Mkomawatu
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 267
- 118
Habari zenu wadau wenzangu wa JF, kwa kuthamini mchango wenu katika masuala mbalimbali ya kisiasa hapa nchini, nimeamua kuandika waraka huu kuomba ushauri wenu kwenu namna ambavyo naweza nikaendesha harakati zangu za kisiasa kwa lengo la kuwakomboa watu wa tabaka la chini ulimwenguni kote, nimemaliza chuo kikuu cha Dodoma ambako kule nilishika nafasi ya Mbunge serikali ya wanafunzi, lakini pia nilikuwa miongoni mwa wadau waandamizi katika Jumuiya ya Vijana Umoja wa mataifa tawi la UDOM na pia mdau mwanzilishi wa Anti corruption society pale chuoni, naomba ushauri wenu ni taasisi gani naweza nikajiunga nayo na kuweza kufanikisha ndoto zangu? Nataka Watanzania na dunia ifaidike na uwepo wangu.