Dunia imesimama na Rais Samia Suluhu Hassan hoja ya Teenage Mothers

unajua hii concept wengi sana inawachanganya..

tumeruhusu wajawazito kurudi shule sawa inawezekana ni uamuzi mzuri, lakini je ni sawa kwa binti mdogo mwanafunzi kupewa ujauzito na kuzalishwa au kufanya ngono?..... hapa ndio kwenye concept na failure za wasomi wetu...

Juhudi gani kali tumefanya sasa kuwalinda hawa mabinti na ujauzito na kufanya haya matukio kuwa negligible.......iko wapi mikakati kutoka ustawi wa jamii, elimu, mambo ya ndani nk kuhakikisha hawa mabinti wanakuwa salama katika kila nyanja kuanzia kitabia na kimaadili..?
Mimba za watoto wa shule na umaskini ni pacha. Kupunguza hili tatizo lazima na umaskini upungue
 
Kama wameruhusu ningependa na wale wanaowapa mimba wapewe adhabu ndogo ili kulinda ustawi wa mtoto asiye na hatia...
Baba gerezani na mama yuko shule, huyo mtoto ataanza kufunzwa na ulimwengu mapema sana.
 
unajua hii concept wengi sana inawachanganya..

tumeruhusu wajawazito kurudi shule sawa inawezekana ni uamuzi mzuri, lakini je ni sawa kwa binti mdogo mwanafunzi kupewa ujauzito na kuzalishwa au kufanya ngono?..... hapa ndio kwenye concept na failure za wasomi wetu...

Juhudi gani kali tumefanya sasa kuwalinda hawa mabinti na ujauzito na kufanya haya matukio kuwa negligible.......iko wapi mikakati kutoka ustawi wa jamii, elimu, mambo ya ndani nk kuhakikisha hawa mabinti wanakuwa salama katika kila nyanja kuanzia kitabia na kimaadili..?
Nadhani hii ndio hoja ya msingi zaidi.

Kwanza ziwekwe seria kali za kulinda hawa mabinti zetu na watoto wetu wa kike na kiume waliopo shule wapewe elimu ya uzazi mapema sana.

Tatizo la msingi nadhani linaanzia kwenye familia zetu, Je sisi kama wazazi tunaongea na binti zetu au watoto wetu wa kiume kuhusu elimu ya uzazi?

Pia sheria zetu zingejikita kwenye kushawishi na kufanya ngono na mtoto under 18 liwe ni kosa la jinai kabisa na mtu akikutwa aadhibiwe kama waingereza wanavyofanya.

So far ni vizuri kurudisha watoto waliopata ujauzito shuleni ila sheria zetu bado haziwalindi hawa mabinti wetu.
 
Hebu toa sababu kwanini mliwazuia wasirejee shuleni baada ya kuzaa
1.hawakuzuiwa wasirejee shuleni waliruhusiwa kusoma kwenye shule za private za ufundi na mambo mengine ya kijamii
2.funzo kwa wanafunzi wengine kutopata ujauzito wakiwah shuleni.
3. Kuwapa mda wa kulea na kuwatunza watoto wao vizuri
4. Kuwapunguzia mzigo wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja na kuepusha mzigo kwa wanafamilia
 
Nadhani hii ndio hoja ya msingi zaidi.

Kwanza ziwekwe seria kali za kulinda hawa mabinti zetu na watoto wetu wa kike na kiume waliopo shule wapewe elimu ya uzazi mapema sana.

Tatizo la msingi nadhani linaanzia kwenye familia zetu, Je sisi kama wazazi tunaongea na binti zetu au watoto wetu wa kiume kuhusu elimu ya uzazi?

Pia sheria zetu zingejikita kwenye kushawishi na kufanya ngono na mtoto under 18 liwe ni kosa la jinai kabisa na mtu akikutwa aadhibiwe kama waingereza wanavyofanya.

