Naombeni ushauri wenu na masahada tafadhali juu ya Swala Hili linalo nikabili mwana forum mwenzenu

Rahul Pacquao

Senior Member
Feb 9, 2013
148
180
Habari za saiz, poleni na majukumu.

Bila kupoteza wakati uzi wangu unahusiana na swala zima la madai ya mtoto mimi ni baba wa mtoto mmoja nilifunga ndoa yangu mwezi 5 mwaka huu lakini chaajabu mwanamke huyu anadai talaka tena amelivalia hasa njuga Swala hili bila kutaka kikako chochote wala suluhu Katika jambo hilo baba yake mzazi mtu amba nimwenye ku support swala hili kwakiasi kikubwa lakini kwa Kipindi chote hicho kwanzi mke wangu ajifungue mama yangu ndio alie beba jukumu lakumwangalia mtoto wangu pamoja na mke wangu kwakua familia yake ilijitenga kabisa na sisi kwahivyo hata salamu na kujakumtembelea mzazi hawaku taka kujua hayo.
Baada ya miezi mi 3 mke wangu alianza kwenda kazini na Mimi pia hua nakwenda kazini tuka kaachini nakujadili Swala la mfanya kazi bahati nzuri tuka pata mfanya kazi akawa anaishi na mama yangu pamoja na kumlea mtoto.

Mke wangu hua anaingia kazini saa 1asubuhi ananiachia mtoto Mimi nakaa na mtoto mpaka anapo amka Alafu namchukua nampeleka kwa mama yangu ndio anae kaa nae mpaka tunaporudi

Mke wangu anaondoka saa 1 asubuhi anarudi saa 1 usiku , Mimi naondoka saa 3asubuhi nakurudi saa 11 jioni nakuja kukaa na mtoto mpaka anapo rudi mke wangu pia yeye hua ana safiri mara kwa mara nakuniachia Mimi jukumu la kukaa na mtoto sasa talaka yake nimempatia lakini mtoto wangu anam ng'ang'ania ili kunikomoa yeye hatakumpa uji hawezi jumapili akitoka out na mtoto badala yakubeba uji anabeba biskuti na soda nahofia Sana mazingira ya mtoto endapo huyu mwanamke ataondoka nae.

Kinachonipa mawazo ni Swala la mtoto kukabidhiwa kwa baba baada ya miaka 7 huyu mtoto ataishi mazingira magumu kwakua hata marazingine mke wangu akiwa nyumbani mtoto akilia njaa usiku hua anampiga nakumwambia la-la achakunisumbua pale ninapo amka nakua mkali naonekana m baya nahofia Sana maisha ya mwanangu atakapo Kua anaishi na huyu mwanamke peke yake nampenda mke wangu Japo yeye hanitaki tena lakini hataaki ondoka mtoto wangu bado namuhitaji niakikishe Yuko salama na anapata malezi bora nisaidieni mawazo juu ya hili na swalazima lakisheria vipi nitakabidhiwa mwanangu kutokana na Swala hili?!
 
Pole ndugu yangu, ni kweli sheria inasema mtoto atakaa na mama kama ni chini ya miaka 7, ila hiyo ni general rule tu isikutishe kwani kila kanuni kuu ina mbadala wake ndani ya sheria.

Ila kabla sijawnda mbali sana napenda kufahamu hiyo talaka unayosema unempatia mkeo ni talaka ya aina gani? Ni talaka ya mswahili au ni talaka inayotambukika kisheria?. Kumbuka mahakama ndio inayoweza vunja ndoa labda kama hamkuoana na hiyo itakuwa si ndoa.

Nawasi wasi kuwa icho ulichompa mkeo si talaka bali mmetengana kwa muda tu!.

Kama ni talaka muende mahakamani na kwa muda wa ndoa yenu hamruhusiwi, narudia HAMRUHUSIWI kutalakiana kwani sheria inataka muwe mmeishi kwa zaidi ya miaka miwili ndani ya ndoa.

Hivyo mkuu futa wazo la umempa talaka mkeo.

Twende kwenye hoja ya awali, Malezi ya mtoto. Malezi ya mtoto siku zote mahakama inayaangalia au inayapanga ikitarajia kuwa yatakuwa yenye maslahi kwa mtoto, hivyo kama unaweza shawishi mahakama na ikaridhika kuwa ukikaa nae wewe malezi yatakuwa yenye maslahi zaidi ya akikaa na mama yake utaweza pewa jukumu hilo, ila bado kwa umri wake nadhani atakuwa ni mdogo sana anayeitaji uangalizi wa mama.

Pole sana mkuu ila nasisitiza HUJAMPA MKEO TALAKA, hamjakidhi vigezo bado vya kutalakiana.
 
Pole ndugu yangu, ni kweli sheria inasema mtoto atakaa na mama kama ni chini ya miaka 7, ila hiyo ni general rule tu isikutishe kwani kila kanuni kuu ina mbadala wake ndani ya sheria.

Ila kabla sijawnda mbali sana napenda kufahamu hiyo talaka unayosema unempatia mkeo ni talaka ya aina gani? Ni talaka ya mswahili au ni talaka inayotambukika kisheria?. Kumbuka mahakama ndio inayoweza vunja ndoa labda kama hamkuoana na hiyo itakuwa si ndoa.

Nawasi wasi kuwa icho ulichompa mkeo si talaka bali mmetengana kwa muda tu!.

Kama ni talaka muende mahakamani na kwa muda wa ndoa yenu hamruhusiwi, narudia HAMRUHUSIWI kutalakiana kwani sheria inataka muwe mmeishi kwa zaidi ya miaka miwili ndani ya ndoa.

Hivyo mkuu futa wazo la umempa talaka mkeo.

Twende kwenye hoja ya awali, Malezi ya mtoto. Malezi ya mtoto siku zote mahakama inayaangalia au inayapanga ikitarajia kuwa yatakuwa yenye maslahi kwa mtoto, hivyo kama unaweza shawishi mahakama na ikaridhika kuwa ukikaa nae wewe malezi yatakuwa yenye maslahi zaidi ya akikaa na mama yake utaweza pewa jukumu hilo, ila bado kwa umri wake nadhani atakuwa ni mdogo sana anayeitaji uangalizi wa mama.

Pole sana mkuu ila nasisitiza HUJAMPA MKEO TALAKA, hamjakidhi vigezo bado vya kutalakiana.
Asante Sana ndugu.

Kwanza samahani kwakua jambo moja sijalitole ufafanuzi vizuri kwakua ndoa tulio ifunga ni ya dini ya kiislam kwahivyo anaetaka ndoa ivunjike ni mke hivyo ikampasa kufuata taratibu za ku Vunja ndoa akaenda baraza LA Uislam BAKWATA akapewa barua ya mimi kuhitajika kufika office hizo Bwakwata walijaribu kutafuta suluhu lakini mwanamke hyo hakuhitaji hilo, kwenye baraza hilo waliamuru mtoto nibaki nae Mimi lakini mwanamke anataka tufike mahakamani kwakua Alisha Apia kuto ruhusu mtoto nibaki nae kirahisi ni kutokana na ushauri anaopata kutoka kwa Marafiki zake kwani wakati mwingine huzungumza na simu mbele yangu nakusisitiza kuondoka na mtoto..
 
Asante Sana ndugu.

Kwanza samahani kwakua jambo moja sijalitole ufafanuzi vizuri kwakua ndoa tulio ifunga ni ya dini ya kiislam kwahivyo anaetaka ndoa ivunjike ni mke hivyo ikampasa kufuata taratibu za ku Vunja ndoa akaenda baraza LA Uislam BAKWATA akapewa barua ya mimi kuhitajika kufika office hizo Bwakwata walijaribu kutafuta suluhu lakini mwanamke hyo hakuhitaji hilo, kwenye baraza hilo waliamuru mtoto nibaki nae Mimi lakini mwanamke anataka tufike mahakamani kwakua Alisha Apia kuto ruhusu mtoto nibaki nae kirahisi ni kutokana na ushauri anaopata kutoka kwa Marafiki zake kwani wakati mwingine huzungumza na simu mbele yangu nakusisitiza kuondoka na mtoto..

Sasa nimekuelewa vizuri zaidi mkuu, ila kuna mahali baraza limeyumba. Embu muache aende mahakamani na uhakika hawezi shinda kirahisi rahisi. Bado ndoa changa sana.

Japo baraza limeonesha kukubali ombi lake, ila mwisho wa yote ni mahakama na mahakama jaipendi kutoa talaka.

Au ngoja niulize sababu gani hasa anayoitumia kudai talaka?
 
Asante Sana ndugu.

Kwanza samahani kwakua jambo moja sijalitole ufafanuzi vizuri kwakua ndoa tulio ifunga ni ya dini ya kiislam kwahivyo anaetaka ndoa ivunjike ni mke hivyo ikampasa kufuata taratibu za ku Vunja ndoa akaenda baraza LA Uislam BAKWATA akapewa barua ya mimi kuhitajika kufika office hizo Bwakwata walijaribu kutafuta suluhu lakini mwanamke hyo hakuhitaji hilo, kwenye baraza hilo waliamuru mtoto nibaki nae Mimi lakini mwanamke anataka tufike mahakamani kwakua Alisha Apia kuto ruhusu mtoto nibaki nae kirahisi ni kutokana na ushauri anaopata kutoka kwa Marafiki zake kwani wakati mwingine huzungumza na simu mbele yangu nakusisitiza kuondoka na mtoto..
Hizo document za bakwata ni stage ya kwanza kabisa katika swala la talaka na sio mwisho mkuu, baada ya kutoka bakwata mnapaswa kwenda mahakamani na mahakama itoe maamuzi juu ya hio talaka/kugawana mali mlizochuma pamoja/malezi ya mtoto.

Haya ni mambo matatu mahakama lazima iyatolee hukumu, hukumu ya bakwata juu ya talaka na mtoto haina nguvu kabisa kisheria, mtu yoyote anaweza kuipamgua hayo maamuzi ya talaka ya bakwata.

Kuhusu talaka, mahakama itaangalia hukumu ya bakwata na itaangalia hoja zenu pande zote mbili juu ya maombi yenu ya talaka, na itaangalia kama ndoa yenu imevinjika na kufikia hatua haiwezi kutengenezeka tena (yani kupatanishwa). Hapo itatoa talaka.

Hatua ya pili, mahakama itaangalia mali mlizochuma mkiwa pamoja, kwenu nyinyi si jambo gumu sana kwani nyote mnafanya kazi, hivyo hakuta kua na mavutano zaidi ya mali/vitu mlivyopata kwa pamoja. Itagawanya mali baina yenu. (Mali ulizochuma kabla ya kumuoa hazita husishwa kwenye mgawanyo).

Hatua ya tatu, mahakama itaangalia nani kua mlezi wa mtoto, kile kipengele cha miaka 7 ni general rule tu kama mkuu alivyosema. Hapa anaweza akapewa mama yako kua mlezi wa mtoto mpaka afikie umri fulani, na unaweza usipewe wewe kumlea wala mke wako (inategemea na maombi yatakavyo fanywa mahakamani, mama yako anaweza akafanya maombi amlee yeye na akapewa kama tu atathibitisha mbele ya mahakama kua mtoto akilelewa na wewe au mke wako hatapata malezi bora/huduma bora - hii inaweza ikashika nguvu kutokana wewe unakua kazini kuanzia asubuhi mpaka jioni pia mkeo hivyo hivyo nae, la pili mama yako kamwangalia/anamwangalia muda wote mkiwa hampo = mtoto amekua vizuri bila shida yoyote).

Akipewa mama yako mamlaka ya kumlea, basi wewe na mkeo mtaamrishwa muwe mnampatia kiasi kadhaa cha fedha kila mwisho wa mwezi kwaajili ya kumwangalia mtoto. Mfano wewe uwe unatoa laki1 na mkeo anatoa laki1.




Asikutishe na hivo vi simu vyake kwa mashoga zake huyo, akienda mahakamani ndo atajua madhara ya ujinga anaofanya. We ukienda mahakamani hakikisha unaweka ombi la mtoto kulelewa na mama yako (halafu yeye mpake matope ya uso kisawasawa kuanzia anatoka saa 1 asubuhi na kurudi saa moja usiku, kumpiga mtoto akilia njaa, tatu mama yako ndio muaangalizi mkuu wa mtoto mpaka sasa)
 
Hizo document za bakwata ni stage ya kwanza kabisa katika swala la talaka na sio mwisho mkuu, baada ya kutoka bakwata mnapaswa kwenda mahakamani na mahakama itoe maamuzi juu ya hio talaka/kugawana mali mlizochuma pamoja/malezi ya mtoto.

Haya ni mambo matatu mahakama lazima iyatolee hukumu, hukumu ya bakwata juu ya talaka na mtoto haina nguvu kabisa kisheria, mtu yoyote anaweza kuipamgua hayo maamuzi ya talaka ya bakwata.

Kuhusu talaka, mahakama itaangalia hukumu ya bakwata na itaangalia hoja zenu pande zote mbili juu ya maombi yenu ya talaka, na itaangalia kama ndoa yenu imevinjika na kufikia hatua haiwezi kutengenezeka tena (yani kupatanishwa). Hapo itatoa talaka.

Hatua ya pili, mahakama itaangalia mali mlizochuma mkiwa pamoja, kwenu nyinyi si jambo gumu sana kwani nyote mnafanya kazi, hivyo hakuta kua na mavutano zaidi ya mali/vitu mlivyopata kwa pamoja. Itagawanya mali baina yenu. (Mali ulizochuma kabla ya kumuoa hazita husishwa kwenye mgawanyo).

Hatua ya tatu, mahakama itaangalia nani kua mlezi wa mtoto, kile kipengele cha miaka 7 ni general rule tu kama mkuu alivyosema. Hapa anaweza akapewa mama yako kua mlezi wa mtoto mpaka afikie umri fulani, na unaweza usipewe wewe kumlea wala mke wako (inategemea na maombi yatakavyo fanywa mahakamani, mama yako anaweza akafanya maombi amlee yeye na akapewa kama tu atathibitisha mbele ya mahakama kua mtoto akilelewa na wewe au mke wako hatapata malezi bora/huduma bora - hii inaweza ikashika nguvu kutokana wewe unakua kazini kuanzia asubuhi mpaka jioni pia mkeo hivyo hivyo nae, la pili mama yako kamwangalia/anamwangalia muda wote mkiwa hampo = mtoto amekua vizuri bila shida yoyote).

Akipewa mama yako mamlaka ya kumlea, basi wewe na mkeo mtaamrishwa muwe mnampatia kiasi kadhaa cha fedha kila mwisho wa mwezi kwaajili ya kumwangalia mtoto. Mfano wewe uwe unatoa laki1 na mkeo anatoa laki1.




Asikutishe na hivo vi simu vyake kwa mashoga zake huyo, akienda mahakamani ndo atajua madhara ya ujinga anaofanya. We ukienda mahakamani hakikisha unaweka ombi la mtoto kulelewa na mama yako (halafu yeye mpake matope ya uso kisawasawa kuanzia anatoka saa 1 asubuhi na kurudi saa moja usiku, kumpiga mtoto akilia njaa, tatu mama yako ndio muaangalizi mkuu wa mtoto mpaka sasa)
Nimekuelewa sana mkuu na pia asante sana kwa ushauri wako, naweza kusema umenifungua macho pia umenitoa wasi wasi kwa kiasi Fulani mawazo yenu yamekua ni yakunifariji nakunipa matumaini kwa kiasi kikubwa mnoo kwani kabla yaku leta jambo hili mezani hapa kiukweli nilikua mnyonge lakini sasa nuru nimeanza kuiona kiukweli kwaniliyo yaelezea yamenisumbua sana ila uwepo wenu ni wafaida sana kwajamii itakayo hitaji msaada kwanzia wa mawazo kutoka kwenu nafikiri sidhani kama Ntakua nakosea kama baada ya kuzungumza yote na kutoa ushahidi mbele ya mahaka juu ya malezi ya mtoto nakuiomba mahaka kumkabidhi mama yangu mtoto na kutoa kiasi cha pesa kita kacho mtunza mtoto kwa kua yeye ndio alio beba jukumu hilo kwanzia miezi mi 3 baada ya mtoto kuzaliwa mpaka sasa miaka mi 2 kwakua sisi niwatu wa kuondoka asubuhi na kurudi jioni isitishe mwenzangu ni mtu wa kusafiri Mara kwa mara.

Pia mwanamke huyu alisha leta ugovi na kubeba baadhi ya vitu tulivo chuma pamoja na kuondoka navyo akapeleka kwao lakini baada ya muda alijirudi na kuniomba msamaha nilimsamehe kwakua nampenda Ila vitu alivo peleka kwao mwanzo ni sofa set na kabati LA vyombo pamoja na kapeti la manyoya (ZULIA) alipo niomba msamaa nika msamehe nilimwambia kama unarudi kwangu usirudi na chochote kati ya ulivo vichukua siku anarudi alitoroka kwao akaja na bag la nguo tuuu vingine vyotee tukaanza upya jeee hapo kwenye kugawana Mali atakua na haki ya kuchukua chochote?!
 
Sasa nimekuelewa vizuri zaidi mkuu, ila kuna mahali baraza limeyumba. Embu muache aende mahakamani na uhakika hawezi shinda kirahisi rahisi. Bado ndoa changa sana.

Japo baraza limeonesha kukubali ombi lake, ila mwisho wa yote ni mahakama na mahakama jaipendi kutoa talaka.

Au ngoja niulize sababu gani hasa anayoitumia kudai talaka?
Sababu alizo tumia kiukweli hata kwa Mimi mume wake nashangaa sana ndio maana nikasema ushauri wa mashoga na support ya kuvunja ndoa kutoka kwa baba yake kwakua mshahara wa mke wangu wote humpatia baba yake na kuniambia nimemsaidia baba yangu alikua ana shida Ila Mimi naona fine jukumu la kuilea familia ni langu kwani Mimi ndio kichwa cha familia.

Kisa kilianza mke wangu Ali nunu brender ya juice tulivo kua kazini kama kawaida huku nyumban mfanya kazi aliona hiyo brender na akaanza kuitumia bila ridhaa ya mama pia akatumia na kinywaji cha mke wangu kilichokua kwenye fredg bila ridhaa yake mke wangu aliporudi alichukia sanaa nakugomba licha ya hivyo pia akaninunia na Mimi nakuninyima haki yangu ya nyumba mwezi mzima lakini nika mkanya mfanya kazi mbele yake akiwepo kua asifanye wala asiguse chochote bila ridhaa ya mke wangu lakini pia hakuridhika nilipo ongea na mfanya kazi kwa ukarimu alitaka nimgombeze nimkemee lakini bila kufikiria kesho mfanya kazi huyo ndo atakua na mtoto pia inaweza kua hatari kama hatuto ishi na mfanya kazi kama ndugu kwakua yeye ndio anae kaa na mtoto pia akisaidiana na bibi wa mtoto.

Mpaka sasa nikimuuliza sababu kuu hasa ananiambia siwezi kuishi kwenye nyumba hii kwasababu yeye vitu vyake vinatumika bila yeye kupenda anataka kuishi peke yake ajitawale mwenyewe hivyo hata uamuzi niliochukua wakumkanya mfanya kazi anaona si kitu yeye anachotaka nikuishi peke yake tu kiukweli inaniumiza sana roho maana sababu ya yeye kuvunja ndo ni brender na ni nzima mpaka sasa sio kama ilitumika ikaaribika pia ilitumika Ku brend chakula cha mwanae dah inanitesa kichwa sanaaaa....
 
Nimekuelewa sana mkuu na pia asante sana kwa ushauri wako, naweza kusema umenifungua macho pia umenitoa wasi wasi kwa kiasi Fulani mawazo yenu yamekua ni yakunifariji nakunipa matumaini kwa kiasi kikubwa mnoo kwani kabla yaku leta jambo hili mezani hapa kiukweli nilikua mnyonge lakini sasa nuru nimeanza kuiona kiukweli kwaniliyo yaelezea yamenisumbua sana ila uwepo wenu ni wafaida sana kwajamii itakayo hitaji msaada kwanzia wa mawazo kutoka kwenu nafikiri sidhani kama Ntakua nakosea kama baada ya kuzungumza yote na kutoa ushahidi mbele ya mahaka juu ya malezi ya mtoto nakuiomba mahaka kumkabidhi mama yangu mtoto na kutoa kiasi cha pesa kita kacho mtunza mtoto kwa kua yeye ndio alio beba jukumu hilo kwanzia miezi mi 3 baada ya mtoto kuzaliwa mpaka sasa miaka mi 2 kwakua sisi niwatu wa kuondoka asubuhi na kurudi jioni isitishe mwenzangu ni mtu wa kusafiri Mara kwa mara.

Pia mwanamke huyu alisha leta ugovi na kubeba baadhi ya vitu tulivo chuma pamoja na kuondoka navyo akapeleka kwao lakini baada ya muda alijirudi na kuniomba msamaha nilimsamehe kwakua nampenda Ila vitu alivo peleka kwao mwanzo ni sofa set na kabati LA vyombo pamoja na kapeti la manyoya (ZULIA) alipo niomba msamaa nika msamehe nilimwambia kama unarudi kwangu usirudi na chochote kati ya ulivo vichukua siku anarudi alitoroka kwao akaja na bag la nguo tuuu vingine vyotee tukaanza upya jeee hapo kwenye kugawana Mali atakua na haki ya kuchukua chochote?!
Kwenye kuchukua mali mahakama ita thaminisha mali mlizo chuma pamoja, na watakata thamani ya vitu alivyochukua. Kama atakua amechukua thamani kubwa kuliko iliobakia mliochuma pamoja, basi ataamriwa na mahakama akulipe wewe ziada ya pesa ya thamani iliozidi. Kama atakua ameshachukua thamani anayotakiwa kupewa stahiki na mahakama, basi hapati kitu.

Wala usihofu yeye kwenda mahakamani, ukiwa mkweli wa mambo mahakamani utafurahi na hukumu, na yeye akijifanya kudanganya atajutia (pengine anaweza akaomba msameheane na jeuri yake akaiweka pembeni).

Pia wewe unaweza ukaamua kwenda mahakamani kabla yake kuomba hayo maswala matatu tulioainisha hapo juu (talaka, mgawanyo wa mali mliochuma pamoja, na maombi ya malezi ya mtoto kwa mama yako). Ni haki yako kisheria, sio lazima umsubiri yeye atangulie mahakamani au akae kukutishia kila siku uwe huna amani wala furaha. (Maamuzi yako hapo sasa, kama utaamua uende mahakamani ili umalizane na hili swala na uangalie maisha yako ya mbele na mtoto, au umsubiri yeye aende mahakamani akiamua).

Ila maombi ya malezi fanya uombe apewe mama yako mzazi amlee mtoto, maana mama yako ana nguvu ya kumlea mtoto kisheria kuliko wewe wala mke wako. (Mama yako anaweza akapeleka maombi usipewe wewe wala mke wako mtoto kumlea (Japo nyinyi ni wazazi halali wa mtoto, ila mahakama wanaangalia mtu atakae mpa MALEZI BORA MTOTO) na mahakama ikakubali na akashinda kesi bila wasiwasi, nyinyi mkapewa amri ya kuchangia gharama za mtoto; kwa kigezo yeye ndio kamlea toka mchanga mpaka sasa ana miaka 2, kigezo kingine nyinyi mpo bussy sana na kazi na hamna muda wa kukaa na mtoto, kigezo cha tatu kwa uangalizi wake mtoto atapata malezi bora kuliko kwako/kwa mkeo, kigezo cha nne ni ndugu wa karibu kwa mtoto **bibi** na si mtu baki.)
 
Kwenye kuchukua mali mahakama ita thaminisha mali mlizo chuma pamoja, na watakata thamani ya vitu alivyochukua. Kama atakua amechukua thamani kubwa kuliko iliobakia mliochuma pamoja, basi ataamriwa na mahakama akulipe wewe ziada ya pesa ya thamani iliozidi. Kama atakua ameshachukua thamani anayotakiwa kupewa stahiki na mahakama, basi hapati kitu.

Wala usihofu yeye kwenda mahakamani, ukiwa mkweli wa mambo mahakamani utafurahi na hukumu, na yeye akijifanya kudanganya atajutia (pengine anaweza akaomba msameheane na jeuri yake akaiweka pembeni).

Pia wewe unaweza ukaamua kwenda mahakamani kabla yake kuomba hayo maswala matatu tulioainisha hapo juu (talaka, mgawanyo wa mali mliochuma pamoja, na maombi ya malezi ya mtoto kwa mama yako). Ni haki yako kisheria, sio lazima umsubiri yeye atangulie mahakamani au akae kukutishia kila siku uwe huna amani wala furaha. (Maamuzi yako hapo sasa, kama utaamua uende mahakamani ili umalizane na hili swala na uangalie maisha yako ya mbele na mtoto, au umsubiri yeye aende mahakamani akiamua).

Ila maombi ya malezi fanya uombe apewe mama yako mzazi amlee mtoto, maana mama yako ana nguvu ya kumlea mtoto kisheria kuliko wewe wala mke wako. (Mama yako anaweza akapeleka maombi usipewe wewe wala mke wako mtoto kumlea (Japo nyinyi ni wazazi halali wa mtoto, ila mahakama wanaangalia mtu atakae mpa MALEZI BORA MTOTO) na mahakama ikakubali na akashinda kesi bila wasiwasi, nyinyi mkapewa amri ya kuchangia gharama za mtoto; kwa kigezo yeye ndio kamlea toka mchanga mpaka sasa ana miaka 2, kigezo kingine nyinyi mpo bussy sana na kazi na hamna muda wa kukaa na mtoto, kigezo cha tatu kwa uangalizi wake mtoto atapata malezi bora kuliko kwako/kwa mkeo, kigezo cha nne ni ndugu wa karibu kwa mtoto **bibi** na si mtu baki.)
Shukran Sana mkuu nazidi kukuelewa zaidi mungu akubariki Sana abariki na kazi za mikono yako asante sanaa..!!!
 
Sababu alizo tumia kiukweli hata kwa Mimi mume wake nashangaa sana ndio maana nikasema ushauri wa mashoga na support ya kuvunja ndoa kutoka kwa baba yake kwakua mshahara wa mke wangu wote humpatia baba yake na kuniambia nimemsaidia baba yangu alikua ana shida Ila Mimi naona fine jukumu la kuilea familia ni langu kwani Mimi ndio kichwa cha familia.

Kisa kilianza mke wangu Ali nunu brender ya juice tulivo kua kazini kama kawaida huku nyumban mfanya kazi aliona hiyo brender na akaanza kuitumia bila ridhaa ya mama pia akatumia na kinywaji cha mke wangu kilichokua kwenye fredg bila ridhaa yake mke wangu aliporudi alichukia sanaa nakugomba licha ya hivyo pia akaninunia na Mimi nakuninyima haki yangu ya nyumba mwezi mzima lakini nika mkanya mfanya kazi mbele yake akiwepo kua asifanye wala asiguse chochote bila ridhaa ya mke wangu lakini pia hakuridhika nilipo ongea na mfanya kazi kwa ukarimu alitaka nimgombeze nimkemee lakini bila kufikiria kesho mfanya kazi huyo ndo atakua na mtoto pia inaweza kua hatari kama hatuto ishi na mfanya kazi kama ndugu kwakua yeye ndio anae kaa na mtoto pia akisaidiana na bibi wa mtoto.

Mpaka sasa nikimuuliza sababu kuu hasa ananiambia siwezi kuishi kwenye nyumba hii kwasababu yeye vitu vyake vinatumika bila yeye kupenda anataka kuishi peke yake ajitawale mwenyewe hivyo hata uamuzi niliochukua wakumkanya mfanya kazi anaona si kitu yeye anachotaka nikuishi peke yake tu kiukweli inaniumiza sana roho maana sababu ya yeye kuvunja ndo ni brender na ni nzima mpaka sasa sio kama ilitumika ikaaribika pia ilitumika Ku brend chakula cha mwanae dah inanitesa kichwa sanaaaa....

Pole sana mkuu, nilichokigundua hapa ni huwenda mkeo 'amekuchoka/amechoka ndoa' ila uzuri sheria ya ndoa haivunji ndoa kwa sababu ndogo tu eti mmechokana.

Tatizo litakuwa kijamii tu kwani kuendelea kuishi na mtu aliyekuchoka/kuchoka mfumo wa maisha ya ndia huwa ni shughuli sana.
 
Wanawake bhna hapo mimi sijaona sababu ya msingi ya kuvunja ndoa kwa kweli huyo anaweza akawa amepata mtu mwingine hakuna jambo baya kama kulazimisha upendo ulio isha achana nae huyo kwani?? Bado anakunyima tendo la ndoa
 
Wanawake bhna hapo mimi sijaona sababu ya msingi ya kuvunja ndoa kwa kweli huyo anaweza akawa amepata mtu mwingine hakuna jambo baya kama kulazimisha upendo ulio isha achana nae huyo kwani?? Bado anakunyima tendo la ndoa
Unaweza ukakuta kuna mtu kampata anamzuzua kichwa tu na ndo maana kaamua kufanya hayo, na kusahau kua kuna maisha tena huko mbele. Mwanamke akikamata pesa/kazi nzuri huwa mara nyingi inakua hivyo, japo sio wote, ila kibarua kikiota nyasi huwa wanachanganyikiwa na kujirudi kuanza kuomba msamaha.

Ndo maana nimemwambia mkuu asijitie mawazo wala presha, japo kweli ni jambo gumu, linauma sana, hasa ukiangalia ndio mtu uliemchagua uishi nae maisha yako yote na ndio mama wa mtoto wako ila kaamua kukugeuka.

Huyo mwanamke naamini atarudi kwa jamaa kumpigia magoti na kumwomba msamaha tu, apewe muda ayaone maisha yanavyokua.

Pia jamaa ndio anauwezo wa kumnyoosha huyo mwanamke kisheria kuliko maelezo, kama ataamua kumnyoosha kweli. (Ila si mshauri amnyooshe, amwache tu arukeruke na afanye analotaka, yeye apambane kupata ruhusa ya mahakama ya kumlea mtoto tu, halafu amwachie mungu amlipie maumivu aliompa)
 
Pole ndugu yangu, ni kweli sheria inasema mtoto atakaa na mama kama ni chini ya miaka 7, ila hiyo ni general rule tu isikutishe kwani kila kanuni kuu ina mbadala wake ndani ya sheria.

Ila kabla sijawnda mbali sana napenda kufahamu hiyo talaka unayosema unempatia mkeo ni talaka ya aina gani? Ni talaka ya mswahili au ni talaka inayotambukika kisheria?. Kumbuka mahakama ndio inayoweza vunja ndoa labda kama hamkuoana na hiyo itakuwa si ndoa.

Nawasi wasi kuwa icho ulichompa mkeo si talaka bali mmetengana kwa muda tu!.

Kama ni talaka muende mahakamani na kwa muda wa ndoa yenu hamruhusiwi, narudia HAMRUHUSIWI kutalakiana kwani sheria inataka muwe mmeishi kwa zaidi ya miaka miwili ndani ya ndoa.

Hivyo mkuu futa wazo la umempa talaka mkeo.

Twende kwenye hoja ya awali, Malezi ya mtoto. Malezi ya mtoto siku zote mahakama inayaangalia au inayapanga ikitarajia kuwa yatakuwa yenye maslahi kwa mtoto, hivyo kama unaweza shawishi mahakama na ikaridhika kuwa ukikaa nae wewe malezi yatakuwa yenye maslahi zaidi ya akikaa na mama yake utaweza pewa jukumu hilo, ila bado kwa umri wake nadhani atakuwa ni mdogo sana anayeitaji uangalizi wa mama.

Pole sana mkuu ila nasisitiza HUJAMPA MKEO TALAKA, hamjakidhi vigezo bado vya kutalakiana.
well said
 
Unaweza ukakuta kuna mtu kampata anamzuzua kichwa tu na ndo maana kaamua kufanya hayo, na kusahau kua kuna maisha tena huko mbele. Mwanamke akikamata pesa/kazi nzuri huwa mara nyingi inakua hivyo, japo sio wote, ila kibarua kikiota nyasi huwa wanachanganyikiwa na kujirudi kuanza kuomba msamaha.

Ndo maana nimemwambia mkuu asijitie mawazo wala presha, japo kweli ni jambo gumu, linauma sana, hasa ukiangalia ndio mtu uliemchagua uishi nae maisha yako yote na ndio mama wa mtoto wako ila kaamua kukugeuka.

Huyo mwanamke naamini atarudi kwa jamaa kumpigia magoti na kumwomba msamaha tu, apewe muda ayaone maisha yanavyokua.

Pia jamaa ndio anauwezo wa kumnyoosha huyo mwanamke kisheria kuliko maelezo, kama ataamua kumnyoosha kweli. (Ila si mshauri amnyooshe, amwache tu arukeruke na afanye analotaka, yeye apambane kupata ruhusa ya mahakama ya kumlea mtoto tu, halafu amwachie mungu amlipie maumivu aliompa)
Ukweli mtupu kabisa na nimeona umemshauri vizuri sana toka uko juu wewe ni miongoni mwa Member Wazuri vichwani 👏👏👏👏👏
 
Hizo document za bakwata ni stage ya kwanza kabisa katika swala la talaka na sio mwisho mkuu, baada ya kutoka bakwata mnapaswa kwenda mahakamani na mahakama itoe maamuzi juu ya hio talaka/kugawana mali mlizochuma pamoja/malezi ya mtoto.

Haya ni mambo matatu mahakama lazima iyatolee hukumu, hukumu ya bakwata juu ya talaka na mtoto haina nguvu kabisa kisheria, mtu yoyote anaweza kuipamgua hayo maamuzi ya talaka ya bakwata.

Kuhusu talaka, mahakama itaangalia hukumu ya bakwata na itaangalia hoja zenu pande zote mbili juu ya maombi yenu ya talaka, na itaangalia kama ndoa yenu imevinjika na kufikia hatua haiwezi kutengenezeka tena (yani kupatanishwa). Hapo itatoa talaka.

Hatua ya pili, mahakama itaangalia mali mlizochuma mkiwa pamoja, kwenu nyinyi si jambo gumu sana kwani nyote mnafanya kazi, hivyo hakuta kua na mavutano zaidi ya mali/vitu mlivyopata kwa pamoja. Itagawanya mali baina yenu. (Mali ulizochuma kabla ya kumuoa hazita husishwa kwenye mgawanyo).

Hatua ya tatu, mahakama itaangalia nani kua mlezi wa mtoto, kile kipengele cha miaka 7 ni general rule tu kama mkuu alivyosema. Hapa anaweza akapewa mama yako kua mlezi wa mtoto mpaka afikie umri fulani, na unaweza usipewe wewe kumlea wala mke wako (inategemea na maombi yatakavyo fanywa mahakamani, mama yako anaweza akafanya maombi amlee yeye na akapewa kama tu atathibitisha mbele ya mahakama kua mtoto akilelewa na wewe au mke wako hatapata malezi bora/huduma bora - hii inaweza ikashika nguvu kutokana wewe unakua kazini kuanzia asubuhi mpaka jioni pia mkeo hivyo hivyo nae, la pili mama yako kamwangalia/anamwangalia muda wote mkiwa hampo = mtoto amekua vizuri bila shida yoyote).

Akipewa mama yako mamlaka ya kumlea, basi wewe na mkeo mtaamrishwa muwe mnampatia kiasi kadhaa cha fedha kila mwisho wa mwezi kwaajili ya kumwangalia mtoto. Mfano wewe uwe unatoa laki1 na mkeo anatoa laki1.




Asikutishe na hivo vi simu vyake kwa mashoga zake huyo, akienda mahakamani ndo atajua madhara ya ujinga anaofanya. We ukienda mahakamani hakikisha unaweka ombi la mtoto kulelewa na mama yako (halafu yeye mpake matope ya uso kisawasawa kuanzia anatoka saa 1 asubuhi na kurudi saa moja usiku, kumpiga mtoto akilia njaa, tatu mama yako ndio muaangalizi mkuu wa mtoto mpaka sasa)
you killed it
 
Wanawake bhna hapo mimi sijaona sababu ya msingi ya kuvunja ndoa kwa kweli huyo anaweza akawa amepata mtu mwingine hakuna jambo baya kama kulazimisha upendo ulio isha achana nae huyo kwani?? Bado anakunyima tendo la ndoa
Hutoa anapojisikia yeye ndio anaanza kuomba msamaha kwa ujinga anao fanya pale anapo ni nyima na Mimi nikikaa kimya muda mrefu bila kumuomba tunaishi Kama marafiki uzalendo ukimshinda ndio anakuja na machozi yaani nashindwa kujua shida yake hasa ni nini wakati mwingine naweza Sema marafiki zake pia humshauri ujinga kwanza marafiki zake wote wameachwa na mabwana zao naniwatu wazma wenyekumzidi umri Sanaa tu hao ndio hua wanawasiliana mara kwa mara nakutembeleana majumbani Jana nilikuta SMS ya rafiki akimshimikiza kuondoka chumba amesha mpatia.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom