MJADALA: Je, Pikipiki gani ni bora kwa matumizi ya nyumbani au biashara kwa Tanzania?

sawe4u

JF-Expert Member
Sep 11, 2016
973
570
1591778932413.png

BAADHI YA MASWALI YALIYOULIZWA NA WADAU WA JF
Twende pamoja kwa waliotumia na wanaotumia pikipiki tuu.

Kati ya hizi pikipiki unaipenda sana ipi na kwanini(based katika matumizi binafsi)?
1. Boxer
2. SANLG
3. Feckon
4. TVS King
5. Hero
6. King Lion
7. Houjo
---

Habari za wakati huu wana JF, kama title inavyojieleza hapo juu;

A] Nataka kununua pikipiki kwa ajili ya matumizi yangu binafsi na baadae kidogo kwa biashara. Hivyo naomba ushauri wa aina ya pikipiki itakayofaa kwa kuzingatia vigezo vifuatavyo;

1)mwonekano mzuri (mvuto)

2) injini kubwa (uwezo wa kuhimili milima -speed)

3)upatikanaji wa spear zake na bei nafuu

4)ubanifu wa mafuta (economical fuel consumption)

5)bei yake nafuu sana

KATI YA PIKIPIKI HIZI ( BOXER 150, TVS, HAOJUE /HONDA ACE, HERO, TANHERO)

NITOE USHAMBA TAFADHALI KTK HAYA
*Pia kati ya Boxer old model na New model ipo bora, na kwann?

*Boxer BM 150 na 125 ipi nzur/kubwa (injini).

*Je kuna boxer yenye gia 5 na ipi?

* Hivi plate namba A inamaanisha chombo ni cha kitambo xana na uwezo/ubora wake ni mdogo ukilinganisha na namba B, C, na D,?
Mfano nikinunua chombo (gari au pikipiki kwa mtu Je ishu ya kubadilisha umiliki inakuaje?

#NATANGULIZA SHUKRANI ZANGU KWAKO MWANA JF... %
---
Wakuu habari za majukumu ya utafutaji.

Nina budget ya 2.5M nataka kununua pikipiki au bodaboda kwa ajili ya matumizi yangu binafsi ya kwenda kwenye mishe zangu. Niko pembeni kidogo na Dar, sasa barabara za huku nilipo hazina rami. Zina vidimbwi vya maji, mabonde in short ni rough road.

Pikipiki ipi inaweza kuhimili changamoto za barabara mbaya japo haipakii mizigo ni kwa ajili yangu tu. Hivi pikipiki kuwa na gear nyingi mfano zipo za gear 4 na zingine 5 kunafanya pikipiki kuwa na speed zaidi?
---
Wakuu wasalaam,

Naomba kujua ni pikipiki gani imara na yenye speed ambayo itafaa kwa matumizi binafsi ya kutembelea (misele) na bodaboda kiasi.

Barabara ni lami na off-roads. Budget ni 2.5M.

Kuna mtu kanishauri nichukue Haojue DH 125. Naomba mwenye ufahamu zaidi juu ya hii pikipiki anijuze kama itanifaa.

Shukrani.
View attachment 1470937Haojue DH 125

1591780821089.png


BAADHI YA MAONI YALIYOTOLEWA NA WADAU WA JF
Pikipiki yoyote inafaa na ni imara endapo tu utazingatia yafuatayo:
  • nunua toleo halisi /original
  • Ijue tabia yake (soma user manual)
  • Jali vilainishi na mafuta: epuka petrol za mtaani, imrchanganywa, ina uchafu, imepigwa jua na kubadilika rangi iko km dizeli, tembeakoki ya mafuta iwe kwenye full sio reserve.
  • Jali muda wa kubadili oil (huu ndio uhai wa injini). usichanganye changanye aina za oil. zoeza aina moja hasa nzito. usiogope bei maana wahangaza walisema CHEAP IS EXPENSIVE
  • Ikiwashwa km injini imepoa sana (asubuhi) iache silencer angalau dk 5 ipandishe oil na injini apate joto (usipandishe kwa kuvuta moto/accelerator)
  • Wajati wa kuendesha; badili gia kwa mpangilio ukisaidiwa na mwongozo wa rpm/mzunguko wa injini. sio km vijana wanabandika na kubandua. ndani ya dk 1 ameshafuta gia zote pikipiki ikiwa na muungurumo km helikopta
  • Usibebe mizigo kupindukia, utaua shock ups/springs na kupunguza ufanisi wa injini/puling capacity maana itahitaji nguvu za ziada kuhimili load na itajilipa kwenye tenki, kukata vyuma hasa chassis na carrier, kuchubua foronya na rangi mwisho waswahili ukiwemo wewe wataanza kuponda chombo sio imara
  • Jaza upepo wa magurudumu itakiwavyo angalau 55 au 60 kuepuka kurika taili, kupunguza spidi (barabara korofi haitakiwi presha kubwa, chombo itakutetemesha na kukukata mgongo. weka 40-50, fundi tyres wana ushauri murua)
  • Usimpatie dereva usiyemwamini uendeshaji wake. hapa usidanganywe na leseni yake
  • Inapobidi, isinyeshewe
  • Epuka kuosha injini ikiwa ya moto. rejea physics kutanuka na kusinyaa. utakegeza nati muhimu za injini na michubuko au kudhoofisha ile steel ya vyuma.
  • Weka vipuri halisi hata kwa gharama kiasi.
  • Tumia fundi mmoja na mwaminifu kwa matengenezo makubwa hasa injini na umeme. awe anakumbuka kipi akifanya previous services.
  • Zingatia sheria za usalama barabarani, rough overtaking na khchomekea kumewaacha wengi kwenye nyumba za milele wakisubiri ufufuo na maelfu hawana miguu, mikono, ngozi za uso n.k