So far ni vizuri kurudisha watoto waliopata ujauzito shuleni ila sheria zetu bado haziwalindi hawa mabinti wetu.
Umeongea ya muhimu sana mkuu
 
1.hawakuzuiwa wasirejee shuleni waliruhusiwa kusoma kwenye shule za private za ufundi na mambo mengine ya kijamii
2.funzo kwa wanafunzi wengine kutopata ujauzito wakiwah shuleni.
3. Kuwapa mda wa kulea na kuwatunza watoto wao vizuri
4. Kuwapunguzia mzigo wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja na kuepusha mzigo kwa wanafamilia
Kwahiyo mlijigeuza watetezi wao,

Wapi walisema hawayawezi hayo?
 
Kila mwaka zaidi ya wasichana 6,500 wakiTanzania waliachishwa|walifukuzwa shule kwasababu ya kupata ujauzito wakiwa shuleni,

Mwaka 2017 aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt John John Joseph Pombe Magufuli kwa kutumia nguvu ya Rais alikataa watoto hawa kuendelea na masomo.

Benki ya Dunia ikatunyima fedha kiasi cha $300M karibu TZS 690BL baada ya kiongozi mkuu wa ACT-Wazalendo Mhe Zitto Zuberi Kabwe kuwataka wafanye hivyo,

Je kulikuwa na haja kwa Hayati Rais Magufuli kufanya hayo?

Sote tunafahamu,Mimba sio ugonjwa, Mimba sio kilema,Mimba sio laana ,Mimba ni dalili ya ukamilifu na utimilifu wa kizazi cha mwanamke,

Lakini pia, Mimba ni baraka ya Uzao toka kwa Mungu iweje iwe laana?

Kwamtazamo wangu,awamu zilizopita zilimchukulia Mwanafunzi aliyepata mimba akiwa shuleni kitofauti sana
1. Zilidhani kupata mimba shuleni ni laana toka kwa Mungu na Wanadamu,

2. Zikamwona kama ni mtoto asiyefaa tena kuishi duniani

3. Zikafikiri ni mtoto asiyetakiwa kupata elimu tena utadhani mimba inafuta kumbukumbu,

4. Zikamwona kama malaya na huenda akipewa nafasi nyingine ya kuendelea na masomo atasambaza tabia hiyo mbaya kwa wanafunzi wengine,

5. Ziliamini kabisa ni mtoto asiyevumilika tena katika kuendelea na masomo yake,

Zitto Kabwe na baadhi ya Wabunge wa CHADEMA kama Esther Matiko na Halima James Mdee pamoja na wanaharakati wengine nguli wa kimataifa kama Maria Tsesai Sarungi na Shangazi Fatuma Karume na wengime wengi,

Watu hawa Wote kwa pamoja, walimpinga Hayati Dkt John John Joseph Pombe Magufuli kwa nguvu na kwaakili zao zote,

Wakati huohuo wakiziandikia taasisi mbalimbali za kimataifa hasa UNESCO|SIDA|IMF|WB zisitishe misaada na mikopo ya masharti nafuu kwa Tanzania kwa kukiuka haki hii ya Watoto,

Kwanini tusimpongeza Rais Samia kwa hili
Leo kwa mara ya kwanza toka kwa Rais wa kwanza mwanamke anayetambua kwa mifano kuwa "Mimba si laana wala mimba sio kilema cha akili"

Rais Samia tayari amerejesha furaha iliyopotea kwa miongo mingi kwa waathirika hawa wa mimba za mashuleni,

Leo haijalishi mimba mwanafunzi kaipataje iwe ni kwakubakwa au kurubuniwa cha kwanza mtuhumiwa atakwenda jela miaka thelathini,

Kisha mwanafunzi huyu baada ya kujifungua mtoto atarejea Shuleni kuendelea na masomo kama kawaida,

Tunaposema Rais Samia ni mteule wa Mungu tunamaana hii kwani hakuna mtimilifu mbele zake,

Hebu chukua huu mfano
Martha Karua mwanasiasa nguli tena mwenye ushawishi mkubwa nchini Kenya,

