Standards Person
JF-Expert Member
- Apr 22, 2021
- 673
- 859
Ninampongeza sana Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani hivi karibuni kupitia ukurasa waofisi yake na ule wa msemaji mkuu wa serikali imeweka akaunti yake ya Instagram inayojulikana kama kassim_m_majaliwa.
Hiyo ni hatua nzuri kwani wananchi walio wengi watamfikishia taarifa mbalimbali kwa usiri, ukaribu na haraka zaidi lakini ninaomba viongozi wakuu serikalini wawe na akaunti zinazotambulika hapa JF ndio itakua rahisi zaidi kuwaambia mambo kinagaubaga.
Hivyo basi waziri mkuu, makamu wa Rais na Mh. Rais waweke akaunti zao na majina halisi hapa ili wapewe taarifa mbalimbali.
Viongozi wanaojiamini waadilifu na watenda haki hawaoni tabu kuweka mawasiliano yao hadharani ili jamii ishiriki nao kwapamoja kusukuma gurudumu la maisha.
Raia wakiwa wanatendewa haki na wakiwa wastaarabu watatumia njia hizo kistaarabu bila tatizo
Hiyo ni hatua nzuri kwani wananchi walio wengi watamfikishia taarifa mbalimbali kwa usiri, ukaribu na haraka zaidi lakini ninaomba viongozi wakuu serikalini wawe na akaunti zinazotambulika hapa JF ndio itakua rahisi zaidi kuwaambia mambo kinagaubaga.
Hivyo basi waziri mkuu, makamu wa Rais na Mh. Rais waweke akaunti zao na majina halisi hapa ili wapewe taarifa mbalimbali.
Viongozi wanaojiamini waadilifu na watenda haki hawaoni tabu kuweka mawasiliano yao hadharani ili jamii ishiriki nao kwapamoja kusukuma gurudumu la maisha.
Raia wakiwa wanatendewa haki na wakiwa wastaarabu watatumia njia hizo kistaarabu bila tatizo