mchwa wanashambulia fremu za milango, milango yenyewe, makabati ya ukutani. Ajabu hata mchwa wenyewe siwaoni. Mwenye kujua dawa ama namna ya kukabiliana na hili tatizo anisaidie
Nyumba imejengwa kwenye msingi wa namna gani? Kama mchwa wanatokea chini kwenye msingi na kupanda kwenye fremu, hapo kazi unayo. Inabidi utafute professionals watakaotatua hilo tatizo kwa kushughulikia mchwa walioko ardhini chini ya msingi/nyumba. Kama mchwa wanatokea nje ya nyumba yako kupitia mapaa na madirisha, hapo unaweza ukaita wataalam wa "fumigation". All in all, it is very expensive kupata permanent solution. Ndio maana wakati wa ujenzi wa nyumba, suala la mchwa inabidi lifikiriwe toka mwanzo.
maduka ya mbao omc dawa ya mchwa watakupa. Ila kama umeweka sakafu ya cementi toa weka tiles, mchwa hawatapata upenyo. Na kutegemea unapoishi fanya ukaguzi mara kwa mara kwenye kuta nje ya nyumba kubaini mchwa wanapopanda ukuta kuelekea madirishani au milangoni uwauwe,kama una pesa weka madirisha ya alminium(spelling cjui ipo sawa)