Namshukuru Mwenyezi Mungu mke wangu amejifungua salama baada ya miezi kumi ya ujauzito. Wakuu naomba kufahamu vyakula gani anaweza kula mama aliyejifungua ili aweze kurecover haraka?
Jitahidi ale balanced diet tu, yaani mlo kamili ambao utakua na makundi yote ya vyakula. Ila moja ya vyakula vinavyohitajika kwa wingi ni
1)PROTEIN. apate protein za kutosha ili kusaidia tissue renewal na kuzalisha maziwa ya mtoto wake .(Nyama, maharage, karanga, samaki, maziwa, mayai)
2)IRON + VITAMINS. Vyakula vya madini ya chuma(iron) na vitamins kwa ajili ya kupambana na anaemia maana mama anaweza kua amepoteza damu nyingi kipindi cha kujifungua. (Maini,dagaa,matunda, mboga mboga za majani kama matembele, mchicha n.k )
3) Anywe maji mengi sana na apate mda wa kufanya mazoezi hata ya kutembea + apate muda wa kupumzika (kulala).
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.