Upigaji Punyeto: Zijue hasara/ madhara pamoja na njia sahihi za kuacha tabia hii

mjizu123

JF-Expert Member
Mar 19, 2016
349
368
1593413313540.png
Punyeto/kujichua ni nini?

Kufanya au kupiga punyeto, ni tendo la kutomasa sehemu zako mwenyewe za siri ili kujisisimua kimapenzi.

Kwa hivyo katika kupiga punyeto hamna hofu ya kuambukizwa magonjwa yanayosambazwa kupitia ngono, kwani haimshirikishi mtu mwengine.

Punyeto ni toshelezo kamili la kimapenzi kama utatumia njia mbali mbali za kujitomosa na kujipa papasa ya kujistarehesha.

Hakuna mtu anayezaliwa akijua jinsi mwili wake unavyoitikia msisimko wa kimapenzi. Inakubidi kujifunza kwa majaribio salama.

Na, kwa vile kila mtu yuko tofauti, njia nyengine ya kujua jinsi unavyoweza kumstarehesha mpenzi wako, ni kujifunza kutoka kwako mwenyewe.

Shughulika zaidi na sehemu ambazo zinasisimka kwa urahisi.

Unaweza kufikia kilele cha starehe yako kwa kuitomasa tomasa mboo au kisimi, lakini kutakupa hamu kubwa na ashiki, na kufikia kutoshelezwa vya kutosha, kama utapapasa pia sehemu nyenginezo za mwili wako.

Kwa nini punyeto huonekana kuwa makosa?
Msimamo wa dini nyingi na watu wengi ni kuwa punyeto ni dhambi, mwiko, jambo lililokatazwa, jambo lisilokubalika kabisa.

Lakini wanasanyansi wanasema ni jambo salama kiafya na dhana zilizopo kulihusu, ni imani za kibinafsi na chaguo la mtu.

Wanaume wengi na wanawake hupiga punyeto maishani mwao, kwa sababu huwafanya wakajisikia vizuri na huondoa dhiki za mihemko ya kimapenzi bila kujiingiza katika ngono na mtu mwengine.

Pia hofu ya kuambukizwa magonjwa ya zinaa, ikiwemo virusi vya HIV ni kichocheo tosha kinachopelekea baadhi ya watu kupiga punyeto.

Punyeto (kujitoa manii kwa mkono):
"Punyeto" ni: Dhana inayowakilisha tendo la kujitoa/kushusha manii kwa njia isiyo jimai. Kupiga punyeto kwa kutumia kiungo/zana yo yote ile ni tendo la haramu mbele za Mafaqihi walio wengi. Na hiyo ndio kauli ya Mafaqihi wa madhehebu ya Imamu Maalik, Shaafiy na Abu Haniyfah. Lakini uharamu wa punyeto mbele zao uko chini ya uharamu wa zinaa; yaani zinaa ni haramu zaidi kuliko punyeto ingawa vyote ni haramu. Kwa muono wao huu, lau mtu ataangukia katika mtelezo wa kutenda mojawapo ya haramu mbili hizi; zinaa na punyeto. Basi hapana makindano kwamba aegemee zaidi janibu ya punyeto ili kuilinda nafsi yake dhidi ya uchafu wa zinaa. Atafanya hivyo kwa mazingatio ya msingi wa Fiq-hi usemao: "lenye madhara khafifu baina ya yenye madhara mawili" na "lenye shari kidogo baina ya yenye shari mawili".

Ama madhehebu ya Imamu Ahmad na maimamu wengineo-Allah awarehemu-ni kuhalalisha punyeto kwa kuizingatia kuwa ni nyenzo inayoweza kumsaidia muhusika kujikinga na zinaa. Na wala hapa hatukusudii na wala hatuna nafasi ya kutaja mkururo wa dalili za kauli mbili hizi; haramishi ya kundi kubwa na ile halalishi ya kundi dogo. Bali tunalazimika na kutosheka na kuashiria kwamba waliosimamia kauli ya uhalali. Hawakusema hivyo ila ni kwa sababu wameona tendo hili linampa kinga ya kiasi fulani mwanadamu dhidi ya kutenda uchafu na uoza wa zinaa.

Hili ndilo walilolizingatia na kulijengea kauli yao hii ya uhalali, lakini hapo hapo hawalioni tendo hili kuwa ni halali iwapo litageuzwa kuwa ndio ada/desturi na mazoea ya mtu. Akawa analifanya zoezi hili kwa kuendelea kiasi cha kuifanya punyeto kuwa maradhi ya nafsi/siha. Kwa sababu hakuna hata mwanachuoni mmoja anayehalalisha madhara hata kama hicho chenye kudhuru kilikuwa halali katika asili yake.

Mathalan tendo la kula, asili yake ni halali na wakati mwingine huwa ni wajibu kwa kiwango cha dharura/ulazima wa kuhifadhi uhai. Lakini tendo hili hili linaweza likawa haramu pale mtu atakapokula zaidi ya uweza/shibe yake na akasababisha kuidhuru nafsi yake. Kwa msingi wa maelezo haya basi, hapana makindano baina ya maulamaa wetu-Allah awarehemu-katika suala zima la kuharamisha punyeto. Kwa sababu tendo hili linaidhuru kano/mishipa ya nguvu ya muendekeza tendo hilo na kulifanya kuwa ndio mchezo wake.

Kama linavyoudhuru mfumo mzima wa viungo vyake vya uzazi (reproductive system) na afya yake kwa ujumla. Kwa hivyo basi, si Imamu Ahmad wala imamu mwingine anayehalalisha kile kinachosababisha madhara kwa hali yo yote. Kwa mapenzi mema kabisa, tunawasihi na kuwanasihi vijana wetu wa kiume na wale wa kike kutoendekeza zoezi hili la kujitoa manii kwa njia isiyo ya jimai. Tena waache kabisa hata kufikiria kulitenda, kwa sababu tendo hilo ni hatari kwa afya zao.

Mwanachuoni mkubwa; Sheikh Muhammad Al-Haamid-Allah amrehemu-katika kitabu chake {RUDUUDUN ‘ALAL-ABAATWIYL}, ametaja maneno kima kuhusiana na maudhui hii, tunamnukuu: "Hakika tene (kichwa cha dhakari) ina hisia kali sana na hapo ndipo patokapo hisia (za raha na ladha) wakati wa tendo la jimai kwenda kwenye kifuko cha manii (spermatic vesicle). Na kusababisha kijibinye ili kitoke humo kiasi fulani cha manii na kuchanganyika na kitu kinachoitwa "prostate gland". Na hapo katika mchanganyo huo ndipo huundika mmiminiko maji huu ambao kutoka kwake huzipoza na kuzituliza shahawa/ashiki/matamanio.

Sasa basi mtu atakapodumu na zoezi la kuichezea dhakari yake, ngozi ya tene huwa ngumu na kusababisha kudhoofika kwa nguvu-hisia zake. Na kuyafanya manii kutoka bila ya kuchanganyika na ute wa "prostate" ambao una athari na mchango mkubwa katika kutuliza kiamshi-shahawa. Kwa hivyo basi manii yanapokuwa hayakuchanganyika na ute huo, kupoa kwa shahawa huwa ni kwa muda mfupi tu, kisha huamka tena kwa nguvu kubwa.

Kwa ajili hii humlazimisha mpiga punyeto kupiga tema mara ya pili, tatu.... na kama hivi. Mpaka mwishowe humwaga damu (badala ya manii), kwa sababu ya kumaliza kabisa kile kiitwacho "spermatic cord/funiculus" na kuudhoofisha kwake mfumo-uzazi kutokana na wingi wa kupiga punyeto. Kinachotokea kutokana na udhaifu wa hisia wa tene kwa sababu ya wingi wa kupiga punyeto: Ni kwamba mwenye kuzoea kupiga punyeto, hutokezea akashindwa kufanya jimai kwa namna anayoweza kufanya mtu asiyefanya mchezo huo. Hii ni kwa sababu tene iliyodhoofika kutokana na wingi wa kupiga punyeto haiathiriki (na tendo la jimai) kwa kiwango kihitajiwacho kutokana na msuguano ndani ya uke. Kwa hivyo basi hawezi kushusha manii ila kwa kujichua na mkono.

Ndani ya tendo hilo kuna madhara kwa nafsi yake na mkewe ambaye ana haki ya kutoshelezwa nae (ili asifikirie/kufanya machafu) kwa jimai halali". Mwisho wa kumnukuu sheikh-Allah amrehemu.

Kwa kuungia maneno kima haya ya sheikh tunaongezea: Kwamba manii ni kimiminika muhimu mno cha mwili na mfumo mzima wa uzazi. Chini ya maana hii Muingereza Dr. Mary Stoubis anasema katika kitabu chake {MARRIED LOVE}: "Kwa yakini mchanganuo wa kikemia wa kimiminika hiki manii, umedhihirisha kwamba pamoja na vitu vingine unahodhi kiwango kikubwa cha "phosphoric acid" na "calcic acid". Na zote mbili hizi ni maada kima zenye taathira adhimu katika ujenzi wetu wa kimwili (kama wanadamu).

Hili likisihi (kuwa sahihi), basi kwa hakika kosa kubwa analolifanya mwanadamu ni kudhania kuwa maada manii ni kitu ambacho kunasihi kujitakasa nacho baina ya kipindi kifupi na kingine. Na kuimwaga hovyo bila ya malengo na kuona haja ya kuihifadhi".

Ni mazuri yaliyoje maneno ya mshairi huyu anayesema na vijana:

{Yahifadhi manii yako kiasi uwezavyo kwani hayo *** Ni maji ya uhai yamwagwayo katika matumbo ya uzazi}.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na wanasansi wa masuala ya ngono wa nchini Marekani akiwemo Dr.
Michael Reece, (PhD, MPH) umebainisha kwamba iwapo utakuwa unapenda kujichua hautaona kama unapata ladha yoyote ya tendo la ndoa na mwenzi wako, lakini sio kweli kama ladha ya mwenzi wako imebadilika au kupotea, la hasha, ila kujichua kumeshabadili akili yako na mbaya zaidi umeshakuwa mtumwa wa kitendo hiki

Unaweza kupata magonjwa ya akili kama vile sonona. Na kujikuta unaanza kuwachukia watu wa jinsia ya tofauti na wewe, kwa sababu tayari akili yake umeshaathirika kisaikolojia anajiona kuwa haja yake ya kimapenzi anaweza akaitimiza yeye mwenyewe pasipo ushirikiano na mtu mwingine

Lakini pia, kujichua kunachangia kupoteza uwezo wa kushiriki tendo la ndoa kikamilifu. Kwa mwanaume kunaweza kumsababishia uume kulegea au kuwahi kufika kileleni, na kwa mwanamke kujichua kunampotezea ile hali ya kuhimili tendo la ndoa (sexual drive).

Pia kama utakuwa mpenzi wa kujichua unakuwa kwenye hatari kubwa ya kupoteza nywele na kupoteza kumbukumbu.

Source EATV

===

Hisia hizi huanza kujitokeza pale mtu anapofikia wakati wa kubarehe. Hapa ndiyo wakati mgumu na mbaya kwa kijana hasa kwa asiyejitambua na asiye na usimamizi wa karibu wa wazazi au walezi.

Ni wakati huu ndipo mbegu za kiume (manii) huanza kuzalishwa katika mwili wa kijana wa kiume na kupelekea kuanza kuona hitaji la kuwa na mchumba au hata mke.

Kutokana na maisha na tamaduni zetu wa afrika zilivyo hapo ndipo kijana huona hana namna zaidi ya kujichua pale anapokuwa hana mtu wa kujamiiana naye ili kupunguza hamu zake. Kitendo hiki kimeathiri sehemu kubwa ya jamii.

Kupiga punyeto au kujichua ni kitendo ambacho huleta matatizo makubwa ya muda mrefu ambayo muathirika huchelewa sana kuyatambua.

Tuangalie sasa madhara 20 yafuatayo ambayo ni matokeo ya kujichua kwa mwanaume:

1. Punyeto hukufanya uwe dhaifu, inapoteza protini na kalsiamu ndani ya mwili wako.

2. Huleta matatizo kwenye neva nyurolojia ndani ya mwili na kupelekea matatizo ya macho kutokuona vizuri

3. Ni moja ya kisababishi kikuu cha uhanithi (uume kushindwa kusimama)

4. Ni rahisi kuwa mtumwa wa kujichua (teja) unaweza kujaribu mara 1 tu na tayari ukawa teja wa jambo hilo kila mara

6. Husababisha mfadhaiko (stress) kwenye akili na kwenye roho yako pia

7. Huleta matatizo ya kisaikolojia, hukusababishia majonzi na huzuni na kukufanya kujilaumu nafsi mara baada ya kumaliza kujichua

8. Punyeto haifanyiki kirahisi, unahitaji akili yako iwaze au itazame picha mbaya au chafu au kumfikiria kimapenzi mtu asiyekuwepo hapo ulipo. Hili ni jambo baya zaidi kwa afya kwani picha hizo hazikuondoki haraka kichwani mwako tofauti na ukishiriki tendo la ndoa na binadamu mwenzio moja kwa moja.

9. Punyeto inakupelekea kufanya makutano haramu kwakuwa hiyo hamu yako ya kutaka kujichua kila mara itakupelekea kuanza kutafuta vijarida au picha za ngono jambo ambalo ni baya zaidi kwa afya yako ya mwili na roho

10. Punyeto inapelekea tatizo lingine kubwa zaidi nalo ni kuwahi kufika kileleni utakaposhiriki tendo la ndoa na mwenza wako, hii itakuletea shida kwenye mahusiano yako wewe mwenyewe na hata kwa mwenza wako.

11. Punyeto inapunguza uwingi wa mbegu (reduces your sperm count) kama matokeo yake mwanaume hataweza kumpa mwanamke ujauzito. Hili la kuwa na mbegu chache ndilo chanzo kikuu cha ugumba kwa wanaume na ni matokeo ya kupiga punyeto mara kwa mara.

12. Kimaadili kabisa punyeto au kujichua ni jambo baya, unamuwaza fulani na kujikuta ukishiriki tendo la ndoa peke yako. Hii inapunguza thamani yako na nidhamu kwa wengine. Unaweza kuwa mzuri kwenye maeneo mengine mengi lakini utaishia kuwa na matatizo kama hutaiacha tabia hii haraka.

13. Punyeto inapoteza muda wako na kukufanya mtu usiye na faida

14. Raha ya kujichua haibaki akilini kwa kipindi kirefu kama vile ukishiriki tendo la ndoa kwa na mtu halisi

15. Punyeto husababisha ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu, ni vigumu kuwa na akili ya utulivu na kukumbuka vitu kama tayari umeshakuwa teja wa punyeto.

16. Kujichua siyo suluhisho la mwisho la hitaji lako, yaani hutaona kuridhika katika kitendo hicho, kadri unavyofanya ndivyo unavyoendelea kuhitaji zaidi na zaidi mpaka mwisho unakuwa hanithi kabisa bila kujitambua

17. Punyeto haina faida yoyote kwenye maisha yako ya kimapenzi, huihitaji kwa ajili ya chochote

18. Punyeto inaongeza aibu, inapunguza uwezo wa kujiamini. Wengi waliozoea kujichua hata kutongoza kwao huwa ni kazi kubwa mno kiasi wengine huona bora kuendelea kujichua kuliko kutongoza mwanamke.

19. Utapoteza hamu ya kushiriki tendo la ndoa kirahisi zaidi kama utaendelea kujichua

_. Punyeto huchochea mapenzi ya jinsia moja hasa mashuleni, vyuoni na kwenye mahoteli na mwishowe hupelekea kusambaa kwa magonjwa mengi ya zinaa.

20. Punyeto inamaliza nguvu za kiume, kama unapenda kujichua basi sahau kuwa na nguvu za kiume. Upungufu wa nguvu za kiume ni janga la kitaifa miaka ya sasa lakini chanzo kikuu ni vijana wengi wa kiume kuanza kujichua tangu wakiwa mashuleni.

Je ufanye nini ili kuacha punyeto au usishiriki mchezo huu mchafu?

Kama muda na umri haukuruhusu kuwa na mke au mchumba, basi fanya yafuatayo:

•Kama bado unasoma kuwa bize na masomo na ujiepushe na makundi hatarishi.

•Jishughulishe na mazoezi ya viungo kila siku. Hii itauchosha mwili wako na hivyo hutapata muda tena wa kujichosha zaidi kwa kujichua kwani tayari utakuwa na uwezo wa kupata usingizi mtulivu sababu ya mazoezi.

•Epuka vyakula vyenye mafuta mengi

•Usipende kukaa muda mrefu peke yako au kujitengaa na watu pia usikae muda mrefu kitandani hasa hasubuhi wakati wa kuamka

•Usikae muda mrefu maeneo kama ya bafuni au chooni

•Usipende kujishikashika na mkono wako sehemu zako za siri wakati wowote

•Futa picha zozote chafu iwe kwenye simu au computer yako na usitembelee blog au tovuti yoyote yenye picha hizo, kama upo kwenye magroup ya namna hiyo kwenye mitandao ya kijamii basi jiondowe haraka iwezekanavyo.

•Kama tayari umeshaoa basi ni dhambi kubwa sana kuendelea kupiga punyeto, utaishiwa nguvu na unaweza kukosa kumpa ujauzito mkeo siku za usoni.

Na kwa upande wa wanawake:

Kujichua a.k.a kujichezea a.k.a “a little help from ur hand” (kupiga puri au punyeto sounds manly) sio kwa wanaume tu bali hata wanawake tunafanya hivyo ila wengi wetu huwa hatuko “comfortable” kulizungumzia au kukili kuwa tukizidiwa huwa tunajisaidia…….wakati mwingine mtu unashindwa kabisa kupata usingizi mpaka upige moja-mbili ndio usingizi unakuja au asubuhi unajisikia mzito kuamka kitandani mapaka upige moja ndio nguvu zinakuja…hasa kama umezoea dozi za maana lakini sasa mpenzi hayupo karibu.

Katika upande wa Mwanamke

Kujichua au kujichezea ni njia pekee ya kujifunza kufika kileleni, kuujua na kuuelewa mwili wako na kujua utamu wa ngono ukoje(incase hujui utamu huo ukoje). Kwa kujichua utajua jinsi kutoa na kupokea raha ya kufanya mapenzi na mpenzi wako, utasaidia ngozi yako kuwa nzuri na laini (mambo ya Urembo hayo) na vilevile utajua jinsi ya kuzuia (kuchelewa kwa makusudi kufikia mshindo) au kumsubiri mwenzio ili mfike pamoja, hakuna raha ya kufanya mapenzi kama kufika kwa wakati mmoja.

Faida za kujichua/chezea:-
1)Kuujua mwili wako na kujiamini zaidi linapokuja swala la kungonoka(fanya mapenzi)
2)Kuongezeka kwa hamu ya kufanyamapenzi kwa vile utakuwa unajua utamu wake.
3)Kujua “vipele vyako viliko”.
4)Kutokuusaulisha mwili wako ikiwa uko nje ya uhusiano au umeamua kuwa single kwa muda.
5)Kuepuka mimba na maambukizo ya virusi vya UKIMWI na magonjwa mengine.

*Kama kuna faida nyingine unaijua basi si mbaya kama utachangia hapa.

Madhara ya kujichua/chezea:-
1)Uchovu wakati wote / Fatigue. Feeling tired all the time.
2)Kujichua kwa kutumia sanamu a.k.a Dildos ni kusamburuka kwa nyama za nyeti zako(inategemea na aina ya sanamu), kupoteza hisia za uume halisi kutokana na kuzoea “dubwana” hizo, kifo kutokana na “shock” ikiwa unatumia ya umeme, vilevile saratani ikiwa unatumia vilainishio ili kurahisisha “dubwana a.k.a toy a.k.a Dildo” kuingia.


3)Maumivu ya nyonga / Lower back pain.
4)Kusinyaa kwa Nywele / Nywele kunyonyoka / Thinning hair / Hair Loss
5)Maumivu ya kiuno

USHAURI ZAIDI NAMNA YA KUACHA SOMA:
- Mjadala: Je, ni jinsi gani mtu anaweza kuacha punyeto?


1579851066668.png



===
BAADHI YA WADAU WALIOPATA MADHARA YA PUNYETO
Miaka karibu ishirini iliyopita kipindi nilipobalehe siku moja nikiwa bafuni naoga nilisikia sauti ya dada mmoja wa jirani akiongea na wenzake na kucheka ktk hali isiyo ya kawaida nikamtamani na kuanza kuvuta hisia nikifanya naye mapenzi na kwa mara ya kwanza nikaanza kupinga punyeto, ukawa ni mwanzo wa safari ambayo imenifikisha sehemu nisiyotamani kabisa kuwepo.

Kama kuna wengine hili kwao halina madhara basi kwa upande wangu limekuwa tatizo kubwa sababu tangia hapo ukawa ni mchezo wa almost kila siku, nikimwona mdada yuko nusu uchi hata kwenye tv mm tamaa inawaka najimaliza kwa punyeto. Wadada wa bongo movie wengi sana nimeshawapigia punyeto yaani nikiona tu mapaja au chupi tu kwangu ni tatizo moyo unaenda speed lazima nipige punyeto.

Miaka ya nyuma kidogo kulikuwa na vijarida vinaandika story za picha za mapenzi nilikuwa navinunua usiku navitumia kuvuta hisia huku napiga punyeto. Kwa sasa almost kila siku niko xvideos napakua video za porn za kila aina nikiwa naangalia namaliza hapo hapo, najisikia hatia nafuta video zote ila kesho yake nazipakua nyingine mchezo unaendelea, nimeshatuma sana elfu tano tano kwa wadada ili wanitumie picha zao na video zao za uchi au sometime kufanya sex video call.

Nimetamani sana kuacha, nimeomba na kuombewa lkn bado, nimejiwekea resolutions mara nyingi ya kuwa sasa naacha, nitajitahidi kujizuia kwa muda kama wiki mbili au tatu baada ya hapo narudi tena kwa nguvu mpya yaani ni kama nakuwa nakusanya nguvu tu ya kurudia upya na hasa kwa kuwa mara nyingi mawazo ya kuacha porn&punyeto huja baada ya kufanya punyeto kwa siku mfululizo so nahisi mwili huwa umechoka/kukaukiwa hivyo akili inakuwa imekaa sawa, ila zikishaongezeka tu mwili unaanza kusukuma kutafuta porn video na kupiga punyeto.

Kuna kipindi smartphone iliharibika nikawa natumia kitochi hapo ndio nilikaa kama miezi 3 kwa sababu sikuwa na means ya kuangalia porn, ila siku nilipopata tu smartphone nilikaa kama wiki mchezo ukaanza upya. Nikiwasha data huwa najisemea leo siingii xvideos so nitaperuzi vitu vingine ila mawazo yatanisukuma tu kwenda xvideos tatizo nikiaanza kuzipakua hadi kuja kumaliza na mwishowe kupiga punyeto mwili na akili vimechoka.

Binafsi hiki kifungo na hizi tabia zimenichosha sana na yako mambo ktk maisha yangu nayaona sasa naamini yako linked na hizi tabia, mimi ni mvivu hasa wa kutenda mambo, nimekuwa mwoga mwoga hivi, muda naotumia kuangalia na kupakua porn kama ningekuwa nautumia ktk mambo ya maana naamini ningekuwa ningepiga hatua zaidi ya niliyopo sasa.

Jana nimeangalia porn mpaka nikakosa kitu cha kuangalia maana vyote nimeshaviangalia mpaka intrest imeisha na hili nalo likanipa hofu sana hadi nikajiuliza kama nimejisikia hivi, nini kitafuata? Ninaamini hii ni ishara nyingine kuwa inabidi nitoke kwenye hili shimo nililoingia.

Nimeishi maisha yenye sura mbili kwa miaka yote hii na sasa natamani niishi maisha ya aina moja yaliyo safi, kuna watu wananiheshimu sana na kuniona mtu wa maana na muhimu sana hata kunishirikisha mambo yao mazito mazito ili niwashauri, huwa najisemea tu kuwa hawajui kuwa mm ni mchafu zaidi yao, ni dhaifu zaidi yao na si msafi kama wanionavyo nje na hili linanisumbua sana natamani niishi maisha safi nje na ndani.

Wale mliowahi kupambana mkashinda ktk changamoto kama hizi naomba ushauri, maana nimedhamiria kabisa kuwa siku ya jana tarehe 05/09/2019 ndio iwe siku ya mwisho ya kupiga punyeto na kujihusisha na pornography na ninaamini "one day at a time" nitafanikiwa.

Natanguliza shukrani kwa ushauri na support nitakayopata hapa.
Hili Jambo Ni tatizo kwa wengi Sana, wengi tumebaki kuwa mateja ktk hili!!

Mi nilianza nikiwa advance Tena sikufundishwa na mtu yeyote nimejaribu Sana kuacha laki nimeshindwa Ila Sasa Ninaimani kubwa Sana yakuacha ndio, naamini nitaacha na mishaanza mipango na naona mwendo mzuri kabisa!!
Nimefanya njia nyingi Sana na za hatari kuacha lakini nilishindwa!!

1) nilipoona nafanya Sana afu kuacha siwezi basi nikachukua wembe nikajichanja uume wote ili vidonda vizuie nisishike uume na kufanya punyeto, vilipo pona tu nikajikuta nimerudi Tena!!

2) Kufunga uume wote na plasta funga nikaacha kichwa tu kwaajili ya kukojoa lakini njia hii pia haikuzaa matunda nayo!!

Katika yote nashukuru Mungu na nazidi kuomba anitoe ktk hili shimo, Maana miaka 7 si mchezo!! Wakati mwingine naona bila punyeto labda ningekuwa nishapata UKIMWI au ningekuwa jela kwa kubaka!


MAONI NA USHAURI ULIOTOLEWA NA WADAU KUHUSU TATIZO HILI
Porn na mastrbation ni samaki na maji.Kuvitenganisha ni ngumu.Hatua ya kwanza kwa mantik hii ni kuacha kuangalia porn.

Hii ni kazi ngumu lakin weka nia ya kuacha kwanza kuangalia porn videos kabisaaaaaa.wkat huu unaweza ukajikuta unaendelea kupiga nyeto lakin rate haitakua kama ile trust me.Na hii ni kwasababu mind yako tayar ina hazina ya kutosha ya kumbukumbu za porn vids ulizoangalia before ambazo huondoka taratibu sana.Hivyo kuacha kuangalia porn unakua kama umeacha ku update mind yako kuhusu habar hiz.Ndio maana kuacha kuangalia porn ni kitu cha kwanza muhimu sana ingawa ni kazi sana.

Hii inahusisha pia kuacha kusoma soma sana makala za mapenz.Jukwaa kama MMU inabid ukikimbie kwa muda maana ukikutana na nyuz za akina Zero IQ hazitakuacha salama katika kioind cha ku recover.

Nb:bado hamu ya kupiga nyeto itakuepo na unaweza ukawa unashtua ila rate huwa inashuka kias maana kwa memory ile ile utajikuta unakosa mshawasha wa kujilipua tofaut na ukiendelea kuangalia mpya.

Badil mfumo wa namna unavyowatazama wanawake.Waone katika mtazamo hakis kabisaa kama awal kuwa hawa ni mama zetu dada zet mabint zet na wake/gfrnds zetu wala sio vifaa vya ngono.Sitawisha hii fikra maana moja ya upumbavu wa porn& nyeto huabdil kabisa namna mwnaume anavyomchukulia mwanamke kifikra ndio maana kila ukiona picha au mtu nusu uchi kinacho kujia akilin ni kutoshelezwa haja zako za tamaa ya kingono.

Hii process ni ndefu sana.BAada ya hapo utajikuta unabadilika kabisaa.Unaweza usiwe mpnz wa kusoma vitabu ila jaribu ku feed taarifa mbadala kwenye akil yako.Mijadala ya milengo tofaut inaweza kukusaidia .

Nachokuambia hiki sio stori bali ni kitu kimenisaidia mwenyewe binafsi.Nilikua napiga punyeto hata baada ya kuoa.Ni mbaya sanaa.Inakufanya kwel kuhis guilty hasa kwakua nje watu wanakuona mtu wa tofauti na vile ulivyo kiuhalisia.
Ikafika hatua nafanya huo mchezo kwa mwezi mara 1 na kwasasa aisee nimeshasahau kwakwel.
INAWEZEKANA

Mkuu Kuacha Punyeto Kuna Hitaji Commitment Ya Hali Ya Juu Ya Kuhakikishia Unaamua Kuacha.

Kwa Takwimu Cha Chamani (CHAPUTA) Zinasema Ukiweza Kuacha Ndani Ya Miezi Miwili Basi Umeweza Ila Nakwambia Takribani More Than 4 Ukiweza Kustaimili Basi Tunakupa Saini Kuwa Si Member Wetu Tena Wa CHAPUTA.

1. Mkuu Tuanze Na Mazoezi Huku Ukiwa Serious
Hakikisha Tunaanza Kwa Kukimbia Kama Kuna Uwanja Karibu Basi Anza Hapo Kwa Round Hata 7 Maana Tayari Ni Muanga Wa Punyeto. Ile Hali Ya Uchovu Umalizapo Kupiga Selfie(Punyeto) Ndio Itakayo Onekana Wakati Unaanza Mazoezi Hakikisha Unalazimisha Akili Yako Kushindana Mawazo Na Yale Ya Kupiga Nyeto Wakati Unakimbia.
Sema Moyoni Haya Maneno Pale Unapoanza Kuchoka Ukiwa Mazoezini "Sitaki Tena Punyeto, Nakuwa Mzembe Kwa Sababu Ya Nyeto" Huku Ukiongeza Round Za Kukimbia.

Hakikisha Tunajitahidi Ku-maintain Speed Kama Ulianza Slow Basi Hakikisha Hahishuki Zaidi Ya Hapo.

Nakwambia Ukweli Boss Wangu Hakuna Kitu Kinachosha Kama Punyeto Halafu Uwe Mfanya Mazoezi. Maana Kama Ni Mpiga Nyeto Ukienda Tizi/Mazoezi Unaona Kabisa Pumzi Inawahi Kukata.

Boss Tumia Mazoezi Kama Silaha Yako Namba Moja Kuwa Uwe Na Consistency Ya Kuhakikishia Kama Leo Ulikimbia Round 7 Kesho Pambana Ukimbie 9 Hii Kichwani Mwako Useme Inatawekana Kama Usipopiga Nyeto.

Hakikisha Unakuwa Hukosi Mazoezini Usiupe Mwili Nafasi Ya Kurelax Sana Na Kujikuta Umeangukia Mikononi Mwa Nyeto.

Progress Utayoona Mwanzo Kabisa Hata Week Hahitoisha Ni Mkunyenge/Machine Kuanza Kuwa Ngumu Maana Madhara Mengine Ya Nyeto Ni Kulegea Kwa Mkunyenge.

Hapa Ni Kwa Uchache Nimetumia Kukimbia Kama Pia Wewe Ni Mpenzi Wa Mpira Rudi Kwa Pitch Uanze Kazi Ila Usisahau Kukimbia Ndio Silaha Yetu Namba 1 Tukiwa Tunaanza Na Hii Tiba.
Pole ndugu yangu, tatizo hayo mambo huleta roho chafu zinakuvaa na kutake control of ur life ndo mana huwa ngumu kuacha.

Cha kukushauri tu kama wewe ni Mkristo hebu omba tena omba hasa, anza na toba. Uzinzi wa aina yoyote ile unamuaibisha Mungu kumbuka mwili ni hekalu la Bwana, sasa dhambi hii huwa inampa shetani kibali cha kuku control kupitia huo mlango ulimuachia wazi, Mpaka utakapoufunga huo mlango ndipo shetani ataacha kukutesa.

Na Mungu ni wa Rehema ndo mana hata anakupa Neema ya kutambua kwamba unakosea na unataka kutubu ili uache kabisa huo uovu. Kumbuka tukitubu kwa moyo wa kumaanisha yeye hutusafisha kabisa na kututenga mbali na dhambi ''kama mashariki ilivyo mbali na magharibi hivyo ndivyo ataweka dhambi zetu mbali nasi''.

Mwambie Mungu nakuja mbele zako naomba toba na msamaha kwa kukuabisha pale nilipozini kinyume na mpango wako, Mungu nakiri kuwa nimekutenda dhambi naomba Unisamehe, unioshe kabisa uovu wangu, unitakase dhambi zangu, mana nimejua mimi makosa yangu na dhambi yangu i mbele yangu daima, unifutie hatia zangu zote,

Bwana neno lako likae ndani yangu nisije kukutenda dhambi, Yesu wewe hukuja kuwaita wenye haki bali wenye dhambi kama mimi, katika jina la Yesu navunja connection zote za kiroho kati yangu na masturbation, navunja mamlaka niliyompa shetani pale nilipotoa mwili wangu kwake, Navunja soul tie zooote na nguvu zote za giza zilizoingia kwangu kupitia masturbation, naweka msalaba wa Yesu kati yangu na kitendo hiki na naagiza nafsi, roho na mwili kusahau kabisa, najiwekea ukuta wa damu ya Yesu. Asante Yesu kwa kunisamehe, kunikomboa na kunisafisha. Amen

Hii iwe sala yako usiku na mchana, na ukumbuke kufanya mazoezi au kujiweka busy ili usipate nafasi ya kuyawaza mambo yatakayofanya mwili upate udhaifu wa kuwaza ngono.
Mimi ninachokushauri ni hiki, kwanza tambua ya kuwa wewe ni wa mhimu sana mbele za Mungu.

Punyeto au utazamaji wa porn ni chukizo kubwa sana mbele za Mungu, kwani unapotazama picha za ngono au kupiga punyeto unakuwa unampa utukufu shetani,na mtu yeyote anayekuwa akitenda dhambi huwa anakuwa mtumwa wa dhambi hiyo, hivyo hawezi kuwa huru hata siku moja.

Picha zote za ngono, majarida au habari za ngono hizo hazipo kwa ajiri ya kukupa burudani, huo ni mtego uliowekwa na mawakala wa shetani ili kuwanasa watu wa Mungu wapate kuanguka. Wacheza sinema za ngono hao huwa wanalaana tangu awali ,kwani wapo tayari kufanya lolote na wakati wowote,ndo mana waweza kuwaona wengine wanafanya ngono,mtu mmoja kwa watu watano au zaidi. Na wengine utawakuta wanafanya ngono na mbwa au na mnyama yeyote, hiyo ni laana.

Kutazama au kupiga punyeto, kunakaribisha pepo wachafu kuweza kumuingia mtu,ndo mana unakuwa na kiu ya kutazama, huwezi kumaliza siku mbili au tatu bila kutazama, mwanamke au mwanaume akinaswa na hizo picha yupo tayari kulala na dada yake au kaka yake. pindi unapotazama picha hizo chafu usizani ya kuwa upo peke ako, hapo unakuwa na pepo wachafu wakikutazama na kushuhudia udhaifu wako.kuna watu unawaona kwenye hizo video clips ,wanawake wazuri na warembo hasa, sio wote ni binadamu, kuna wengine ni pepo wachafu wakiwa wamevaa maumbo ya kibinadamu, wapo tayari kumuangamiza yeyote anae kuja mbele yao.

Na tambua ya kuwa sisi sote tu viumbe vya Mungu na hivyo twatakiwa kuwa safi wakati wote, kiroho na kimwili. Sasa pindi utazamapo picha za ngono au kupiga punyeto roho wa Mungu huwa anaondoka na kukuacha peke yako mana hawezi kuishi katika mwili utendao maovu, kama tunavyojua ya kuwa mwili ni hekalu la roho mtakatifu aliye msaada wetu wakati waote,

Sasa tunapokuwa mbali na roho mtakatifu uwepo wetu umekuwa bure, maana yeye ndio msaada wetu kwa kila jambo,atuepusha kwa ajari, atupatia neema na baraka na ndio mwombezi wetu .

Ushauri wangu, jikane nafsi yako tangu sasa na uamue kuacha mara moja huo mchezo mchafu, jiulize tangu umekuwa ukifanya hayo umefaidika na nini sasa???

