Naomba Uzoefu wa zao la nazi

JF Member

JF-Expert Member
Dec 14, 2014
7,360
9,615
Kwa haraka haraka nimeambiwa hiki kilimo kina lipa.
Naambiwa shina Moja la Nazi linatoa Nazi 15 hadi 20 kila baada ya miezi 2.
Ukiwa na mashina 1,000 una Nazi 15,000.

Ukiuza kwa 600 kila Nazi ( 1,500 x Shilingi 600) ni sawa na Shilingi 9,000,000 kila baada ya miezi miwili.

Wastani wa 4,500,000 kila mwezi.

Wajuzi mnaushauri gani?
 
Mnazi hadi uje kuanza kutoa nazi nyingi ni baada ya kupita miaka kadhaa (siwezi kutaja miaka, kwa sababu inategemea na aina ya mnazi) pamoja na kwamba kuna minazi inaweza kuanza kuzaa ikiwa na miaka 3, lakini inakuwa midogo/umbo dogo kwahiyo haiwezi kubeba nazi nyingi. Ni mpaka iwe mikubwa, yaani iwe na shina kubwa/Nene, na makuti mengi ili uweze kushikilia mzigo wa nazi. Ni sawa na mtoto mdogo anaweza kula kutembea nk lakini hawezi kubeba mzigo mzito lakini mtu mzima anaweza.

Kwahiyo uwe mvumilivu utaanza kuvuna nazi kwa uchache huku unaendelea kukua na kuwa mkubwa, kwa kifupi fanya uwekezaji, usitegemee kupata fedha nyingi ndani ya miaka 4-7, labda baada ya miaka 10.

Nakushauri fanya huo mradi, utafaidika nao baadaye, pia bei ya nazi Ni 500-600, ukiwa na nazi usipeleke sokoni, ingia nazo mtaani, ( kwa Dar na Pwani)sokoni bei ni kuanzia 600 na kuendelea wewe uza 500 fasta unamaliza hata zikiwa nyingi. Kwenye masoko kuna dhuluma zinafanyika watakuambia nazi ndogo, hazijakomaa nk, maneno yatakuwa mengi ili ushushe bei.

Naongea kutokana na uzoefu, mzee wangu alipanda minazi miaka ya 1989, 1990 na 1993, bado anavuna.

Kwa ushauri vijana tuwekeze kwenye kilimo kama cha minazi, korosho, michikichi nk uzeeeni tuishi maisha mazuri, vijana wa wakati huo watuite Freemason utasikia "huyu mzee hafanyi kazi, amestaafu lakini ana pesa nyingi, atakuwa Freemason"

Uzuri wa kilimo cha aina hii hakihitaji usimamizi mkubwa, unafanya kazi zako mjini, weekend unatembelea shamba lako.
 
Mnazi hadi uje kuanza kutoa nazi nyingi ni baada ya kupita miaka kadhaa(siwezi kutaja miaka,kwa sababu inategemea na aina ya mnazi)pamoja na kwamba kuna minazi inaweza kuanza kuzaa ikiwa na miaka 3,lakini inakuwa midogo/umbo dogo kwahiyo haiwezi kubeba nazi nyingi .Ni mpaka iwe mikubwa,yaani iwe na shina kubwa/Nene, na makuti mengi ili uweze kushikilia mzigo wa nazi.Ni sawa na mtoto mdogo anaweza kula kutembea nk lakini hawezi kubeba mzigo mzito lakini mtu mzima anaweza.
Kwahiyo uwe mvumilivu utaanza kuvuna nazi kwa uchache huku unaendelea kukua na kuwa mkubwa,kwa kifupi fanya uwekezaji,usitegemee kupata fedha nyingi ndani ya miaka 4-7,labda baada ya miaka 10.

Nakushauri fanya huo mradi ,utafaidika nao baadaye,pia bei ya nazi Ni 500-600, ukiwa na nazi usipeleke sokoni,ingia nazo mtaani,( kwa Dar na Pwani)sokoni bei ni kuanzia 600 na kuendelea wewe uza 500 fasta unamaliza hata zikiwa nyingi.Kwenye masoko kuna dhuluma zinafanyika watakuambia nazi ndogo,hazijakomaa nk,maneno yatakuwa mengi ili ushushe bei.

Naongea kutokana na uzoefu ,mzee wangu alipanda minazi miaka ya 1989,1990 na 1993,bado anavuna.

Kwa ushauri vijana tuwekeze kwenye kilimo kama cha minazi,korosho,michikichi nk uzeeeni tuishi maisha mazuri,vijana wa wakati huo watuite Freemason utasikia "huyu mzee hafanyi kazi, amestaafu lakini ana pesa nyingi, atakuwa Freemason"
Uzuri wa kilimo cha aina hii hakihitaji usimamizi mkubwa,unafanya kazi zako mjini , weekend unatembelea shamba lako.
Umeongea vema ila kwa kuboresha minazi ya kisasa yaan 3yrs unanza kunufaika hasa kuanzia mwk wa 5 -7 hyo awamu ya kwanza ila mwk wa 7 -15 mti 1 unatoa mpka naz 40 kwa mwaka ,hivyo ili ufurahie zao hil panda ekari 10 utakuja nishukuru na kwel utaitwa freemanson
 
Mnazi hadi uje kuanza kutoa nazi nyingi ni baada ya kupita miaka kadhaa(siwezi kutaja miaka,kwa sababu inategemea na aina ya mnazi)pamoja na kwamba kuna minazi inaweza kuanza kuzaa ikiwa na miaka 3,lakini inakuwa midogo/umbo dogo kwahiyo haiwezi kubeba nazi nyingi .Ni mpaka iwe mikubwa,yaani iwe na shina kubwa/Nene, na makuti mengi ili uweze kushikilia mzigo wa nazi.Ni sawa na mtoto mdogo anaweza kula kutembea nk lakini hawezi kubeba mzigo mzito lakini mtu mzima anaweza.
Kwahiyo uwe mvumilivu utaanza kuvuna nazi kwa uchache huku unaendelea kukua na kuwa mkubwa,kwa kifupi fanya uwekezaji,usitegemee kupata fedha nyingi ndani ya miaka 4-7,labda baada ya miaka 10.

Nakushauri fanya huo mradi ,utafaidika nao baadaye,pia bei ya nazi Ni 500-600, ukiwa na nazi usipeleke sokoni,ingia nazo mtaani,( kwa Dar na Pwani)sokoni bei ni kuanzia 600 na kuendelea wewe uza 500 fasta unamaliza hata zikiwa nyingi.Kwenye masoko kuna dhuluma zinafanyika watakuambia nazi ndogo,hazijakomaa nk,maneno yatakuwa mengi ili ushushe bei.

Naongea kutokana na uzoefu ,mzee wangu alipanda minazi miaka ya 1989,1990 na 1993,bado anavuna.

Kwa ushauri vijana tuwekeze kwenye kilimo kama cha minazi,korosho,michikichi nk uzeeeni tuishi maisha mazuri,vijana wa wakati huo watuite Freemason utasikia "huyu mzee hafanyi kazi, amestaafu lakini ana pesa nyingi, atakuwa Freemason"
Uzuri wa kilimo cha aina hii hakihitaji usimamizi mkubwa,unafanya kazi zako mjini , weekend unatembelea shamba lako.
Naomba kuuliza eneo la kilimo cha minazi unaweza lima pia mchikichi?

#MaendeleoHayanaChama
 
Katika ekari 1 inapandwa miche mingapi ya minazi ?

Au mpangilio wa shamba unakuwaje yaani UREFU kunakuwa na umbali wa mita ngapi toka mnazi mmoja kwenda mwingine, hivyo hivyo kwa UPANA toka mnazi mmoja kwenda mnazi mwingine inakuwa mita ngapi ?

Kuna suala la

1. Miche
2. Mbegu
3. Uhakika wa ubora wa miche
4. Mashimo na ukubwa wake
5. Changamoto za udongo, magonjwa na hali ya hewa
6. Na kadhaalika
 
Kwa haraka haraka nimeambiwa hiki kilimo kina lipa.
Naambiwa shina Moja la Nazi linatoa Nazi 15 hadi 20 kila baada ya miezi 2.
Ukiwa na mashina 1,000 una Nazi 15,000.

Ukiuza kwa 600 kila Nazi ( 1,500 x Shilingi 600) ni sawa na Shilingi 9,000,000 kila baada ya miezi miwili.

Wastani wa 4,500,000 kila mwezi.

Wajuzi mnaushauri gani?
Piga hesabu vizuri ni 900000
 
Back
Top Bottom