Martha ndiye anayetarajiwa kuwa Mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais kwenye Uchaguzi Mkuu Ujao wa Kenya wa mapema 2022,

Ningumu kuamini ila mama huyu ni muhanga wa "Mimba za Shuleni " aliyepewa nafasi ya pili kuendelea na masomo yake,

Kwa msiofahamu,
Kenya imekuwa na ruhusu kwa Wale wanaopata mimba shuleni kurejea na kuendelea na masomo yao baada ya kujifungua,

Nakwamantiki hii,Huenda Kenya ikapata Makamu wa Rais aliyepewa mimba akiwa bado shuleni,

Tunamengi ya kujifunza ila kwa sasa pongezi nyingi zimfikie Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutambua kuwa mimba sio laana bali ni baraka toka kwa Mungu.
Safi sana! Una Big Vision sana wewe!
 
Kila mwaka zaidi ya wasichana 6,500 wakiTanzania waliachishwa|walifukuzwa shule kwasababu ya kupata ujauzito wakiwa shuleni,

Mwaka 2017 aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt John John Joseph Pombe Magufuli kwa kutumia nguvu ya Rais alikataa watoto hawa kuendelea na masomo.

Benki ya Dunia ikatunyima fedha kiasi cha $300M karibu TZS 690BL baada ya kiongozi mkuu wa ACT-Wazalendo Mhe Zitto Zuberi Kabwe kuwataka wafanye hivyo,

Je kulikuwa na haja kwa Hayati Rais Magufuli kufanya hayo?

Sote tunafahamu,Mimba sio ugonjwa, Mimba sio kilema,Mimba sio laana ,Mimba ni dalili ya ukamilifu na utimilifu wa kizazi cha mwanamke,

Lakini pia, Mimba ni baraka ya Uzao toka kwa Mungu iweje iwe laana?

Kwamtazamo wangu,awamu zilizopita zilimchukulia Mwanafunzi aliyepata mimba akiwa shuleni kitofauti sana
1. Zilidhani kupata mimba shuleni ni laana toka kwa Mungu na Wanadamu,

2. Zikamwona kama ni mtoto asiyefaa tena kuishi duniani

3. Zikafikiri ni mtoto asiyetakiwa kupata elimu tena utadhani mimba inafuta kumbukumbu,

4. Zikamwona kama malaya na huenda akipewa nafasi nyingine ya kuendelea na masomo atasambaza tabia hiyo mbaya kwa wanafunzi wengine,

5. Ziliamini kabisa ni mtoto asiyevumilika tena katika kuendelea na masomo yake,

Zitto Kabwe na baadhi ya Wabunge wa CHADEMA kama Esther Matiko na Halima James Mdee pamoja na wanaharakati wengine nguli wa kimataifa kama Maria Tsesai Sarungi na Shangazi Fatuma Karume na wengime wengi,

Watu hawa Wote kwa pamoja, walimpinga Hayati Dkt John John Joseph Pombe Magufuli kwa nguvu na kwaakili zao zote,

Wakati huohuo wakiziandikia taasisi mbalimbali za kimataifa hasa UNESCO|SIDA|IMF|WB zisitishe misaada na mikopo ya masharti nafuu kwa Tanzania kwa kukiuka haki hii ya Watoto,

Kwanini tusimpongeza Rais Samia kwa hili
Leo kwa mara ya kwanza toka kwa Rais wa kwanza mwanamke anayetambua kwa mifano kuwa "Mimba si laana wala mimba sio kilema cha akili"

Rais Samia tayari amerejesha furaha iliyopotea kwa miongo mingi kwa waathirika hawa wa mimba za mashuleni,

Leo haijalishi mimba mwanafunzi kaipataje iwe ni kwakubakwa au kurubuniwa cha kwanza mtuhumiwa atakwenda jela miaka thelathini,

Kisha mwanafunzi huyu baada ya kujifungua mtoto atarejea Shuleni kuendelea na masomo kama kawaida,

Tunaposema Rais Samia ni mteule wa Mungu tunamaana hii kwani hakuna mtimilifu mbele zake,

Hebu chukua huu mfano
Martha Karua mwanasiasa nguli tena mwenye ushawishi mkubwa nchini Kenya,

Martha ndiye anayetarajiwa kuwa Mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais kwenye Uchaguzi Mkuu Ujao wa Kenya wa mapema 2022,

Ningumu kuamini ila mama huyu ni muhanga wa "Mimba za Shuleni " aliyepewa nafasi ya pili kuendelea na masomo yake,

Kwa msiofahamu,
Kenya imekuwa na ruhusu kwa Wale wanaopata mimba shuleni kurejea na kuendelea na masomo yao baada ya kujifungua,

Nakwamantiki hii,Huenda Kenya ikapata Makamu wa Rais aliyepewa mimba akiwa bado shuleni,

Tunamengi ya kujifunza ila kwa sasa pongezi nyingi zimfikie Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutambua kuwa mimba sio laana bali ni baraka toka kwa Mungu.
Unaweza kutukumbusha mwaka gani nchi hii watoto wa kike waliopata ujauzito wakirejea mashuleni?
Zile harakati za kupima mimba mashuleni zilikuwa kwaajili gani? Zilianza lini na zilikoma lini?
Kikwete aliwahi kusema watoto wa kike kubeba mimba ni kiherehere Chao
Magufuli akamalizia kabisa kusema hasomeshi wazazi shule za umma.
Wazazi wanaojitambua hawakumuacha mtoto wao aliezaa abaki nyumbani Bali walikuendeleza lakini sio shule za umma na hakukuwa na zuio hata Mara moja.
Kufanikiwa kuacha siasa za watu na kuyajadili maslahi mapana ya taifa hili itakuwa hatua kubwa sana kwa nchi yetu.
 
Zanzibar imo nchini Tanzania na inatumia mfumo wa elimu ya Tanzania lakini wasichana waliopata mimba huruhusiwa kuendelea na masomo wakijifungua! Mapacha wangu Kulwa ni wa kichina na Doto wa kisomali!
Zanzibar sio Tanzania
 
Juhudi zimefanyika na nikubwa sana, Ukitaka kujua wewe mpe Mwanafunzi mimba ndio utaziona juhudi za Serikali,
Juhudi za kusubiria tatzo ndio mchukue hatua? Hizi sio hatua effective inatakiwa serikali na jamii ije na hatua mbadara za kuzuia mimba kabla haijatokea sio kusubiria tatzo litokee Ndio mchukue hatua tena hatua zenyewe zinaweza leta chuki kwa mzazi mtoto.
 
Juhudi za kusubiria tatzo ndio mchukue hatua? Hizi sio hatua effective inatakiwa serikali na jamii ije na hatua mbadara za kuzuia mimba kabla haijatokea sio kusubiria tatzo litokee Ndio mchukue hatua tena hatua zenyewe zinaweza leta chuki kwa mzazi mtoto.
Toa way forwards
 
Unaweza kutukumbusha mwaka gani nchi hii watoto wa kike waliopata ujauzito wakirejea mashuleni?
Zile harakati za kupima mimba mashuleni zilikuwa kwaajili gani? Zilianza lini na zilikoma lini?
Kikwete aliwahi kusema watoto wa kike kubeba mimba ni kiherehere Chao
Magufuli akamalizia kabisa kusema hasomeshi wazazi shule za umma.
Wazazi wanaojitambua hawakumuacha mtoto wao aliezaa abaki nyumbani Bali walikuendeleza lakini sio shule za umma na hakukuwa na zuio hata Mara moja.
Kufanikiwa kuacha siasa za watu na kuyajadili maslahi mapana ya taifa hili itakuwa hatua kubwa sana kwa nchi yetu.
Umeandika vizuri ila hausomeki mkuu wangu
 
Back
Top Bottom