Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Kesi ipo mahakamani toka mwezi wa 10 mwaka jana na inaendelea mwezi wa pili,
Sasa hivi nimeshamwacha na yupo mwenyewe pale
Duuh afadhali sana...ulimpenda sana masikini


But sio kosa lako huo ni upendo kama upendo mwingine wowote, tatizo mpendwaji sasa
 
Yani mwishoni lazima mwanamke ndio awe mshika mpini
Sijawahi kuona mwanaume anafurukuta mwishoni
Sababu mwanamke anakuwa na watoto upande wake always na huwa wanasubiri wazee wazeeke warudishe mapigo
Wanaume wahuni mwisho wao unakuwaga mbaya wanajisahaulisha tu hapa....
Mwanaume mwenye akili kubwa lazima mwisho ndiyo atakua mshindi, tena hapo mapenzi aweke kando,na afanye maamuzi ya kiume ,si Nyumba ndogo wala kubwa wote watamuogopa! Wanaume slahaa yetu kubwa kwa Wanawake ni msimamo tu!!
 
OMBI WAKUU NA USHAURI

hii nyumba niifanye nini, ni nyumba kubwa,
Ipo kwenye kiwanja cha eka moja,

Eneo ni ni zuri sana, sasa hivi nyumba ni nyingi, lakini ya kwangu kila mtu anaitamani,

Ila bado haijaisha,

Madilirisha nilishaweka ya aluminium bado matatu tu ya dining room
Kama nimekuelewa vizuri.... hii nyumba umeijenga kwenye viwanja ambavyo hati yake ina jina la mchepuko wako...

Kama ni hivyo, hiyo nyumba mbona siyo yako?
 
Kama nimekuelewa vizuri.... hii nyumba umeijenga kwenye viwanja ambavyo hati yake ina jina la mchepuko wako...

Kama ni hivyo, hiyo nyumba mbona siyo yako?
Hapana, mwanzo kama ulipapitia, wakati anaenda kulipa pesa ya ya manunuzi alienda yeye na kuandika majina ya watoto,

Muuzaji akakataa, lakini akalazimisha mimi niliporudi safari,nikalazimisha majina yabadilishwe, nikachukua zile karatasi nikampelekea muuzaji nikaweka jina la kwangu, na anafahamu , na toka kipindi hicho ninazo mimi mwenyewe,
 
Tayari anajua,
Na kanishauri nianze kwenda kanisani,
Na ameshauri ile nyumba niipige bei
Ila sasa huko mahakamani mchepuko kakataa kuwa hakuwa akijua mimi nina mke,
Ameshapewa maujanja na watu,

Na anasema anajua mali zangu zote pamoja na nyumba ya mke mkubwa zote anataka zichanganywe kwenye kesi na kama kugawana, zigawanyee zote
 
Tayari anajua,
Na kanishauri nianze kwenda kanisani,
Na ameshauri ile nyumba niipige bei
Basi kama kashajua imeisha hiyo. Vipi mahusiano ya watoto wa pande mbili?

Maana ukiuza nyumba watoto wa mchepuko lazima wahamie kwa bimkubwa
 
Hapana, mwanzo kama ulipapitia, wakati anaenda kulipa pesa ya ya manunuzi alienda yeye na kuandika majina ya watoto,

Muuzaji akakataa, lakini akalazimisha mimi niliporudi safari,nikalazimisha majina yabadilishwe, nikachukua zile karatasi nikampelekea muuzaji nikaweka jina la kwangu, na anafahamu , na toka kipindi hicho ninazo mimi mwenyewe,
Basi hapo hana maujanja tena. Ni kukomaa naye mahakamani tu.
 
Ila sasa huko mahakamani mchepuko kakataa kuwa hakuwa akijua mimi nina mke,
Ameshapewa maujanja na watu,

Na anasema anajua mali zangu zote pamoja na nyumba ya mke mkubwa zote anataka zichanganywe kwenye kesi na kama kugawana, zigawanyee zote
Huyo kichaa. Anaweza kukusunbua kwenye hii nyumba mliyojenga mkiwa pamoja. Zile nyingine cheti cha ndoa na bimkubwa kitampigisha chini big time

Nimekusoma kwa makini na nimesoma waliokuwa wanakubeza...

Mimi kiukweli nimejifunza mengi na ahsante kwa kushea hii stori yako.
 
Basi kamankashajua imeisha hiyo. Vipi mahusiano ya watoto wa pande mbili?

Maana ukiuza nyumba watoto wa mchepuko lazima wahamie kwa bimkubwa
Wanatabia kama ya mama yao,
Wamenivunja moyo sana,

Mmoja ndio kaanza chuo mwaka huu,

Wakati mama mama yake hayupo na yeye ansubiria matikeo yake tulikubaliana aende kwetu kabla ya matokeo,

Nilitaka niifunge nyumba, nikamkatia mpaka ticketi, maana mimi nilikuwa nasafari kwa mwezi mmoja,

Matokeo yake wakaongea na mama yake, akagoma kusafiri na tiketi akauza,
Na mimi nilivyosafiri tu, ndio huyu mwanamke akarudi,

Sikuwa na njia nyingine zaidi ya kwenda mahakamani,

Mtoto wa pili matokeo yametoka anasubiri kwenda F 5,

Kuhusu watakaa wapi, Ngoja nisubiri hukumu ya mahakamani
 
Huyo kichaa. Anaweza kukusunbua kwenye hii nyumba mliyojenga mkiwa pamoja. Zile nyingine cheti cha ndoa na bimkubwa kitampigisha chini big time

Nimekusoma kwa makini na nimesoma waliokuwa wanakubeza...

Mimi kiukweli nimejifunza mengi na ahsante kwa kushea hii stori yako.
Ahsante sana
 
Wanatabia kama ya mama yao,
Wamenivunja moyo sana,

Mmoja ndio kaanza chuo mwaka huu,

Wakati mama mama yake hayupo na yeye ansubiria matikeo yake tulikubaliana aende kwetu kabla ya matokeo,

Nilitaka niifunge nyumba, nikamkatia mpaka ticketi, maana mimi nilikuwa nasafari kwa mwezi mmoja,

Matokeo yake wakaongea na mama yake, akagoma kusafiri na tiketi akauza,
Na mimi nilivyosafiri tu, ndio huyu mwanamke akarudi,

Sikuwa na njia nyingine zaidi ya kwenda mahakamani,

Mtoto wa pili matokeo yametoka anasubiri kwenda F 5,

Kuhusu watakaa wapi, Ngoja nisubiri hukumu ya mahakamani
Kama wana tabia kama ya mama yao ni hatari kuwaweka pamoja na watoto wa ndoa. Maadam washakuwa wakubwa unaweza kuwapangishia vyumba sehemu.... hii ni baada ya sakata la mahakamani

Na huko mahakamani usitulie kimya. Mahakama zetu unazijua.... tembeza mpunga kesi inaisha mapema tu.
 
Ila sasa huko mahakamani mchepuko kakataa kuwa hakuwa akijua mimi nina mke,
Ameshapewa maujanja na watu,

Na anasema anajua mali zangu zote pamoja na nyumba ya mke mkubwa zote anataka zichanganywe kwenye kesi na kama kugawana, zigawanyee zote
Sasa Kama bi mdogo hajui kuhusu Mke,je hizo Mali za Mke yeye kazijuwaje bila ya kumjuwa mmiliki!?
 
Sasa Kama bi mdogo hajui kuhusu Mke,je hizo Mali za Mke yeye kazijuwaje bila ya kumjuwa mmiliki!?
Anasema.
Anajua nyumba ilipo, lakini ni yetu na yeye, yeye bi mkubwa hamtambui,
Na sio nyumba tu hata mashamba na nyumba ya mkoani na yenyewe anasema zijumuiswe
 
Anasema.
Anajua nyumba ilipo, lakini ni yetu na yeye, yeye bi mkubwa hamtambui,
Na sio nyumba tu hata mashamba na nyumba ya mkoani na yenyewe anasema zijumuiswe
Swali la jamaa ni kuwa huu mchepuko ulizijuaje hizo mali?
 
Anasema.
Anajua nyumba ilipo, lakini ni yetu na yeye, yeye bi mkubwa hamtambui,
Na sio nyumba tu hata mashamba na nyumba ya mkoani na yenyewe anasema zijumuiswe
Kama mlifunga ndoa na mke mkubwa hapo hizo Mali ambazo mmechuma na bi mkubwa hazimuhusu Kwan Chet Cha ndoa kitaleleza na ndyo ushahidi



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Kama mlifunga ndoa na mke mkubwa hapo hizo Mali ambazo mmechuma na bi mkubwa hazimuhusu Kwan Chet Cha ndoa kitaleleza na ndyo ushahidi



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Chet cha ndoa kipo,
Hati za nyumba zote ni jina langu,
Nyumba nikiyouza akakimbia na robo ya pesa inaonesha mimi ndio niliuza yeye akiwa kama shahidi,

Kiufupi vielelezo vyote vinanihusu mimi
 
Naendelea tulipoachia pale, alipopata zile pesa,

Tulipo tulia kidogo, nilimuuliza kwa utaratibu sana kuwa ni biashara gani anataka kufanya?

Hakunijibu kitu, alichagua kukaa kimya,

Baadaye nikawaita watoto na kuwasimulia, kilichosababisha tugombane na mama yao,

Na nini wazo lao, je wanakubaliana na mimi au mama yao,sasa sielwe labda ni umri au mama yao tayari alishawapa matumaini ya biashara yake mpya au italipa sana.

Nikawaambia umuhimu wa kuwa na kiwanja kwanza na biashara ifate baadaye kwa kuwa huo ni mwezi December 2016 na fungu la kwanza ndio hilo tunapigana,

Mwezi wa kwanza au wa pili tunapata fungu la pili, na hapa sio kwetu tena, sisi ni wapangaji, muda ukifika mwenye nyumba anahitaji kwake,

Sikuona jibu lolote la kueleweka.

Baaday kabisa tena nikamuuliza mmama aniambie ni biashara gani anataka kufanya,

Akanijibu anahitaji biashara ya kupeleka nguo mikoani,
Mimi nikamjibu hiyo biashara mimi sitaiafiki,
Na sababu ninazo.

NATUMA HII KWANZA ISIJE IKAPOTEE NA YENYEWE HALAFU NAENDELEA
Watoto wako wa kuzaa wanakuambia urudi kwenu usimpige mama yao?? Duh! Hawakupendi nini? Yaani wanakushikia mpaka mawe?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom