Naombeni msaada: Dawa ya kupunguza uzito/unene/kitambi

Pastory Kimaryo

JF-Expert Member
Jan 16, 2018
967
664
Wana JF habarini, bila ya kupoteza muda na maneno mengi naombeni mnisaidie ushauri wa dawa nzuri ya kupunguza unene, hasa kitambi.

Nawategemea jamani
 
Sasa hizo dawa zinatengezwa ili iweje au mnataka kujibu tu muonekane mnajua kitu fulani, kama hamuwezi kutulia ndio mchangie ni bora mkae kimya watu waje na mbinu mseto hapa.
Afu mmekuja mpo limited na njia moja tu eti "fanya mazoezi" mnafikiri kila njia inawork sawa kwa kila mtu. Kwani mi sijui kama kufanya mazoezi kuna punguza uzito?
 
Sasa hizo dawa zinatengezwa ili iweje au mnataka kujibu tu muonekane mnajua kitu fulani, kama hamuwezi kutulia ndio mchangie ni bora mkae kimya watu waje na mbinu mseto hapa.
Afu mmekuja mpo limited na njia moja tu eti "fanya mazoezi" mnafikiri kila njia inawork sawa kwa kila mtu. Kwani mi sijui kama kufanya mazoezi kuna punguza uzito?
Unamkasirikia nani humu alikuambia uwe mzembe mzembe na kula kula?
Punguza wanga angalao nusu ya unaokula Sasa,jazia matunda mboga mboga za maji.

Fanya Mazoezi hasa sio unajidekeza kama mwali hizo Ndio dawa.

Huu Upuuzi mnaotangaziwa mtandaoni eti punguza mwili kwa siku 3 ni ujuha kabisa.
Angalia watoto wanaoenda JKT wakiwa mibonge ndani ya miezi mitatu anakuwa modo kabisa,au Unafikiri kule wanapewa dawa.Zoezi zoezi zoezi
 
Unamkasirikia nani humu alikuambia uwe mzembe mzembe na kula kula?
Punguza wanga angalao nusu ya unaokula Sasa,jazia matunda mboga mboga za maji.

Fanya Mazoezi hasa sio unajidekeza kama mwali hizo Ndio dawa.

Huu Upuuzi mnaotangaziwa mtandaoni eti punguza mwili kwa siku 3 ni ujuha kabisa.
Angalia watoto wanaoenda JKT wakiwa mibonge ndani ya miezi mitatu anakuwa modo kabisa,au Unafikiri kule wanapewa dawa.Zoezi zoezi zoezi
Nashukuru ndugu kwa ushauri wako ila kama kitu hukijui ni bora ukae kimya sio kupondea tu kisa huna uelewa na hicho kitu.
 
Hakuna dawa 'nzuri' ya kupunguza uzito unless unataka 'sumu' nzuri ya kupunguza uzito.

Talking through experience, ushauri wangu wa bure kwako ni huu - 'change life style' kwa kufanya yafuatayo:
  1. Fanya mazoezi karibia kila siku at least for 30 minutes i.e. Unaweza tumia free android app inaitwa 'Home Workout'
  2. Badili mfumo wako wa kula i.e Acha/ punguza kabisa kula wali, red meat, sembe na hata dona kula mara chache
Pia fanya yafuatayo:
  • Punguza portition ya chakula.
  • Kula mboga kama mlo kamili bila kuweka ugali, chapati ama wali.
  • Kula zaidi samaki, veggies na pia vyakula/ matunda yenye LOW GI Index
Kumbuka - Kufanya mazoezi ni tabia na si vifaa so no excuse, unaweza kuwa na vifaa na usifanye mazoezi hata siku moja.

Nakutakia utekelezaji mwema.
 
Nashukuru kwa uchangiaji wako mkuu.
Hakuna dawa 'nzuri' ya kupunguza uzito unless unataka 'sumu' nzuri ya kupunguza uzito.

Talking through experience, ushauri wangu wa bure kwako ni huu - 'change life style' kwa kufanya yafuatayo:
  1. Fanya mazoezi karibia kila siku at least for 30 minutes i.e. Unaweza tumia free android app inaitwa 'Home Workout'
  2. Badili mfumo wako wa kula i.e Acha/ punguza kabisa kula wali, red meat, sembe na hata dona kula mara chache
Pia fanya yafuatayo:
  • Punguza portition ya chakula.
  • Kula zaidi samaki, veggies na pia vyakula/ matunda yenye LOW GI Index
Kumbuka - Kufanya mazoezi ni tabia na si vifaa so no excuse, unaweza kuwa na vifaa na usifanye mazoezi hata siku moja.

Nakutakia utekelezaji mwema.
 
Speaking from a 1 year experience ya kupunguza kitambi na kujenga misuli, Dawa kama dawa ya kupunguza kitambi hakuna, zipo njia kuu 2 rahisi
1. (a) kupunguza kula vyakula vyenye calories nyingi (carbohydrates & fats/oil) mfano soda, keki, ugali/wali, beer, chips, vyakula vya kukaanga n.k
(b)kula sana vyakula vyenye calories chache. Mfano mboga mboga, matunda, nyama choma, kuku, samaki n.k. Kwa kifupi kufanya diet.
2. Fanya mazoezi. Sio lazima uende gym unaweza tu ukawa unatembea, jogging, kwenye majengo badala ya kupanda lift ukawa unatumia ngazi, ila kama nafasi unayo sio vibaya ukaenda gym. Mazoezi yanasaidia kuchoma calories mwilini.

Muhimu:
1). Calories ni kipimo cha nguvu iliyopo kwenye chakula. Kuna vyakula vina nguvu nyingi mfano ugali au wali. So unapokula mwili unatumia calories unazoihitaji TU zile zinazobaki zinahifadhiwa kama Fats na kwa case yako ni kitambi.

2). Ili kupungua ni lazima uupe mwili calories chache kuliko unazohitaji ILI lile gap liweze kulipwa na zile calories ambazo mwili umezihifadhi. Kwa mfano mwili unahitaji calories 2500 wewe unakula chakula chenye calories 2000, kwahiyo calories 500 zitatoka kwenye hazina ya mwili. Ukifanya hivi kwa muda mrefu utapungua

3). Huwezi kulenga kupunguza kitambi pekee, utakapoanza kupungua utapungua mwili mzima. Namaanisha kwamba, kutoka point ya (2) hapo juu, hizo calories 500 hauwezi kuamua zitoke kwenye kitambi, mikono au sehemu nyingine yoyote. Zinazotoka kwenye mwili mzima sio tu sehemu moja.

4). Dawa zinazotangazwa kuwa zinapunguza kitambi na kwamba ukizinywa unaenda kuharisha mafuta sio za kweli. Kitu ambacho zinafanya ni kuuzuia mwili wako usimeng'enye vizuri chakula kwa maana hiyo nguvu/calories nyingi kwenye chakula unachokula zinaishia chooni. Kwa mtindo huo, ni kweli utapungua ila afya itakongoroka kwa sababu mwili utakua haupati virutubisho badala yake unavitoa karibia vyote.

5). Kupunguza kitambi inachukua muda kwahiyo Usijiwekee matarajio ya muda mfupi. Ukikaza kwenye diet na ukafanya mazoezi matokeo yatakuja TU.
 
Speaking from a 1 year experience ya kupunguza kitambi na kujenga misuli, Dawa kama dawa ya kupunguza kitambi hakuna, zipo njia kuu 2 rahisi
1. (a) kupunguza kula vyakula vyenye calories nyingi (carbohydrates & fats/oil) mfano soda, keki, ugali/wali, beer, chips, vyakula vya kukaanga n.k
(b)kula sana vyakula vyenye calories chache. Mfano mboga mboga, matunda, nyama choma, kuku, samaki n.k. Kwa kifupi kufanya diet.
2. Fanya mazoezi. Sio lazima uende gym unaweza tu ukawa unatembea, jogging, kwenye majengo badala ya kupanda lift ukawa unatumia ngazi, ila kama nafasi unayo sio vibaya ukaenda gym.

Muhimu:
1). Calories ni kipimo cha nguvu iliyopo kwenye chakula. Kuna vyakula vina nguvu nyingi mfano ugali au wali. So unapokula mwili unatumia calories unazoihitaji TU zile zinazobaki zinahifadhiwa kama Fats na kwa case yako ni kitambi.

2). Ili kupungua ni lazima uupe mwili calories chache kuliko unazohitaji ILI lile gap liweze kulipwa na zile calories ambazo mwili umezihifadhi. Kwa mfano mwili unahitaji calories 2500 wewe unakula chakula chenye calories 2000, kwahiyo calories 500 zitatoka kwenye hazina ya mwili. Ukifanya hivi kwa muda mrefu utapungua

3). Huwezi kulenga kupunguza kitambi pekee, utakapoanza kupungua utapungua mwili mzima. Namaanisha kwamba, kutoka point ya (2) hapo juu, hizo calories 500 hauwezi kuamua zitoke kwenye kitambi, mikono au sehemu nyingine yoyote. Zinazotoka kwenye mwili mzima sio tu sehemu moja.

4). Dawa zinazotangazwa kuwa zinapunguza kitambi na kwamba ukizinywa unaenda kuharisha mafuta sio za kweli. Kitu ambacho zinafanya ni kuuzuia mwili wako usimeng'enye vizuri chakula kwa maana hiyo nguvu/calories nyingi kwenye chakula unachokula zinaishia chooni. Kwa mtindo huo, ni kweli utapungua ila afya itakongoroka kwa sababu mwili utakua haupati virutubisho badala yake unavitoa karibia vyote.

5). Kupunguza kitambi inachukua muda kwahiyo Usijiwekee matarajio ya muda mfupi. Ukikaza kwenye diet na ukafanya mazoezi matokeo yatakuja TU.
Nashukuru kwa ushauri wako
 
Wana JF habarini, bila ya kupoteza muda na maneno mengi naombeni mnisaidie ushauri wa dawa nzuri ya kupunguza unene, hasa kitambi.

Nawategemea jamani
Kimbia.
Anza kutembea haraka huku unakimbia kidogo
Ukiwa unapumzika usisimame tembea haraka
Then utakua ukiongeza kidogokodogo muda wa kukimbia mpaka uwe unakimbia full.
Anza na Km 3 then ongeza kila wiki.

#YNWA
 
Sasa hizo dawa zinatengezwa ili iweje au mnataka kujibu tu muonekane mnajua kitu fulani, kama hamuwezi kutulia ndio mchangie ni bora mkae kimya watu waje na mbinu mseto hapa.
Afu mmekuja mpo limited na njia moja tu eti "fanya mazoezi" mnafikiri kila njia inawork sawa kwa kila mtu. Kwani mi sijui kama kufanya mazoezi kuna punguza uzito?
Unapewa ushauri unatufokea. Bonge nyanya halafu jinga kabisa
 
Back
Top Bottom