Naombeni wenye kujua haya mambo, naona kama nina kitu Cha kipekee

Midazolam

JF-Expert Member
Aug 15, 2020
806
1,337
Wajuzi wa mambo haya,

Naomba nirudi nyuma kidogo,nilikuwa mdogo bado nina kumbukumbu yapata miaka 29 nyuma. Nilikuwa na uwezo wa kuona vitu au kitu kibaya,au kujua ni lini tutapata wageni na nilikuwa nikimwambia mama,

Mamangu ni mwana maombi sana na maombi yake juu yetu ni kama umetufunika na ulinzi Fulani maana alikuwa ananitamkia hata kipindi naenda kusoma mbali alikuwa akisema maneno Fulani kufika kule naona kama vile au nitapokelewa Fulani hivi shuleni na kupendwa sana na hata kipindi nakosa chakula pale shuleni kutokana na shule zetu za bweni mnafahamu kama huna nguvu utateseka sana,ila ilichukua miezi kadhaa,na nilikuwa natoroka na kwenda vijini vya karibu na nitapewa chakula huko na kurudi nikiwa safi,

Mamangu alikuwa na utaratibu wa kuleta wana maombi nyumbani kwetu na tulikuwa wale walokole kweli kweli.Hapo ndo niliposikia sauti kwenye ndoto kuwa mbona hutaki kuokoka na wewe piga Magoti uokoke,nikawa mgumu kidogo nikaona kama nguvu Ile ni kubwa nikalipuka pale Moja kwa Moja na kusema Nahitaji kuokoka na kupiga Magoti na kuongozwa maneno siku hiyo hiyo,

Baada ya hapo niliishi kwenye huo ulokole ila nilikuja kutereza kutokana na hizi shule zetu za mbali ,ila Kila nikipita karibu na kanisa,huwa nilikuwa naumia sana kwa nini Mimi sijaenda kanisani,hiyo hali na hiyo nguvu iliendelea kunitesa moyo hivyo,

Na kipindi nikianza kusoma biblia huwa najihisi nguvu Fulani hivi ya kuona vitu kwa watu wengine,

Na hii ndo inanitesa zaidi naweza kupanda daladala nikiwa kwenye mizunguko yangu au wakati wa kwenda kazini nikahisi mbele Kuna ajali na nikifika mbele naona ajali,imekuwa ikiniongoza hivyo ,au nitapanda gari konda asinidai au labda nikikumbuka Huwa Nampa au nisilipe,au naweza kula mgahawani na nikalipa ela na kurudishiwa chenji zaidi Kuna mda narudisha na Kuna mda nakuwa Sina ela nakaa kimya,

Pia naweza kumuona mtu nikamwambia ukweli juu ya jambo analopitia,na nimekuwa nikimwambia mwanamke ambaye nipo naye kwa harakati ya kutaka kumuoa na amekuwa akiniamini sana kutokana na Mimi kumwambia mambo ya familia yake na mpaka nimekuwa nikimwambia ukweli na hata kumwambia hujawahi kuingiliwa na mwanaume hapo ndo alibaki kuwa hoi nikaja kumwambia kuhusu mamake na wadogo zake na kaka yake,

Na hii jambo imekuwa nikijihisi kuwa Kuna nguvu Fulani nyuma yangu ,na hii ya kuona ajali imekuwa ikinisumbua sana maana nimekuwa najitahidi kuikemea sana lakini naona Bado,na kwa sasa naona hii nguvu inanituma sana kuwaombea wagonjwa maana nafanya kazi kwenye hospitali na hii nguvu inazidi kuwa kubwa.

Kuna rafiki yangu alinidhulumu ela zangu na kushirikiana na mchumba ambaye nilitaka kumuoa nilisema maneno machache tu juu Yao, walipata ajali mwendelezo na kupita wakati mgumu sana,na Bado wanaoitishwa kwenye moto huo huo ,

Naombeni kama Kuna watu wa mambo ya kiroho kuhusu mambo haya najiona wa tofauti sana
 
Back
Top Bottom