-MWISHO SI KWA UMUHIMU: TOA SADAKA, FANYA MAOMBI UWE KARIBU NA MUUMBA MAANA HAYA NI MAJENEZA YANAYOTEMBEA
---
Ni wazi kua pikipiki imara ni za mjapan.
Sasa basi kwa bajeti yako nakushauri usifanye makosa tafuta pikipiki ya mjapan na unaweza kuongezea pesa kidogo ila usiogope maana unanunua mkataba haswa.

Tafuta pikipiki hizi,kwa matumizi yako binafsi na vimizigo vya hapa na pale:
1.Honda CGL 125
2.Honda CG 125
3.Honda Ace cb 125(ila hizi nadhani ni za south africa kama sikosei)
Machaguo ya kwanza ndo mjapan mwenyewe na zote zina starter.

Nina Honda CG 125 huu mwaka wa 8 sasa kitu piru bado,nna jamaa yangu alinunua mapikipiki yenu ya kihindi na mchina kwa miaka mi5 ila ukiziweka pamoja yangu bado inaonekana mpya na tunapiga na kufanya mizunguko inayofanana kwakua mishe tunafanya pamoja.

Narudia tena na tena jikaze kwenye bei pikipiki ni za mjapani
---
TVS Jamani mnajua bei ya vifaa vyake?

Ngoja niwaweke sawa ndugu zangu. Mie simpotezi mtoa Mada. Ila nampa ushauri mzuri sana. Sio lazima anunue bike ya mil 18, au mil 10.. Zipo bike mpk mil 4.. Na ni same type na specs tofaut ni imetumika muda gani na year of prod.


Nunua pikipiki hyo ya mil 2.. Utumie mwaka mmoja uje kuuza laki 9!

Pili.,Utaingia cost zisizo na maana.. Jiandae kununua spocket kila mara.. Chain drive.. Jiandae kubadir front/rear suspension kila mara..

Jiandae kukosa uhuru njiani.. Ipo wazi ukiendesh Boxer au TVS kila mtu anakuona bodaboda tu ndo hapo rafu za maksudi zinatawala.. Ukiwa na kx! Au crf kwanza mwenye crown anakupisha upite..

Pili kiuhalisia.. Hata usumbufu wa wale Tigo haukupati.. Unaingia popote mjini.. Advantage hzo! Kingine cha mwisho hz bike unaweza nunua mil 5 ukaja kuuza mil 7.. Ila tvs unanunua mil 2.5 unakuj kuuza lak 9.

Bike yangu ina mwaka saiv nabadili oil tu.... Basi.. Uliza wamilik wa Boxer au TVS maintanance cost thou ni cheap spare parts ila hazidumu.. Humaliz mwezi unafungua hiki unafunga kile.. Ukija kupga mahesabu umetumia hela nyng..

Faida ya hzo Tvs na boxer unaweza ukawa unapakia abiria njiani kufidia mafuta.. Kujipatia kipato ukiwa free!

Mwisho.. <Cheap is expensive!>

shortcut always is a longcut
---
Boxer, TVS na Mahindra
ni piki piki nzuri sana mfumo wake ni wa timing chain unapungunguza nguvu kubwa ya kuchoma mafuto mengi lakin mzungo wa ijini unakuwa mkubwa kwenye mafuta zipo vizuri ...changamoto.

