Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Wapambanaji natumaini hasira za Jairogate zinapungua sasa. Hivyo naomba sasa mtulie mnipe Mwongozo wa kikatiba na kikanuni kuhusu bajeti ya serikali kwa muktadha wa bajeti ya Nishat na MadiniKwa kuwa sasa tunajua kwamba Kamati za Bunge zimekuwa zikihongwa kupitisha bajeti za serikali,Kwa kuwa Bajeti ya Nishati na Madini ilikutikana na kasoro za ujumlishaji na inasemekana bajeti zote zina kasoro hizo,Kwa kuwa Mkulo na Pinda walikwisha soma bajeti zao na kupitishwa na Bunge,Kwa kuwa bajeti ya Mkulo ilikuwa ni bajeti ya serikali nzima ikijumuisha ya Nishati,Kwa kuwa bajeti ya Pinda ilijumuisha halmashauri zote nchini ikiwa ni pamoja na idara za Nishati na Madini,Kwa kuwa bajeti ya Nishati na Madini imekataliwa hadi ikarekebishwe na kuongezwa kutoka kwenye bajeti za Wizara na idara zingine,JE?1. Baada ya marekebisho ya bajeti ya Nishati na Madini itabidi kurudia kujadili bajeti zilizopitishwa kabla hasa ya Mkulo na Pinda?2. Wabunge wetu wamepoteza sifa na uwezo wa kupitia bajeti za serikali hivyo watafutwe wataalamu ambao kazi yao ni kuchambua na kupitia bajeti za serikali?3. Wabunge wetu waendelee na upitishaji wa bajeti zilizobakia na bila kurekebisha zilizokwishapitishwa kana kwamba kurekebishwa kwa bajeti ya Nishati na Madini hakutaparaganya bajeti zingine?Naomeni majibu ya kikatiba na kikanuni