Naombeni mnifundishe jinsi ya kutengeneza mishkaki mitamu na laini

mchajikobe

JF-Expert Member
Aug 14, 2009
2,652
1,238
Jamani mwenzenu nina jiko nimenunua la kuchomea nyama, lakini kila nikichoma mishkaki haina ladha na ni migumu,wenye utaalam juu ya hili nisaidieni please.
 
Jamani mwenzenu nina jiko nimenunua la kuchomea nyama,lkn kila nikichoma mishkaki haina ladha na ni migumu,wenye utaalam juu ya hili nisaidieni plz
Andaa nyama yako kwa kukatakata vipande size ya kawaida.Hifadhi kwenye bakuli ama sufuria.Andaa viungo Kama tangawizi,kitunguu swaum na limao /ndimu /vinegar changanya kwenye nyama uliyoandaa kisha ifunike kwa dk45 hadi saa nzima.

Kabla ya kuchoma unaweza pia ongeza viungo Kama soy sauce ama berbercue sauce na chumvi kiasi.

Natumaini utakua umeandaa jiko. Choma mishkaki yako kwa moto wa kiasi ili iive vizuri. Serve kwa chachandu na salad na chakula upendacho Kama chips,ndizi Choma ama ugali.Enjoy
 
Andaa nyama yako kwa kukatakata vipande size ya kawaida.Hifadhi kwenye bakuli ama sufuria.Andaa viungo Kama tangawizi,kitunguu swaum na limao /ndimu /vinegar changanya kwenye nyama uliyoandaa kisha ifunike kwa dk45 hadi saa nzima.Kabla ya kuchoma unaweza pia ongeza viungo Kama soy sauce ama berbercue sauce na chumvi kiasi.Natumaini utakua umeandaa jiko. Choma mishkaki yako kwa moto wa kiasi ili iive vizuri. Serve kwa chachandu na salad na chakula upendacho Kama chips,ndizi Choma ama ugali.Enjoy
Asante kwa darasa
 
Inategemeana na aina ya nyama unayotumia.si kila nyama inafaa kuchoma mishkaki.ongea na alwatan wa bucha akuelekeze nyama ipi inafaa
 
Nadhani hakuuliza kuwa Nyama gani inafaa kwa mishikaki?
Anko mbona unataka kuanza ligi asubuhi namna hii.Amesema nyama haina ladha na inakuwa ngumu.logicaly inamaana kuna kitu anakosea.eidha kwenye kuandaa,kwenye kuchoma,ama aina ya nyama anayotumia.mimi sio mjuaji nimetoa tu angalizo hapo
 
  • Thanks
Reactions: amu
Anko mbona unataka kuanza ligi asubuhi namna hii.Amesema nyama haina ladha na inakuwa ngumu.logicaly inamaana kuna kitu anakosea.eidha kwenye kuandaa,kwenye kuchoma,ama aina ya nyama anayotumia.mimi sio mjuaji nimetoa tu angalizo hapo
Nilidhani ungeanza kumuelekeza kuwa nini afanye ili mishikaki yake iwe raini na yenye radha,, then mwishoni ndo umpe angalizo lako, coz Nyama inayofaa kwa Mishikaki haiwezi Tu kuwa raini na yenye radha bila kuweka viungo kama Mdau alivyosema hapo juu post # 3.
 
Habari wanajamvi!

Naomba kujuzwa kuhusu biashara ya mishikaki has a inayouzwaa barabarani karibu na vituo vya daladala.

Ni maarufu sana kwa mkoa wa Dar es salaam. Mwenye experience nayo anijuze mtaji kwa kuanzia ni shilingi ngapi? Na kijana anayechoma unamlipa shilingi ngapi kwa siku? Pia ushauri na maoni yanakaribishwa. Natanguliza shukrani.
 
Aisee ngoja nikupe mbinu kidogo
Kwanza 98% ya wale wachoma mishkaki ni mitaji yao,yaani wao ndio matajiri,maana ni mitaji midogo sana. Na ile kazi haina guarantee,maana watu wa Afya na city wakitibuka zoazoa inaanza.Unless kwa wale wenye Banda zao.

Ushauri,tafuta eneo mwenye kisha chomoa kijana Bush au kwenye familia yenu kisha mfungulie. Ukitaka kujua faida kama una mke muulize atakupa jibu,utafaham umuhim wa kuoa hapa mkuu, hahahha.

Maana mke yoyote alielelewa Jikoni sio hao wapaka rangi,ukimuuliza tu anakujibu kwamba Idadi ya kilo inatoa wastan wa mishkaki mingapi then unapiga hesabu hapo na una relate na cost ndogo za mkaa nk ambazo zinajulikana
 
Hii biashara nilishaifanya sana na ina faida sana. Na faida yake inategemeana sana;

1. Uzuri au ubora wa nyama utakayopata toka buchani,

2. Utalaam wa jinsi ya kukakata/ kucharanga vipande.

3. uchomaji mzuri, kwani ukiunguza sana inapungua ubora au radha na kusababisha kupoteza wateja.

5 Utumiaji mzuri wa mkaa, hakikisha unakuwa na maji kwenye chupa ili kupunguza kiwango cha moto kwenye jiko, hivyo kupunguza matumizi ya gharama yamkaa
 
Unaweza tia paste ya tamarind au yoghort, chumvi, kitunguu saumu, tangawizi na pilipli manga. Aiche kwa muda wa lisaa.
 
Jamani mwenzenu nina jiko nimenunua la kuchomea nyama,lkn kila nikichoma mishkaki haina ladha na ni migumu,wenye utaalam juu ya hili nisaidieni plz
Ukiweka viungo kiasi cha kutosha na kuiacha ikae kwenye viungo (marinated) inapata ladha na kuwa laini... viungo vya kutengeneza ladha tamu ya mishikaki ni vinegar au limao au ndimu, kitunguu saumu, kitunguu maji unakata vicube vidogo vidogo, chumvi kiasi, tangawizi, pili pili manga ya unga, mafuta ya maji (ya alizeti, au olive,) huu mchanganyiko ndo unachanganya na nyama kisha unaifunika viungo vifanye kazi yake kwa saa moja hivi. Wengine huweka na papai bichibichi lilipondwa ili kulainisha nyama mana yanakuwa na enzyme fulani ya kulainisha protein/nyama.

Unaweka mafuta kwasababu ni rahisi kwa mafuta kufyonza harufu nzuri ya viungo hivyo yanaingia kwenye nyama na nyama kupata harufu nzuri.

Iwapo jiko lako la kuchomea nyama lina mfuniko hakikisha unafunika mvuke usitoke maana mvuke hulainisha ile nyama. Iwapo halina mfuniko, tumia sufuria kubwa kufunika mishikaki yako kwa muda ili mvuke ulainishe.

Yale maji yanavodondokea kwenye moto ndo yanaleta mvuke.
 
Ukitaka mishikaki iwe laini ikande na papai lililoiva then weka pembeni kama nusu saa choma mishkaki yako
 
Wanajukwaa biashara ya mishkaki inanivutia na ninaona ni rahisi kuimudu!! bt naombeni ushauri. nina kianzio cha sh 150000/=
 
Back
Top Bottom