Kama sio kupoteza mda, kujitia hatia, kusononesha roho yako, kupata hasara ya bando zako kwenda bure kutokana na kupakua vitu viovu na kuvifuta tena na tena, kuwa chukizo mbele za Mungu.

Kweli Mungu huchukizwa na dhambi, sasa unapenda wewe akuchukie na kukuona wa ovyo ulie kubali kushindwa na mambo ya kidunia?.

Au hujui ya kuwa imeandikwa, "msiifate dunia wala vilivyomo ndani yake,mana dunia imejaa tamaa ya macho, tamaa ya mwili na kiburi cha uzima"

Tena imeandikwa ikimbieni zinaa, tena tumeambiwa tuvitunze viungo vyetu na tuvifanye viwe safi,na tuifanye miili yetu kuwa safi na tayari kwa kumtolea bwana.


Mungu huchukizwa na dhambi. muombe Mungu wa rehema akurehemu,akusamehe na uaachane na uovu huo usio na faida, kwa Mungu yote yawezekana maana yeye ndo muweza wa yote. Ubarikiwe katika kristu bwana
Mkuu kuangalia porn na kupiga puli ni vitu visivyoachika kwa hiyo njia uliyoitoa ndugu.

Njia pekee ya kuacha hivyi vitu viwili, in fact siyo kuacha, ngoja niweke sentensi vizuri. Njia pekee ya kupumzika kujihusisha na hivyo vitu ni kwa kukaa na watu muda wote.

Kwa basi ni kukaa na watu?

Kwanza ujue, kupiga puli kunaitaji faragha ya hali ya juu, yaani mtu anapopiga puli akikutwa ni sawa na "kafumaniwa" sasa ili mtu aache puli ni akae na watu muda mwingi.

Njia ya pili ni kutokuwa na stress, amini wapiga puli wengi almost wote huwa wanapiga puli wakiwa na stress. Hakuna mpiga puli anayepiga puli akiwa na furaha. (Member watatoa ushuhuda)

Mtu pekee anayeweza kumfanya mpiga puli akaacha kupiga puli ni mpenzi mkorofi na aliye romantic, hapa nieleweke nikisema mkorofi ninamaanisha mtata kweli ila ndani ya utata wake awe romantic pia. Huyu anao uwezo wa kumfanya mpiga puli akaacha kupiga puli kwa 90%

Tip: wapiga puli ndio watu wenye nafasi kubwa ya kufanikiwa mambo yao. Mf. masomo, kazi na biashara, sababu huwa hawana vikwazo vya wapenzi, ila ni wapuuza mambo. Hali inayofanya watu wahisi wapiga puli ni wasahaulifu, si kweli, wapiga puli wana memory active sana. Mpiga puli anauwezo wa kukumbuka mpangilio wa sauti alizowahi kuzisikia hata miaka 5 iliyopita kwa usahihi.
JINSI PUNYETO INAVYOWAMALIZA VIJANA.

Habari ninasaidia vijana kuondokana na tatizo la nguvu za kiume leo nimeamua kushare na nyinyi “jinsi punyeto inavyomaliza vijana”. Unapopiga punyeto unakuwa unaiminyamishipa ya uume ambayo ndio inafanya uume usimame matokeo yake unaifanya mishipa hiyo ilegee na kutokuwa na uwezo wa kupitisha damuya kutosha.
Mishipa ya uume iliyolegee kuttokana na upigaji wa punyeto uleta madhara yafuatayo:
1) Huondoa uwezo wa mishipa ya uume kutanuka. (unapopata wazo la kufanya mapenzi mishipa ya uume ina relax, mishipa ikitanuka husababisha mishipa ya ateri kutanuka na kuruhusu damu kuingia ndani ya mishipa ya uume na hatimaye kuufanya uume usimame na kuwa mgumu.

2) Mishipa ya uume ikishindwa kutanuka husababisha mishipa ya ateri kuziba

3) Mishipa ya ateri ikiziba, damu inashindwa kutiririka kwenye mishipa ya uume n ahata ikitokea damu imeingia ndani ya mishipa ya uume basi huingia kiasi kidogo sana tena kwa presha ndogo sana hivyo basi hata kama uume ukisimama utasimama ukiwa legelege

4) Mishipa ya uume ikishindwa kutanuka basi haitakuwa na uwezo wa kupush na kuiziba mishipa ya neva ambayo ndio hunyonya damu kutoka kwenye mishipa ya uume uliosimama. Matokeo yake damu kidogo iliyoingia kwenye mishipa ya uume hunyonywa na kutolewa nje ya mishipa ya uume ndani ya sekunde chache na kufanya uume usinyae ndani ya muda mfupi.

5) Uume kurudi ndani na kusinyaa na kuwa uume kama wa mtoto.

6) Punyeto pia usababisha kutoa manii kwa haraka. Hujenge ukungu kwenye kiwanda cha uzalishaji manii ambayo hudhoofisha manii na kusababisha joto la haraka pindi tu upatapo hisia ya mapenzi ndio unajikuta unakojoa haraka.
 
Hilo tatizo ni baya sana na kwa wale kama ushawahi kukutana kimapenz na mwanamke aliyezoea kujichua. Wengi huchelewa kufika kileleni na wengine hupenda kushika papuchi zao wakati wakiwa wanaingiziwa. Hii mbaya sana.msishabikie huu ujinga waelemisheni wadada waolewe na wadumu kwene ndoa zao.
 
Madhara ya kujichua kwa wanawake na wanaume

Punyeto ni nn

Punyeto ni kitendo cha kufanya au kupiga punyeto, ni tendo la kutomasa sehemu zako mwenyewe za siri ili kujisisimua kimapenzi.

Haya ni baadhi ya madhara awezayopata mwanamke anayejichua au kufanya punyeto;

1. Inaharibu kizazi

2. Inakufanya kua mvivu mara kwa mara

3. Unakuwa unakosa hamu ya tendo

4. Maumivu ukeni yasiyo na sababu

5. Uke kuwa mlegevu yaani mtepeto

6. Hupelekea uke kutoa maji maji mara kwa mara au maji yale ambayo utoka kabla ya tendo kuto kuwepo ivyo itakufanya kupata michubuko na maumivu makali wakati wa tendo.

