Naomba ushauri wenu katika hili

Machmadem

JF-Expert Member
Jul 9, 2017
758
933
Habali zenu

Naomben ushauri jamani niko njia panda. Nifanye nini katika hili. Nipo katika mahusiano ni Taktiban miez 2 ila shida iko sehemu moja huyu bidada nilienaye ana wivu yes wivu haswaa uliopitiliza asione sim imepigwa atataka ajue, asione naongea na jinsia tofauti ndo kabisa ni mwendo wa kununa ka paka aliyekosa maziwa kwakwel hii kitu mimi siwezi vumilia napenda uhuru katka ishu nzima ya mahusiano sasa nawaza nifanye kipi kutatua hii disaster.

Nimejaribu kuandika kwa ufupi ila yapo mengi tu. Naombeni ushauri wenu jamani ni nifanye nini
 
Kumshinda na wivu wake wewe kuwa mkweli tu..kila anachotaka kujua mwambie akitaka kukagua simu mpe akague mwisho wake atachoka ataona anajisumbua tu.
Sasa si atakuta meseji za michepuko ya jamaa
 
Katika hili usijidanganye kuwa utaweza kumrekebisha.. HUYU ACHANA NAYE TU.. Kuna siku utakuwa unaongea namama yako halafu aje atoe mineno ya ajabu na mama aisikie ndo tabu itakapoanza.. AU hata kwa dada au ndugu zako wengine
 
Ukikiona hivyo ujue alishatendwa xx mpk akakosa imani kuwa kweny mahusiano... Xx hapo ameingia kwny mahusiano na ww ndy kama hivy anajitahidi kuwa makini ktk kukufuatilia kwmb yasije kutokea kama ya mwanzo.. we kama uko serious na huyo dada zungumza naye.. mueleze wazi kwmb hulipendi jambo hilo kwasababu ww umempenda yy tu na kwmb huwezi kumcheat.. na umuonyeshe matendo/upendo ambao utamfany yy akuamini.. basi hapo lzm atakaa sawa.. ila hapo ujue kbs kwmb mwenzio alishakataga tamaa sema tu ndy ameamua kujaribu kuingia tena kwny mahusiano.
 
Ukikiona hivyo ujue alishatendwa xx mpk akakosa imani kuwa kweny mahusiano... Xx hapo ameingia kwny mahusiano na ww ndy kama hivy anajitahidi kuwa makini ktk kukufuatilia kwmb yasije kutokea kama ya mwanzo.. we kama uko serious na huyo dada zungumza naye.. mueleze wazi kwmb hulipendi jambo hilo kwasababu ww umempenda yy tu na kwmb huwezi kumcheat.. na umuonyeshe matendo/upendo ambao utamfany yy akuamini.. basi hapo lzm atakaa sawa.. ila hapo ujue kbs kwmb mwenzio alishakataga tamaa sema tu ndy ameamua kujaribu kuingia tena kwny mahusiano.
Asante sana
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom