Naombeni kujua jina la huu wimbo

Rutunga M

JF-Expert Member
Mar 16, 2009
1,769
1,382
Kuna wimbo mmoja wa dansi wa miaka ya 2000 kutoka kwa moja ya bendi za hapa hapa nchini. Naweka chini baadhi ya maneno maarufu yaliyomo katika wimbo huo ili mnisaidie kuujua jina ili niupate.

Ndani una majigambo ya kujibizana kama hivi:

Mtu no 1: Usiku nilisikia shemeji analia
Mtu no 2: Ahaa pale nilishamchapa
Mtu no 1: Kwanini?
Mtu no 2: Aliingiza mwenyewe akashindwa kutoa
Mtu no 1: Nini?
Mtu no 2: Mkanda wa video kwenye deki
kiitikio yalahaaaa!

Hapo juu ni moja ya maneno yaliyokuwa maarufu wakati huo kutoka kwenye huo wimbo.

Asante!
 
Ha ha ha! Jamaa kaupata fasta ila ulizia Sasa ambao hauna maneno ya Hivyo!! Kuupata utahitaji maombi
 
Huo ni wimbo wa Tanzania One Theatre (TOT) enzi za akina Abdul Misambano, Leyla Rashid na Banza. Wimbo unaitwa Sweet baby. Nadhani upo youtube. Ukiukosa basi utafute humu JF. Kuna thread moja hivi nimeuweka
Kuna wimbo mmoja wa dansi wa miaka ya 2000 kutoka kwa moja ya bendi za hapa hapa nchini. Naweka chini baadhi ya maneno maarufu yaliyomo katika wimbo huo ili mnisaidie kuujua jina ili niupate.

Ndani una majigambo ya kujibizana kama hivi:

Mtu no 1: Usiku nilisikia shemeji analia
Mtu no 2: Ahaa pale nilishamchapa
Mtu no 1: Kwanini?
Mtu no 2: Aliingiza mwenyewe akashindwa kutoa
Mtu no 1: Nini?
Mtu no 2: Mkanda wa video kwenye deki
kiitikio yalahaaaa!

Hapo juu ni moja ya maneno yaliyokuwa maarufu wakati huo kutoka kwenye huo wimbo.

Asante!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Okay, maneno yalinishtua kidogo
emoji2.png


Sent using Jamii Forums mobile app

Huu hapa. Sikiliza kuanzia 5:20
Pia muuliza swali achukue hapa.


Update.

Sorry umegoma kutumwa hapa. Ninao, ni mp3. Unaitwa sweet baby wa Tot
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom