Naombeni ushauri niende kubaki Marekani au nirudi nyumbani

Kwa kifupi unaweza kuwa na viza lakini ukishia airport na kupanda ndege hiyo hiyo iliyokubeba kurudi nayo iwapo utatiliwa shaka,kwani kuna viswali huulizwa kabla hujagongewa muhuriwa kuruhusiwa kuingia,pia jua digrii yako ya Bongo hakuna anayeijua huko Marekani na mwisho hadi kuja kufanikiwa Marekani inachukua miaka, na Marekani si lelemama kama wengi tunavyodhani huku au tunavyoangalia kwenye FB ,na kwa hali ya mtawala wa sasa aliyepo kwenye jengo jeupe,sidhani kama ni jambo jema kupiga kambi Marekani na kwa sasa sijui hata nafasi za kusomea unesi kama zipo kama ilivyokuwa awali,kwa wengi ukiwa nesi angalau ndio unakuwa na maisha ya uhakika au uwe na skills za kufa mtu ndio mfumo ukuhitaji, na mwisho kaka bila makaratasi utaishia kuuza maji mitaani kwa pesa ndogo. Ni bora uende ukaangalie na urudi tu ,hapa Bongo ni peponi kulinganisha na huko unakotaka kuzamia,maisha si rahisi kama wengi tunavyodhani,Marekani hakuna cha mjomba wala kwenda kuchimba mhogo shambani,usipofanya kazi/kibarua jua hutakuwa na sehemu ya kulala wala kula,yes kila kitu kipo lakini kila kitu ni pesa.Nenda kajionee mwenyewe halafu uje utuambie hapa,lakini jua moja tu huko utaenda kupigika kweli kweli, na utaikumbuka Bongo.Nimeandika kwa uzoefu nilionao wa kuishi Marekani japo si kwa muda mrefu,ikabidi ni Uturn asap.
U nailed it..asipoelewa hapa basi tena
 
Ni kweli bro unayoyasema au ni unataka kunikatisha tamaa?
Hii ndo mara ya kwanza hata kupanda ndege umesema nadhani pata uzoefu kwanza...then tupate mrejesho
Marekani ione kwenye TV tu si kwepesi...
 
Umepewa Visa ya nini ? Au unamaanisha unataka uzamie baada ya kuhudhuria huo mkutano ?

Kama ndivyo usifanye hivyo ,nenda kwenye mkutano halafu rudi nyumbani ,fuata proper channels upate Visa kama ni student ili uishi angalua vizuri kidogo

Vinginevyo utalimia meno.
 
Wamarekani wenyewe wanazamia Canada na Nordic countries

Kwanza unaenda kufikia wapi baada ya kuzamia? Una pesa kiasi gani na umepanga kwenda kufanya nini?

Kama ni kazi za hovyo kweli zipo nyingi tu ila utazifanya kazi tofauti sio chini ya 3 mpaka 5 kwa saa 24 ili uweze kumudu maisha ya hovyo tu, kama huna ramani yoyote ya maana ikiwemo valid permit unaenda kuwa homeless faggot with no apology na kiukweli umenichekesha sana ulivyosema nikifika nitaileta familia yangu (5 people) wewe mwenyewe ukijimudu binafsi shukuru Mungu.
 
Wamarekani wenyewe wanazamia Canada na Nordic countries

Kwanza unaenda kufikia wapi baada ya kuzamia? Una pesa kiasi gani na umepanga kwenda kufanya nini?

Kama ni kazi za hovyo kweli zipo nyingi tu ila utazifanya kazi tofauti sio chini ya 3 mpaka 5 kwa saa 24 ili uweze kumudu maisha ya hovyo tu, kama huna ramani yoyote ya maana ikiwemo valid permit unaenda kuwa homeless faggot with no apology na kiukweli umenichekesha sana ulivyosema nikifika nitaileta familia yangu (5 people) wewe mwenyewe ukijimudu binafsi shukuru Mungu.
Hawa Wabongo wanadanganyika sana na maneno ya kwenye vijiwe au kwa kuangalia FB na runinga,homeless wa US huwezi fananisha na wa hapa,kwanza sidhani kama tuna homeless hapa Tanzania,US ione hivyo hivyo kama huna mpango Bongo ni paradiso,halafu watu wanachekesha kwanza anaenda kuzamia ,je unazamia kwenda kuishi kwa nani?hakuna anayetaka kubeba mzigo wa mwingine US,US ni kuchapa kazi,Bongo wengi tumezoea ukienda kwa mjomba ni kulala na kula tu,hiyo US sahau,usipofanya kazi ,huli na utakosa sehemu ya kulala,hakuna nyumba ya urithi wala ya baba mdogo, bila makaratasi utaishia kuwa mzururaji tu,na kupata makaratasi sio shughuli nyepesi hasa siku hizi.halafu US wakati wa kiangazi joto ,joto kweli na wakati wa baridi ,ni baridi kweli sasa mwenzangu ukikosa sehemu ya kujisitri na huku vibarua vyenyewe ni shida hapo ndio utakumbuka Bongo,na kurudi bongo angalau basi uwe na pesa kwani nauli nayo pasua kichwa.
 
Sijawah kuwaza kuishi nje ya nchi.
Plus nikiwa zoom wanangu na wazee basi ndio kabisaa nje nazid kusahau kabisaa nazid kupambana hapa hapa.
Ila ww kama una mudu mzee nenda tuu.
 