7. Uwezi kuja kujua raha ya tendo ukizoea punyeto sana wewe dada.

8. Punyeto inafanya uke wa mwanamke kukosa ladha kabisa hiyo itapelea kukimbiwa na mmeo au mwenzako kutafuta kamchepuko kenye uke mtamu.

9. Na ukizoea punyeto itakufanya kuwa mtu wa hasira hasira kila mara

10. Punyeto ni hatari kwa afya yako pia ukiizoea sana itapekekea kufanya mapenzi ya jinsia moja.

Hay ni baadhi ya madhara ya kupiga punyeto kwa wanaume

1. Punyeto hukufanya uwe dhaifu, inapoteza protini na kalsiamu ndani ya mwili wako.

2. Huleta matatizo kwenye neva nyurolojia ndani ya mwili.

3. Ni moja ya kisababishi kikuu cha uhanithi (uume kushindwa kusimama)

4. Ni rahisi kuwa mtumwa wa kujichua (teja) unaweza kujaribu mara 1 tu na tayari ukawa teja wa jambo hilo kila mara

5. Huleta uchomvu sugu na kwa haraka zaidi, mara nyingi utahitaji kulala usingizi hata nyakati za mchana

6. Husababisha mfadhaiko (stress) kwenye akili na kwenye roho yako pia

7. Huleta matatizo ya kisaikolojia, hukusababishia majonzi na huzuni na kukufanya kujilaumu nafsi mara baada ya kumaliza kujichua

8. Punyeto haifanyiki kirahisi, unahitaji akili yako iwaze au itazame picha mbaya au chafu au kumfikiria kimapenzi mtu asiyekuwepo hapo ulipo. Hili ni jambo baya zaidi kwa afya kwani picha hizo hazikuondoki haraka kichwani mwako tofauti na ukishiriki tendo la ndoa na binadamu mwenzio moja kwa moja.

9. Punyeto inakupelekea kufanya makutano haramu kwakuwa hiyo hamu yako ya kutaka kujichua kila mara itakupelekea kuanza kutafuta vijarida au picha za ngono jambo ambalo ni baya zaidi kwa afya yako ya mwili na roho

10. Punyeto inapelekea tatizo lingine kubwa zaidi nalo ni kuwahi kufika kileleni utakaposhiriki tendo la ndoa na mwenza wako, hii itakuletea shida kwenye mahusiano yako wewe mwenyewe na hata kwa mwenza wako.

11. Punyeto inapunguza uwingi wa mbegu (reduces your sperm count) kama matokeo yake mwanaume hataweza kumpa mwanamke ujauzito. Hili la kuwa na mbegu chache ndilo chanzo kikuu cha ugumba kwa wanaume na ni matokeo ya kupiga punyeto mara kwa mara.

12. Kimaadili kabisa punyeto au kujichua ni jambo baya, unamuwaza fulani na kujikuta ukishiriki tendo la ndoa peke yako. Hii inapunguza thamani yako na nidhamu kwa wengine. Unaweza kuwa mzuri kwenye maeneo mengine mengi lakini utaishia kuwa na matatizo kama hutaiacha tabia hii haraka.

Je ufanye nini ili kuacha punyeto au usishiriki mchezo huu mchafu?

Kama muda na umri haukuruhusu kuwa na mke au mchumba, basi fanya yafuatayo:

•Kama bado unasoma kuwa bize na masomo na ujiepushe na makundi hatarishi.

•Jishughulishe na mazoezi ya viungo kila siku. Hii itauchosha mwili wako na hivyo hutapata muda tena wa kujichosha zaidi kwa kujichua kwani tayari utakuwa na uwezo wa kupata usingizi mtulivu sababu ya mazoezi

•Usikae peke yako muda mrefu bila kuwa bize na shughuli yoyote. Kichwa kitupu ni nyumba ya maasi mengi.

•Epuka vyakula vyenye mafuta mengi

•Tumia muda ambao huna kazi kwa kulala na hivyo utakuwa unaipumzisha pia akili yako

•Usikae muda mrefu maeneo kama ya bafuni au chooni

•Usipende kujishikashika na mkono wako sehemu zako za siri wakati wowote.

•Futa picha zozote chafu iwe kwenye simu au computer yako na usitembelee blog au tovuti yoyote yenye picha hizo, kama upo kwenye magroup ya namna hiyo kwenye mitandao ya kijamii basi jiondowe haraka iwezekanavyo.
"KUISHI BILA CHAPUTA INAWEZEKANA"
 
Uongo hakuna uthibitisho wa kisayansi unaonesha punyeto ni chanzo cha ukosefu wa Nguvu za Kiume.

Vipi kuhusu mtu mwenye Kisukari, pressure na Magonjwa mengine wanaokosa Nguvu za kiume wakati hawajiusisha na Punyeto.
 
Uongo hakuna uthibitisho wa kisayansi unaonesha punyeto ni chanzo cha ukosefu wa Nguvu za Kiume.

Vipi kuhusu mtu mwenye Kisukari, pressure na Magonjwa mengine wanaokosa Nguvu za kiume wakati hawajiusisha na Punyeto.
Testesterone(korodani) hupungukiwa ujazo wa homoni za kiume, so huwezi kuwa na uwezo wa kuzalisha mwanamke(kumpatia ujauzito) maana shahawa zako zitakosa nguvu.

Pili mara kwa mara misuli husinyaa ndiyomaana hutakiwi kupiga nyeto.

Tatu mshirikishe sana mungu katika kuacha kwako punyeto maana wakati mwingine huwa kuna mapepo yaliyoingizwa humo kupitia picha mbali mbali na mitandao ya vedeo za "X".

Pia mungu hakukuumbia hizo homoni zimwagwe nnje ya uke, subiri mungu akupatie chaguo lako sahihi(mke mwema) uwe unamwaga hizo homoni zako katika uke wake maana mungu huchukizwa sana na hicho kitendo.
 
Wadau, msaada mwenye picha za mange Kimambi alizopost akiwa kwenye jacuzzi
 
Back
Top Bottom