1. Mafundi wa kuzitengeneza ni wachache..ukiipeleka kwa mafundi wa piki piki za mchina hasa kufungua ijini tegemea kuharibiwa kabisa.

2. Spare zake zipo juu sana tofauti na piki piki za kawaida.

3.zinahitaji oil za gharama za juu na zenye quality kwa usalama wa igini yako !!Vinginevyo utaichakaza mapema kuanzia sha 10,000 oil.

4.spare zake nyingi haziingiliani na piki piki za chini.

5. Hazikubali modification hasa ya spare kama imekosekana agiza usije kumodifire ukafunga ...utapata ajali
---
Pikipiki ni matunzo yako mkuu, Boxer ukiitunza utadumu nayo muda mrefu. Spea zipo ila bei yake ipo juu tofauti na mchina. Mafundi wapo kila sehemu pikipiki hizo zimesambaa sana.

Ukitaka uishi nayo muda mrefu ukifanya service ya kumwaga oil kumbuka kubadili Oil filter na kusafisha air cleaner, exhaust iache hiyohiyo usiweke au kuchezea ili iwe na makelele.
---
Mkuu Umetaja Piki piki Nyingi tuu kama Boxer,Fekon,Sanlg,TVS,nk

Ila Mwisho wa yote Kuna Pikipiki moja inaitwa HOAUJUE...au Kiswahili wanasena "Haujue" Hii Pikipiki ni noma Asikwambie Mtuu,Uliza waendesha Pikipiki watakuambia.

Ni Imara,inapiga Mzigo na Nzito. Ikitulia Barabarani Hakuna na Boxer, TVS,au wala sijui nini atafuata hii. Niliwahi Siku moja Kupakia Mzigo wangu,gunia 2 za Nazi kwenye "Hoaujue" nami nikapanda Boxer, Tumeanza tuu Boxer akatupita akaenda mbali.

Baada ya kama Dk 7 hivi,lilitupita kama tunesimama, nikamwambia Dereva wa Boxer Aisee vipi ongeza mwendo Mkuu,akaniambia hiyo ni "Hoaujoue" taamka "Haujue" ni balaa siwezi fuata pale linapokuwa limechanganya!

Na ni BORA usipime! Yaani Imara!

Inavumilia kila hali!
---
Kwa upande wa Yamaha crux ni pikipiki nzuri sana.
1. Inakula wese vizuri tu lt1 unaenda mpka 55km hadi 60km kutegemea na uendeshaji wako.

2. Ina kamlio flani amazing kama kamluzi hivi, kapo kwenye yamaha nyingi (huwa nakafurahia).

3. Sio yeboyebo kama mchina, zipo chache.

4. Service ni kawaida tu, mie natumiaga total oil 8000/= na 500/= au 1000/= ya fundi kumwaga oil. Service huwa nafanya kila mwezi, pikipiki ni binafsi halafu haina mizunguko zaidi ya mishe zangu na nyumbani tu.

Changamoto nlizokuwa napata ni pamoja na;

1. Upatikanaji wa vifaa (sio kila duka waweza pata spea).

2. Brake zake sio strong kivile sababu ni drum especially ya mbele halafu utaudjust sana hizo break ili zibaki na ile grip unayoitaka.

3. Tairi zake ni nyembamba zinataka lami tu kwa hiyo ukipita sehemu yenye kamchanga kuwa makini sana sana sana sanaaa..... yaani kwa lugha nyingine ukiona mchanga punguzu mwendo mapema sana kabla hujawa maarufu mbele ya umati wa watu kwa mfano anapopita SanlG,Fekon n.k kama kuna mchanga unaopitika vizuri tu, ukiwa na yamaha crux unaweza kukutupa chini.

Vilevile tairi zake ni za tube kwa hiyo ukipiga msumari haina cha kusubiri ndani ya dk moja upepo kushnei, sali sana sehemu ya mafundi iwe karibu.

4. Kana gia 4 tu kwa hiyo kanadai sana gia.

5. Ngoma ni kick to start only.

Mbali na hizo changamoto naikubali sana.
 
Pikipiki, inategemea umeinunua kwa shughuli inayofavor mazingira gani? Kama wewe ni mtu wa shamba na kubeba mizigo, barabara zenye vigongo, urahisi katika bei ya vipuri. Kwa maoni yangu Sanlg, ni nzuri.
umeambiwa matumizi binafsi
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom