Naombeni ushauri....!!!

cashmoney

Member
Dec 14, 2011
89
30
Habari wakuu..!!
Kifupi nina shida na uhitaji wa kupata mtaji wa kuendesha biashara yangu (operating capital). Nina kampuni changa ya microcredit activities (utoaji wa huduma za mikopo) ambayo nimeisajili na kuianzisha tangu mwaka 2011. Mwaka 2012 nilitarajia kuanza kutoa huduma lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu na imenichukua takribani mwaka sasa nimejaribu kuhangaika kupata mtaji niendelee na biashara hii. Nina ka nyumba ka urithi (ingawa mzazi bado yupo hai) ambacho Bi mkubwa (mama) alinishauri either nikaombee mkopo benki, ktk taasisi za kifedha au kwa mtu binafsi au kuiuza nipate mtaji, lakini nimejaribu kufuatilia njia hizo hadi sasa bilabila. Ktk taasisi za kifedha na mabenki wameniambia inatakiwa uzoefu wa kuendesha biashara hiyo usiopungua miezi sita hadi mwaka. Kuna threads ktk jukwaa la matangazo madogomadogo nilipost humu JF tangu miezi sita iliyopita kuhusu kuuza nyumba hiyo lakini sijafanikiwa kupata mteja hadi leo (hata wa kwenda kuiona tu sijampata). Mda unavyozidi kwenda akili inazidi kunipelekesha nikiwazua namna ya kufanikisha lengo langu. Nimeshachoma meli moto (nimeachana na kazi zangu za kuajiliwa tangu mwaka juzi) lakini changamoto ni nyingi mno. Ufupi naombeni ushauri nifanyeje kufanikisha mpango huu maana mwaka ndo huu unakatika na sijui hata niweke mikakati gani kwa ajili ya mwakani.
Natanguliza shukrani.
 
iyo ni nyumba ya familia na sio urithi kama ulivyosema unaweza kuitumia kuombea mkopo bank.
 
iyo ni nyumba ya familia na sio urithi kama ulivyosema unaweza kuitumia kuombea mkopo bank.

Ni nyumba yangu ya urithi na si ya familia kama unavyong'ang'ania. Na kuhusu kuombea mkopo bank kwangu ktk hali niliyonayo kibiashara ni ngumu kama nilivyoeleza hapo juu, kuwa kampuni yangu yenyewe ni ya kutoa mikopo na sina experience ya operations za kutoa huduma, nimeshajaribu bank zote wameniambia niwe na experience isiyopungua miezi sita au mwaka ya utoaji huduma maana kwa sasa ndo naanza (start up).
 
Hongera kwa kuwa na Mawazo ya kujitegemea.

1. Biashara yako ina vibali vyote halali?

2. Unaweza kuandika andiko linoonyesha kuwa ukipewa fedha itaweza kurudi. (Kwamba mradi utarudisha pesa)

3. Unataka Hiyo pesa kwa ulipe kwa utaratibu upi, kwa mwezi ama?

4. Una mdhamini ama dhamana kwa hiyo pesa unayotaka kukopeshwa?

Nijibu hapo then I will see the best way we can assist.
 
Changamoto ndiyo kipimo cha akili komaa na wazo lako ukishinda changa moto ndiyo umeshinda mtihani wa maisha.
kuwa mwangalifu na majibu yako wengine wanapima akili yako ili pengine akupe msaada wewe unajibu vibaya wote watakupuuza mfano :umesema UNANG'ANG'ANIA
 
Hongera kwa kuwa na Mawazo ya kujitegemea.

1. Biashara yako ina vibali vyote halali?

2. Unaweza kuandika andiko linoonyesha kuwa ukipewa fedha itaweza kurudi. (Kwamba mradi utarudisha pesa)

3. Unataka Hiyo pesa kwa ulipe kwa utaratibu upi, kwa mwezi ama?

4. Una mdhamini ama dhamana kwa hiyo pesa unayotaka kukopeshwa?

Nijibu hapo then I will see the best way we can assist.

1. ndio biashara ina vibali vyote
2. ndio naweza andika
3. nitakuwa natoa mikopo kwa wafanyakazi ambao muajiri wao atakuwa tayari kuwadhamini ili marejesho yatoke ktk makato ya mishahara yao. mikopo itatolewa kuanzia kipindi cha mwezi mmoja hadi miezi 12.
4. nitaweka nyumba kama dhamana
 
Umesema vema mkuu! Huyu jamaa inabidi achunge sana asiingiwe na hasira katika utoaji wa majibu yake wakati anaulizwa.
Changamoto ndiyo kipimo cha akili komaa na wazo lako ukishinda changa moto ndiyo umeshinda mtihani wa maisha.
kuwa mwangalifu na majibu yako wengine wanapima akili yako ili pengine akupe msaada wewe unajibu vibaya wote watakupuuza mfano :umesema UNANG'ANG'ANIA
 
1. ndio biashara ina vibali vyote
2. ndio naweza andika
3. nitakuwa natoa mikopo kwa wafanyakazi ambao muajiri wao atakuwa tayari kuwadhamini ili marejesho yatoke ktk makato ya mishahara yao. mikopo itatolewa kuanzia kipindi cha mwezi mmoja hadi miezi 12.
4. nitaweka nyumba kama dhamana
Mkuu ni mtaji kiasi gani unahitajika ili kuanzisha hii biashara
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom