Naombeni msaada: Baba yangu amechukua mkopo kwa dhamana ya nyumba niliyowajengea na ameshindwa kurejesha mkopo, ameniomba nimsaidie...

Ntikwite

Member
May 13, 2017
93
52
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 23, ni mfanyakazi wa Serikali, mwaka 2017 niliamua kuwajengea wazazi wangu nyumba ya kuishi na niliijenga kwa shida sana maana ilifika wakati nikachukua mkopo benki na hela yote nikapeleka kwenye hiyo nyumba na kiukweli nilijibana sana na kwa maumivu makubwa, lakini baada ya kumaliza ujenzi baba yangu aliingiwa na tamaa ya kutaka kukopa pesa benki kwa dhamana ya hiyo nyumba

Nirudi nyuma kidogo yaani kabla ya hii nyumba baba alikuwaga na nyumba nzuri lakini iliuzwa na Saccos mwaka 2006 kwa sababu ya mkopo wa namna hii, naendelea, mabishano kati yangu mimi na baba yalikuwa makubwa na mimi sikuwa na nguvu kwa sababu nilikuwa mbali na nyumbani na baadaye alichukua mkopo huo.

Alianza kurejesha marejesho benki na ilipobaki miez mitatu akafeli. Kiukweli sikutaka nyumba iuzwe kwa sababu hela iliyokuwa imebaki ilikuwa ni chache na nilikuwa naimudu coz alikuwa anatoa 194k per month for 1yr na makubaliano yetu yakawa akikopa tena sitakuja kuhusika.

Jamani mimi mpaka sasa siamini baba yangu amechukuwa Tsh. Milioni 5 mwezi uliopita kwa makubaliano ya kurejesha 472k per month for 1yr na juzi kanipigia simu kuwa amemaliza ile hela na kujuta sana kuwa amekosea sana na hela ameimaliza yote na ananiomba msaada tena nimsaidie, mimi kiukweli kipato changu hakitoshi hata kulipa hiyo hela ya kila mwezi coz tayari ninabmkopo.

Jaman mimi nifanyaje jamani nyumba inaniuma sanaa nashindwa kuelezea vizuri hapa ila nina mengi juu ya hili.

Naombeni msaada wa mawazo.
 
Kisheri ukilipa nusu ya deni unakuwa umeubadilisha mkopo wako, mtu akikopa na hajarudisha hata sh, huyu anakuwa mtu aliejipatia mali kwa njia ya udanganyifu hapa kesi yake ina ugumu kidogo,ukilipa robo ya deni unakuwa una unafuuu,ukilipa nusu ya mkopo unakuwa na unafuu said, sasa kama deni la nyumba limefika nusu nenda kwenye hiyo Sacco's ongea nao wakupe muda , yaaani lile deni lako walifanye mara 2 japo wanaweza kukuongea riba.

Mfano unadaiwa m2 na unalipa kwa mwezi laki 1,waombe wakupe mara mbili yake yaani uwe unalipa 50 elfu kwa hiyo utaongezewa muda zaid , ikishindikana ongea na mawakili wakusaidie , au kwa kuwa ww mfanyakazi selikalini ule mkopo wako omba ugawanye marejesho lkn ukatwe vile vile.

Fanya hivi ,kama ulikuwa unakatwa laki 2kwa mwezi omba hiyo pesa igawanywe mara mbili chukua akaunti ya ile taasisi aliokopa mzee wako uwe unawaingizia laki nawe kwenye deni lako unalipa laki, natumai utalipa japo kwa kuchelewa ,alafu nenda ktk ile nyumba andika kwa maaandishi makubwa nyumba hii ya ulithi haiwekwi dhamana kwa jambo lolote ogopa matapeli,

Sent from my itel S11 using JamiiForums mobile app
 
Hiyo nyumba ya mwanzo ni kama mlidhurumiwa jwa sasa mkiripot takukuru mbaweza igomboa kama mlikuwa na kumbu kumbu za malipo.
 
Kwa umri ulio nao jipinde ulipe huo mkopo.Usimtelekeze mshua wako.

Na pindi umalizapo huo mkopo,chukua hati andika jina la mama yako,au familia yote

BTW huo mkopo aliufanyia biashara!?
 
Dah pole,
mzee wako anatamaa, na hata ukimkwamua kwenye janga hili ataingia kwenye jingine.
Kama hiki kiwanja ni cha wazazi wako basi nunua hii nyumba kabisa, na ubadikishe hati ya nyumba iwe kwa jina lako na watoto wako waje qapate urithi hapo.
 
Huyo mzee itakuwa huwa anapendeza kila jioni.

Mkuu fanya kutafuta marafiki wa karibu wanaokuamini na imani unaweza kunusulu nyumba.

Ila madeni mengi uvunja urafiki!
 
Pole sana mkuu naelewa inavyouma, je baba alichukua mkopo kwaajili ya kufanyia nini hasa, je uliongea nae ukamuuliza alikopa kwasababu gani
 
Sometimes madingi tunazinguaga mbaya! Hapa ukipandwa na hasira unaweza kumtolea mbovu mshua!

Pole asee!
 
Nyumba ina hati? Kama ndivyo, ulipaswa kukaa na hati ili ashindwe kukopea na kuweka dhamana.

Hata sasa hujachelewa. Mwambie sharti la ww kulipa hilo deni ni akukabidhi hati ukae nayo wewe.

Tena ikibidi, kuwa mbinafsi kabisa. Badilisha jina hati transfer kwa jina lako. Naamini lengo ni wao wawe na pahali salama pa kuishi. Kwa umri wao, fanya kama nyumba ni yako ila umewaweka waishi bure for as long as they live. That way hata wakifariki baadae( ni njia yetu sote), huna migogoro ya mirathi kwa kuwa tayari nyumba ni yako kwa hati. And rightly so because uliikopea kujenga, na kuigomboa kwenye madeni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom