juu mnapotembelewa na wageni mbalimbali hapo shuleni hasa wakaguzi na viongozi. Pia uwe mwepesi wa kutetea zaidi kuliko kuchongelea.

Umeelewa maana ya ushauri wangu huo hapo juu?? Kama hujaelewa basi ni hivi;

1. Siku zote fursa hujitokeza pale tu unapojituma na kuipenda kazi unayoifanya

2. Jamii inayokuzunguka ina nafasi ya kwanza kusambaza cv yako ya ukweli iwe mbaya au nzuri bila kujali uko shimoni kiasi gani. Fursa zitakutafuta na kukufuata hadi ulipo na kukunyakua

3. Kuyatekeleza hayo niliyo kwambia ni rahisi maana yako ndani ya uwezo wako na hautahitaji mkopo au mtaji kuyafanya. Anza kesho usisubiri, chukulia ndio fursa hiyo na ninakuhakikishia itakutoa

4. Hivi sasa kuna rundo la walimu wabovu wasio ipenda kazi, wanaifanya tu basi kwasababu hawanajinsi na hailipi. Kwako wewe chukulia hiyo fursa. Kuna uhaba mkubwa wa walimu bora. Weka malengo ya kuwa mwalimu bora kabisa. Watakufata, utaanzia ualimu wa somo, nidhamu na bidii, baadae utaanza kusimamia zamu. Utaanza kumsaidia majukumu mwalimu mkuu kutokana na kujituma kwako na uaminifu. Mwisho mwalimu mkuu msaidizi. Mara afisaelimu au mratibu kakuona....huyoo...wilayani.....mkoa. ukifika mkoa sasa ndio kwenyewe katika ku-make money....utapata mpaka connections za kuchapisha kitabu chako kikapata na EMAC ukapiga mpunga

5. Amini nakuambia, ukifuata hiyo mikakati basi miaka minne tu ijayo as maximum. Wewe si mwenzetu tena.

MWISHO:
Unapoyafanya hayo yote usiache kumuomba Mungu wa imani yako, japo usiingie sana kweye ufia dini. Hata hapo home au ofisini "Omba Mungu abariki mipango yako kila unapokumbuka na kupata nusu dakika ya kumuomba Mungu" kimya kimya kimoyomoyo hata sikio lako la kushoto lisisikie.

Kila la Kheri Ndugu!
 
Pole sana mkuu, usikate tamaa na hongera sana kwa kufunua yaliko moyoni mwako binafsi ningeomba ujaribu kuainisha yaliyo matamanio yako hata tujue pa kuanzia kukushauri kwa urahisi
 
pole mkuu...
mtazamo wako ndio kikwazo wala siyo kazi, wala kijiji ulichopo...
ngoja namalizia glass ya maziwa ntarudi
 
Upo kijiji gani na kuna shughuli gani za kiuchumi unaona zikifanyika
 
Pole sana mkuu, usikate tamaa na hongera sana kwa kufunua yaliko moyoni mwako binafsi ningeomba ujaribu kuainisha yaliyo matamanio yako hata tujue pa kuanzia kukushauri kwa urahisi
Thanks mkuu,ndoto yangu kuu ni kujiajiri kupitia kilimo cha kisasa na ufugaji lakini kwa kuanzia nijiajiri kwanza kwenye ushereheshaji na zaidi nichape kitabu changu.
 
Pole sana ndugu.

Hayo ndio maisha, mshukuru Mungu kwamba pamoja na changamoto unazoziona walau una kazi ya kukufanya uwe busy kwa muda fulani na kusahau kidogo changamoto zako.

Kuna wengi tunakaangwa huku hata hiyo laki hatujui kama tutakuja kuiona tena toka tutumbuliwe.

Wakati mwingine katika maisha, mambo huenda kombo kiasi kwamba mbele huwa na giza nene la kutisha na kutupotezea matumaini kabisa.

Nini ufanye;

1. Usiache kazi kabla hujapata kazi.

2. Hebu jaribu kubadiri mtazamo katika kazi yako. Anza kuipenda na kujituma kwa nguvu zako zote. Chukulia hilo ndio boya pekee ulilorushiwa majini ujiokoe...kwamba ukiliachia umekwisha.

3. Wakati unatekeleza hayo niliyosema kwenye namba 2. Tanguliza na ongeza upendo kwa walimu wenzio na wafanyakazi, penda wanafunzi, wazazi na hata wanakijiji mnapokutana mtaani baada ya kazi.

4. Wasaidie kwa moyo wote walimu wenzio katika utendaji wa kazi pale wanapokwama kwa kuwaelekeza wafanye nini. Usionyeshe maringo au kujivuna kwa kil

Nashukuru mkuu kwa ushauri wako.
 
Back
Top Bottom