Mnyalu-DSM
Member
- Oct 2, 2011
- 90
- 16
Jumapili iliyopita nilijisikia kizunguzungu na kichwa kuwa kizito.Nikaenda hospitali wakanipima pressure wakaona 123/75.Wakapima damu na kuona sina maleria bali nina Typhoip.Nikapewa dawa za kunywa kwa siku kumi na bado naendela nazo na leo ni siku ya 4.Lakini bado najisikia kizunguzungu na joto kali mara moja moja na hali nilitegemea nipate ahueni.Sasa sijui kuna tatizo jingine au la.Na je kweli kizunguzungu ni dalili ya Typhoid?.Tafadhali naomba ushauri?