Hivi huwaoni wa mexico waliozamia wanavyokua deported kwao kila siku na sasa hivi wapo kwenye enforcement ya kuwarudisha wazamiaji wote.
Na kingine fwatilia news za marekani sana utagundua siku hizi Kuna mass shooting and massacre zinazowalenga hasa wasio wamarekani.... Sasa we jichanganye kidogo uone mziki wake.... Utavuka bahari na mata**ko
 
Hawa Wabongo wanadanganyika sana na maneno ya kwenye vijiwe au kwa kuangalia FB na runinga,homeless wa US huwezi fananisha na wa hapa,kwanza sidhani kama tuna homeless hapa Tanzania,US ione hivyo hivyo kama huna mpango Bongo ni paradiso,halafu watu wanachekesha kwanza anaenda kuzamia ,je unazamia kwenda kuishi kwa nani?hakuna anayetaka kubeba mzigo wa mwingine US,US ni kuchapa kazi,Bongo wengi tumezoea ukienda kwa mjomba ni kulala na kula tu,hiyo US sahau,usipofanya kazi ,huli na utakosa sehemu ya kulala,hakuna nyumba ya urithi wala ya baba mdogo, bila makaratasi utaishia kuwa mzururaji tu,na kupata makaratasi sio shughuli nyepesi hasa siku hizi.halafu US wakati wa kiangazi joto ,joto kweli na wakati wa baridi ,ni baridi kweli sasa mwenzangu ukikosa sehemu ya kujisitri na huku vibarua vyenyewe ni shida hapo ndio utakumbuka Bongo,na kurudi bongo angalau basi uwe na pesa kwani nauli nayo pasua kichwa.
Nina uhakika 150% akifika US na kuwahadithia Wamarekani kwamba alikua akilelea ndugu zake 7 na kuwasomesha wengine na anayo familia ya watu 5 watamuona ana Steel balls na hiyo ndio point niliyomuona hayupo serious

Sababu kama ameweza kufanya hayo yote bongo then bado ana uchu wa kwenda kuzamia marekani maana yake ni kwamba anahamu ya kupata zaidi na kukamilisha Makubwa zaidi ya hayo aliyoyafanya kitu ambacho hatokaa akifanikishe hata robo ya alichofanya so far kwa hii approach yake akiwa marekani.
 
Sijawahi ishi Marekani, But one thing nipo sure kipato anachoweza pata mchakarikaji Marekani hakifanani hata kidogo na cha Bongo.
Kaka nadhani umekuwa mkweli kwa kusema hujawahi ishi Marekani, sababu ungesema umeishi Marekani usingewaza hivyo,kwa kifupi kipato na matumizi Marekani ni vitu visivyoendana ,nina maana unafanya kazi na hela yako inaishia yote kwenye malipo na ili kesho uamuke uende kwenye kibarua,nadhani nikisema kibarua unaelewa maana ya malipo ya kibarua,kingine Marekani kama hueleweki kwa maana bima huna matibabu yake yako juu sana,wengine huagiza dawa kutoka Bongo kupeleka US sababu kama huna bima dawa ambayo Bongo unanunua kwa TZS 20,000 Us utanunua kwa USD 200. Nikuulize ni watu wangapi wanaishi Marekani wamejenga nyumba zao Bongo kwa vyovyote ni wachache sana kulinganisha na wabongo waliopo Bongo,Bongo utaenda kwa Mpemba kukopa unga US hakuna hicho kitu,utaomba kwa Mpemba akupunguzie bei US hakuna hicho kitu,ukienda madukani kila kitu kimewekwa bei na tofauti na Bongo bei iliyowekwa ndio unalipa lakini US kitu kimeandikwa USD 20 unaenda lipa kaunta usd 21 au 22 kutokana na hesabu ya kodi,Lakini kama nilivyoandika mwanzo wacha mdau aende na akazamie kama anavyotaka halafu aje atupe mrejesho,US kuna taka mipango kabambe kuishi na si kama yule mtu anatoka Shirati anaenda Dar kwa shemeji kutafuta kibarua.
 
Nimekaa marekani na kufanya kazi marekani miaka nane sikuwa kuona cha maana zaidi ya kukadiriwa mikodi mikubw mikubwa weweee..nipo zangu bongo nauza magari hapa kariakoo life linasonga
 
Yani wewe umefika mpaka chuo kikuu lakini unafikiria kuzamia? Kweli elimu yetu haina thamani.

Akili zako wewe na za mtu wa mkoani anayefikiri akija Dar anakuwa katoka kimaisha hazina tofauti. Kweli umesoma? Au shule ndio imekusoma wewe?
 
Nimekaa marekani na kufanya kazi marekani miaka nane sikuwa kuona cha maana zaidi ya kukadiriwa mikodi mikubw mikubwa weweee..nipo zangu bongo nauza magari hapa kariakoo life linasonga
Hebu waambie hawa kaka,maana hawaelewi lakini sio makosa yao sababu hawajawai fika au ishi Marekani. Saving Marekani ni kazi sana.
 
Hongera sana ndugu. sana sana. kweli unayaweza majukumu. hujazungumzia kutafuta kazi nyingine yenye kipato kikubwa, pili unabaki hapa ya nini kaka?! mke unaye. watoto pia. mama umemwezesha, ndugu ndio usiseme. sasa cha kukuweka hapa ni nini????!!! nenda US of A upate zaidi uweke boma lako kamtaji kagari pale huku waendelea kuwasaidia ndugu mama na familia yako mpaka mwili utakapochoka au kutimiza malengo. ebu panda ndinga haraka sana kaka..
Mkuu wewe ni mmoja kati ya watu wenye Uelewa wa hali ya juu mno

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom