Naombeni mawazo jamani

mjasiria2mbo

Member
Apr 23, 2014
43
18
Mwenzenu nimeolewa,naishi na binti wa kazi na tunapoishi ni nyumba ambayo mume wangu alianzia maisha so ni chumba na sebule tuu!

Binti huwa namlaza kwa sebule na godoro dogo tu sasa mume wangu ana kaka yake anaishi huko na ana familia cha ajabu huwa anaweza akaja hapa kwangu na hakuna cha maana anakuja kufanya sasa akija manake namlaza apo sebuleni na binti ni inabidi nimuombee kwa jirani ajibane kulala sasa mi hiki kitu kwa kweli kinanikwaza!
 
Kazana pigana..jihusishe kwenye biashara ndogondogo jikaze ujenge nyumba.. Kero zote zitapungua
Mwenzenu nmeolewa,naishi na binti wa kazi na tunapoishi ni nyumba ambayo mume wangu alianzia maisha so ni chumba na sebule tuu! Binti huwa namlaza kwa sebule na godoro dogo tu sasa mume wangu ana kaka yake anaishi hko na ana familia cha ajabu huwa anaweza akaja hapa kwangu na hakuna cha maana anakuja kufanya sasa akja manake namlaza apo sebulen na binti ni inabidi nimuombee kwa jiran ajibane kulala sasa mi hiki kitu kwa kweli kinanikwaza!
 
ongea na mumeo
hasikubebeshe mzigo bure... na ndugu yake huyo hana akili
anashindwa kusoma mazingira
dah! Familia zingine ni joto jaman
 
Ndo kwanza tuna miez tu ndugu Jawilat tutajenga tu lakini kwa sasa nafanyaje mana usiku napita apo seblen naenda uani labda ni shida
 
Majigo yule ni kaka yake sasa nikimwambia wasijeona labda sipendi ndugu si unajua moyo wa mtu ndugu?
 
Ndiyo maana nasemaga siku hizi hakuna wife material.
Hivi wewe ndoa hata haijamaliza mwaka tayari una hausemaid wanini?
 
Tafuta hela bibie upange nyumba kubwa, ndo suluhisho! Tena utafute wewe hio hela, ukimngoja mume utasubiri sanaaaa! Kwa sie wazee wa mjini kupata kodi ya chumba cha pili sio ishu kabisaa kwetu! Unafunga macho mara 1, unajiachie mwaka mzima! Hata uje ukoo!

Tangia hapo ushukiru maana una chumba na seble, mwingine ana chumba kimoja na baba mkwe ndani, so wewe ndo unaenda kulala kwa jirani! Chezea jiji wewe!
 
Mwambie mumeo apige marufuku wageni wote wa kulala, waje kutembea tu.

Angekuwa kwangu ningemwambia ukija mjini hulali kwangu, tafuta pa kulala
 
Kama hali ya mumeo hairuhusu vumilia mambo madogo na ya mpito kama hayo
 
Mambo mengine hata uya handle vipi lawama ip pale pale so you have to do what is right.

Face your husband.
 
Ndo kwanza tuna miez tu ndugu Jawilat tutajenga tu lakini kwa sasa nafanyaje mana usiku napita apo seblen naenda uani labda ni shida

House girl wa nini na wewe una chumba na sebule huna mtoto.
Jamani mbona mizigo mnajibebesha wenyewe utasema kazi mbona sir mabachelor na tunaishi na wadogo zetu wadogo tuna mudu.
weekend unaingia jikoni unapika hasa,usafi huku mume anakusaidia hata asipokusaidia ile kukaa tu we wafanya kazi inasaidia kukuspeed up.
Jiko za mchina,za gesi zipo siku hizi chakula fasta.
Shopping vyakula fanya ijumaa kama ukitoka au wikiend ukipata.
haaa ndoa ina miezi huinjoy kujibana na watu.
Hapo ulipo ndo mwapo kuinjoy mara sebuleni kwa kochi,mara chini yaani full raha mara wafanya usafi huku wamdandia shem.
Mwanamke jiongeze bana!!!!
 
Tafuta hela bibie upange nyumba kubwa, ndo suluhisho! Tena utafute wewe hio hela, ukimngoja mume utasubiri sanaaaa! Kwa sie wazee wa mjini kupata kodi ya chumba cha pili sio ishu kabisaa kwetu! Unafunga macho mara 1, unajiachie mwaka mzima! Hata uje ukoo!

Tangia hapo ushukiru maana una chumba na seble, mwingine ana chumba kimoja na baba mkwe ndani, so wewe ndo unaenda kulala kwa jirani! Chezea jiji wewe!

Hayo maneno mekundu maana yake nini?
 
Bibie Karucee kwa kweli sitokusahau, nimeiona PM yako ulionitumia jana kwa kweli

Nimejifunza kitu muhimu sana kutoka kwako, wachache sana wenye uwezo kama wako.

Hivi wewe umesomea nchi gani hapa ulimwenguni?! Maana una elimu kweli.

Naomba uwe unaendelea kunipa mazoezi ya Elimu kwa PM, ila tatizo siku hizi umekuwa mvivu yaani mara tatu kwa wiki, zamani ulikuwa unanifundisha kila siku.

Najua nimetoka nje ya mada ili nimekuona upo hewani ndio nikaamua kukufahamisha nimeiona PM yako.

Wee mkali
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom