Naomba ushauri

herimimi

Member
Aug 4, 2011
62
10
mimi nimeoa jirani sana na nyumbani kwetu. tangu nimeoa sijawahi kulala ukweni kwa sababu ni mwendo wa dakika tu kutoka kwetu hadi ukweni. rafiiki yangu anasema kuwa kitendo cha kutolala na mke wangu kwao ni kutomtendea haki kwani yeye analala kwetu. anasema ni vizuri kwa mahusiano kulala ukweni na mkeo eti inakuongezea heshima toka kwa wazazi wa mke wako! mimi kweli sielewi lakini mke wangu anasapoti. naombeni ushauri wenu.
 
Mambo mengine bana. Kama hakuna madhara yoyote wewe kalale tu uwafurahishe wakwe.
 
Sijaelewa vizuri... inamaana wewe unakaa kwenu na mkeo ama hua manalala kwenu mkienda kutembea huko nyumbani?? Alafu mila ya makabila mengi ya hapa Tz sio heshima mwanaume kulala kwa wakwe na Mkewe labda in speacial cases.. mbona kitendawili... mbaya zaidi anaesema hivo na kukupa headache ni rafiki wala hata sio wakwe.... kuna nini hapa Herimini??
 
Kulala ukweni ni heshima?
Mi mbado kusikia hii
Huyo rafiki yako anakupa ushauri wa giza tena hata sijjui kama anajua nini maana ya wakwe
Hakuna cha heshima wala nini we kaa kwako bana na ndo maana ukaoa. Ingekuwa heshima ungemuacha mkeo kwa wazazi wake ukiwa na hamu nae unaenda kwa wakwe unafanya unalotaka then unarudi kwako
 
Sijaelewa vizuri... inamaana wewe unakaa kwenu na mkeo ama hua manalala kwenu mkienda kutembea huko nyumbani?? Alafu mila ya makabila mengi ya hapa Tz sio heshima mwanaume kulala kwa wakwe na Mkewe labda in speacial cases.. mbona kitendawili... mbaya zaidi anaesema hivo na kukupa headache ni rafiki wala hata sio wakwe.... kuna nini hapa Herimini??


tunalala kwetu tukienda kuwasalimia wazazi wetu..naambiwa siku nyingine tulale ukweni!
 
tunalala kwetu tukienda kuwasalimia wazazi wetu..naambiwa siku nyingine tulale ukweni!


Hapo nimekupata... sijui kwa mila zetu, kama mnaishi karibu ina maana hata mila zenu wewe na Mkeo za fanana.... Fuatilia na uliza wazee wako kama ni kweli hayo maneno (thou bado siamini)... Mimi kama mtoto wa kike naweza ona aibu saana kutoka chumbani na mume wangu hata kama hatujafanya kitu... alafu nagongana na wazazi asubuhi... Liangalie kwa umakini hili suala...
 
Ashadii hapo ndio ninapoona kituko. Unaamka asubuhi na mkeo hata kama hamkufanya lolote unakutana na mama mkwe mlangoni au koridoni mnaangalianaje na wanafikiria nini vichwani mwao
Ahh hata kama ni mila hizo nyingine ni balaa bana
 
Ashadii hapo ndio ninapoona kituko. Unaamka asubuhi na mkeo hata kama hamkufanya lolote unakutana na mama mkwe mlangoni au koridoni mnaangalianaje na wanafikiria nini vichwani mwao
Ahh hata kama ni mila hizo nyingine ni balaa bana


Hapa ndo unatamani hata uulize wife ana age gani... ili walau kuelewa, kweli katika mila zetu za ki Africa leo ndo kusikia... Wengine hata ukiwa na ujauzito tu unaona aibu kwenda home...
 
huyo si rafiki mzuri, mkimbie. Mwanaume huwa ni aibu kukaa ukweni. Mkeo akikung'ang'aniza mwambie wewe ndo umeoa,hujaolewa.
 
haina haja kulala ukweli kama ni karibu, labda ingekuwa ni mkoa mwingine mbali na kwenu mmekwenda kusalimia sawa lakini hapo hapo karibu ulale kwao ili iweje? hata wazazi wako watakuona ze comedy. vitu vingine bwana usiishi kwa kuogopa watu bali we ishi kadiri unavoona inakufaa wewe lakini isiwe kinyume na morals, sasa kulala kwa wakwe ndio utawaongea heshima? maisha? sifa au?? we kidume bwana umeoa lala kwako.
 
mimi nimeoa jirani sana na nyumbani kwetu. tangu nimeoa sijawahi kulala ukweni kwa sababu ni mwendo wa dakika tu kutoka kwetu hadi ukweni. rafiiki yangu anasema kuwa kitendo cha kutolala na mke wangu kwao ni kutomtendea haki kwani yeye analala kwetu. anasema ni vizuri kwa mahusiano kulala ukweni na mkeo eti inakuongezea heshima toka kwa wazazi wa mke wako! mimi kweli sielewi lakini mke wangu anasapoti. naombeni ushauri wenu.

Mimi mila na desturi yangu hainiruhusu kwenda kulala kwa mama/baba mkwe. Na hili kwetu linaongeza sana heshima kwa wazazi wa mke. Hivyo nina zaidi ya miaka kumi kwenye ndoa na sijawahi kulala huko. Sana sana huwa niawatembelea na kuondoka.
 
huh...............kwahiyo bro umeoa bado upo maskani?basi ka ndo hvo nenda na wwe mkalale kwao kidogo
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom