Naomba ushauri: Technolojia ya ujenzi wa gharama nafuu Tanzania

Kimla

JF-Expert Member
Jun 8, 2008
3,335
5,568
Ndugu wapendwa, Je ni kweli kuna mfumo wa kutumia udongo wa mfinyanzi kwa kuchanganya na cement kidogo ukapata tofari zitakazo saidia kujenga nyumba kwa gharama nafuu? Ukitembelea web site Brick and Block Machine Manufacturers Hydraform wanasema interlocking bricks zinapunguza gharama za ujenzi kwa 50%, je kunaukweli? nipeni taarifa zaidi wadungu
 
kaka ushauri wangu , angalia kwa makini interblocking zilikuja na zikaanza kuvuma sasa zimepotea watu wanajengea ukuta tu . Usikubali kufanya majaribio subiri technology hiyo itumike kwanza then uone ila bora tumia tofali za kawaida zenye ratio bora
 
kaka ushauri wangu , angalia kwa makini interblocking zilikuja na zikaanza kuvuma sasa zimepotea watu wanajengea ukuta tu . Usikubali kufanya majaribio subiri technology hiyo itumike kwanza then uone ila bora tumia tofali za kawaida zenye ratio bora

Asante kwa taarifa, je kwanini waliacha kuzitumia kujengea?
 
Asante kwa taarifa, je kwanini waliacha kuzitumia kujengea?

Unajua sula la mabadiliko sio kitu kidogo katika maisha ya watu. Tabia za binadamu ni kufanya mambo ambayo baba na babu zake walikuwa wakifanya awali. hata katika research nyingi miaka ya 1940- 1960 katika nyanja ya habari yanathibitisha hayo. TWO STEP FLOw inasema kuwa ili kuwafikia wananchi wa mwisho lazima kuwe na mtu kati (opinion leader) - ambaye huwa anajaribu na wale wa mwisho wanasubiri kuona matokeo ndo na wao waanze kutenda hilo jambo. Hii mara zote inatokea kwenye kilimo na shughuli kama hizo za ujenzi. interlocking blocks zimeshindwa kuwa na opinion leaders wazuri. Kila mtu anaogopa kujaribu na mwishowe tunabakia kule kule. Bwana interlockin bricks zinapunguza gharama na zinadumu kwa muda mrefu sana. Kumbuka gharama inayopungua ni katika kuta tu, ukiingia finishg mzazi kimbembe kama kawa maana hakuna interlocking iron sheets, tiles elctrical installations na kadhalika. hapo kaka akili lazima ikukae sawa.
 
ukweli ni kwamba inapunguza gharama wala si uongo kwa vile;
  1. unapanga tofari kwa ajili ya kuta na kutumia muda mfupi zaidi ktk kuzijenga.
  2. Huhitaji finishingi kama plaster kwa nje kwani huwa imekwishajipamba yenyewe
  3. unatumia cement kidogo sana na katika mfuko mmoja wapata tofari mia.
Kuna baadhi ya watu wanashindwa kuifahamu kwa vile haijaenea sana na hawa taasisi ya utafiti mwenge NBRA wamekuwa hawana fungu la kupeleka demonstration ya nyumba hizi japo kuna baadhi ya watu wamejenga nyumba zao kwa matofari haya. Nyumba zinapendeza sana facade zake na ni imara usipime. Elimu ya kuzitengeneza ni rahisi. Pia kuna nyumba zaidi ya 40 za teknolojia hii zinajengwa Chamazi. Pia kuna office ya youth imejengwa manispaa ya Temeke kwa kutumia tofari hizo. okoa fedha yako kwa kutumia teknolojia rahisi na imara.
 
achana na ujenzi kwanza njoo piga klilimo kwanza faida ujengee ujenzi wa tanzania auna adabu ndugu utaona mamilion yako unajua unaingia ndani unaishia kutzama pango kama uko bagamoyo
 
Asanteni wadau, Je watu au kampuni gani dar wanahusika na ujenzi wa aina hii hapa Dar?
 
Waungwana hapa kwetu watu wanamatumaini kibao kuwa Dr. Slaa atachaguliwa kuwa Rais.ila wasiwasi nikwa hawa wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi maana raia wamesimamisha ujenzi wakisubiri bei ya cement ishuke ambapo sasa mfuko mmoja wa cement ni sh.20000 na Dr.alituahidi kuwa tutanunua kwa sh.5000.nilijaribu kuongea na baadhi ya wafanya biashara wakamuomba Dr. awafikirie kwamba atawasaidiaje maana mzigo hautoki na wanananchi wakisubiri mh aapishwe na kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi ili waendelee na ujenzi.
wakati wananchi wakiwa wamesimamisha ujenzi kwa muda kusubiri tumaini Jipya
wafanyabiashara wanauliza Dr.waukweli atawasaidia vipi kwani wanastock kubwa na wengine contena ziko njiani.
 
solution will come on due date.................inamaana hata watu wameacha kupeleka watoto wao shule wakisubiri elimu ya bure?...................u're a gud lier
 
Waungwana hapa kwetu watu wanamatumaini kibao kuwa Dr. Slaa atachaguliwa kuwa Rais.ila wasiwasi nikwa hawa wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi maana raia wamesimamisha ujenzi wakisubiri bei ya cement ishuke ambapo sasa mfuko mmoja wa cement ni sh.20000 na Dr.alituahidi kuwa tutanunua kwa sh.5000.nilijaribu kuongea na baadhi ya wafanya biashara wakamuomba Dr. awafikirie kwamba atawasaidiaje maana mzigo hautoki na wanananchi wakisubiri mh aapishwe na kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi ili waendelee na ujenzi.
wakati wananchi wakiwa wamesimamisha ujenzi kwa muda kusubiri tumaini Jipya
wafanyabiashara wanauliza Dr.waukweli atawasaidia vipi kwani wanastock kubwa na wengine contena ziko njiani.
kila kitu huenda kwa mipango!!
 
mimi mwenyewe nimesitisha kuifuata katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania!
 
Yes waambie wawe na SUBIRA
na wale wanafanuzi wanaosubiri mkopo wanaweza ku-postpone masomo yao ili waje wasome bwerere,,just few days to go
teh teh,,, thats our great SLY
 
Lets just be realistic kidogo.
Bei ya cement itakua 5,000. kutoka kiwandani.
kwahiyo m2 wa songwe, Wazo hill na tanga atapata Cement kwa Bei tofauti na m2 wa Tabora.
Sitaki kuja kusikia bughudha kwa rais wangu Slaa hapo Baadae. Kama Cement itakua ni Elfu tano hiyo itakua ni bei ya kiwandani na inaweza kuwa ni Vat Exclusive. sawa?
 
Waungwana hapa kwetu watu wanamatumaini kibao kuwa Dr. Slaa atachaguliwa kuwa Rais.ila wasiwasi nikwa hawa wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi maana raia wamesimamisha ujenzi wakisubiri bei ya cement ishuke ambapo sasa mfuko mmoja wa cement ni sh.20000 na Dr.alituahidi kuwa tutanunua kwa sh.5000.nilijaribu kuongea na baadhi ya wafanya biashara wakamuomba Dr. awafikirie kwamba atawasaidiaje maana mzigo hautoki na wanananchi wakisubiri mh aapishwe na kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi ili waendelee na ujenzi.
wakati wananchi wakiwa wamesimamisha ujenzi kwa muda kusubiri tumaini Jipya
wafanyabiashara wanauliza Dr.waukweli atawasaidia vipi kwani wanastock kubwa na wengine contena ziko njiani.

Jana (October 5, 2010) nilimwuliza mjenzi ninayetaka anijengee msingi wa nyumba akasema kule Kijichi mfuko mmoja wa cement ni 12,500/-.

Kitu cha msingi hapa ni kubadili mfumo wa utawala ili viongozi wetu wawe wawajibikaji. Mfumo ukibadilika ni wazi kwamba maisha ya Watanzania yatakuwa ya ahueni. Kwa sasa ni kama hakuna anayemjali mtu - kila mtu kivyake! Binafsi napenda kuwepo mabadiliko katika uongozi wa nchi ili wanasiasa wetu wajifunze kuwa wakizembea hawataweza hata kumaliza muhula wa pili wa uongozi wao.

Kwa bahati mbaya sana Watanzania walio wengi ni wale wanaoona matatizo yakiwapata wao tu na yakipungua wanasahau. Lakini kama tungekuwa tunaguswa na matatizo yanayotupata, tungependa kwa dhati walau tuone mabadiliko ili kupeleka ujumbe mwafaka kwa wanasiasa wetu. Hii ndiyo inayonisukuma nitake mabadiko Tanzania. Siridhishwi na kasi ya maendeleo na jinsi mambo yanavyoenda. Tunataka utendaji na uawajibikaji wa hali ya juu serikalini na hatimaye tutaendelea.

Uongozi wa sasa umwshindwa kushughulikia masuala ya msingi ya Watanzania na ndio maana umaskini, ujinga na magonjwa ya kila aina vinaendelea kututesa. Tulipoahidiwa maisha bora kwa kila Mtanzania ifikapo 2010 kila mmoja wetu alitegemea maisha yangebadilika kwa kiwango kikubwa. Lakini umaskini bado ni uleule na hakuna juhudi za madhubuti za kuwawezesha Watanzania waondokane na umaskini, ujinga na magonjwa. Tujaribu kiongozi tofauti - mwenye kasi ya maendeleo na uwajibikaji kati ya wagombea wetu wote!
 
Kama cement inatoka all the way toka pakistan na inauzwa kwa 9000 tshs kwa mfuko tutashindwaje kuuza yetu 5000.
Main drive ya gharama ya cement ni energy chimba mkaa pale liganga lisha ivi viwanda na tumia uranium ya namtumbo kuzalisha umeme cheap.
Hatiame bati na cement vyote vitakuwa 5000.
Ni utashi tuu unaotakiwa apo
 
ACHA WACHAGUE WAKITAKACHO KWA UPOFU WA MBONI ZAO. IKO SIKU YATAKAPOTUFIKA WATATAMBUA KUWA KILE WALICHODHANI NDICHO, SICHO. HAPO NDIPO PATAKAPOKUWA NA KILIO KATIKA NCHI YOTE YA 'WADANGANYIKA'.

Natamani wakati huu ufike upesi. WENYE AKILI NA WATAMBUE!!!
 
kabla ya kuanza kwa mfumo mpya wa kutotoza kodi kwenye vifaa vya ujenzi ni lazima kuwe na kipindi cha mpito,ili kuratibu madhara makubwa kwa wafanyabiashara wenye bidhaa kwenye maghala yao.
 
Back
Top Bottom