Naombeni ushauri namna ya kuepukana na hili tatizo,
Mume wangu alipata ajali na kufariki mwanzoni mwa mwaka huu huku akiniacha nikiwa na ujauzito wa miezi miwili, tangu kitokee kifo cha mume wangu nimekuwa na msongo wa mawazo, nimekuwa nikikosa usingizi muda mwingi usiku nakuwa macho, muda wote ninaokuwa macho nakuwa namfikiria tu marehemu mume wangu na hii hali huwa inanitokea hata mchana pia, usiku nikibahatisha kupata usingizi ninamuota pia.
Nimekuwa mtu wa kukosa furaha na kuwa na huzuni muda wote, muda mwingi nikiwa pekeyangu najikuta tu nalia, sipendi kukaa na watu au kuwa kwenye mkusanyiko wa watu wengi na pia najihisi hata utendaji kazi wangu kazini haupo sawa kwani nakuwa na hasira hata mtu akikosea kitu kidogo.
Nilifikiri labda nilijifungua tatizo hili litaisha kwakuwa mtoto atanifariji, namshukuru Mungu nilijifungua salama mwezi uliopita lakini mtoto amefanana sana na babake, kila ninapo mwona mtoto wangu namkumbuka baba yake nakuanza kufikiria vitu vingi na mawazo ndiyo yameongezeka zaidi.
Ninatamani kuwa na amani kama zamani ila nashindwa, naombeni ushauri namna ya kuepukana na hili tatizo na kama wapo hapa waliowahipatwa na tatizo hili naomba wanishauri jinsi walivyoweza kulimaliza.
Nashukuru kwa wote watakaonishauri
Mume wangu alipata ajali na kufariki mwanzoni mwa mwaka huu huku akiniacha nikiwa na ujauzito wa miezi miwili, tangu kitokee kifo cha mume wangu nimekuwa na msongo wa mawazo, nimekuwa nikikosa usingizi muda mwingi usiku nakuwa macho, muda wote ninaokuwa macho nakuwa namfikiria tu marehemu mume wangu na hii hali huwa inanitokea hata mchana pia, usiku nikibahatisha kupata usingizi ninamuota pia.
Nimekuwa mtu wa kukosa furaha na kuwa na huzuni muda wote, muda mwingi nikiwa pekeyangu najikuta tu nalia, sipendi kukaa na watu au kuwa kwenye mkusanyiko wa watu wengi na pia najihisi hata utendaji kazi wangu kazini haupo sawa kwani nakuwa na hasira hata mtu akikosea kitu kidogo.
Nilifikiri labda nilijifungua tatizo hili litaisha kwakuwa mtoto atanifariji, namshukuru Mungu nilijifungua salama mwezi uliopita lakini mtoto amefanana sana na babake, kila ninapo mwona mtoto wangu namkumbuka baba yake nakuanza kufikiria vitu vingi na mawazo ndiyo yameongezeka zaidi.
Ninatamani kuwa na amani kama zamani ila nashindwa, naombeni ushauri namna ya kuepukana na hili tatizo na kama wapo hapa waliowahipatwa na tatizo hili naomba wanishauri jinsi walivyoweza kulimaliza.
Nashukuru kwa wote watakaonishauri