Naomba ushauri: Naishi na mtoto wa mke wangu, wangu anaishi kwa bibi yake nashindwa kumchukua

NIMEONA

JF-Expert Member
Aug 4, 2019
3,865
5,683
Ushauri tafadhali!

Umeoa mke mwenye mtoto na unaishi naye huyo mtoto ukihudumia huduma zote!!

Huko nyumbani nawe una mtoto pia yuko kwa bibi yake (mama yako) anaishi na kusoma, mama wa mtoto wako ametangulia mbele ya haki.

Hapo kwa bibi yake anaishi na mtoto wa kaka yako (dada yake) wanaofanana umri, na historia ikiwemo ya kufiwa mama. hawa watoto wamekuwa kama mapacha, hawatenganishiki.

Ukinunua kitu lazima uwanunulie wote, ukitaka akutembelee mtoto wako bila huyo mwingine basi lazima utaonekana mbaguzi na hauko sawa na huyo utakayemuacha atakuwa kwenye msongo wa mawazo sana.

Maisha ya kuishi kwa bibi yana changamoto zake za hapa na pale; huduma hazitoshelezi, kukosa hela ya shule, kukosa vitafunwa, kukosa nguo, kutoshiba, kutokula unachotaka n.k. Umbali kati yako na mtoto huchangia zaidi changamoto hizi.

Uwezo wako hautoshi kuhudumia kwa kiwango sawa pande hizi mbili, frankly, upande wako na mkeo unapata huduma bora zaidi.

Katikati ya changamoto hizi kwa mtoto wako wa kumzaa, mtoto wako wa kambo unayeishi nae anakula hadi anasaza, anaoga anavyotaka, anapata 200 au zaidi ya kutumia shule kila siku, ananyosha kwa umeme wako kila siku, anapendeza, ananawiri kwa huduma.

Kama nilivyoeleza juu, wako ni tofauti kwani unyoshaji hufanyika kwa pasi ya mkaa, ulaji si wa kuamua, kukosa hela na vitafunwa ni jambo la kawaida, kulala na mlo wa ugali usiku ni kawaida n.k.

Unafikiria kumhamisha na kumleta unakoishi, lkn kuna changamoto hizi zinakutatiza;

1. Shule ya msingi iliyopo eneo lako ni mbovu kuliko huko kwa bibi anakoishi - walimu wachache, ufaulu si wa kuridhisha

2. Ukimhamisha huyo basi kuna uwezekano mkubwa ukalazimika kumhamisha na huyo mwenzie anayeishi nae. Nae ni mkiwa na anahitaji msaada; kaka yako hali si nzuri na yuko mbali huko katika kuhangaika na maisha.

3. Bibi (mama yako) nae ni changamoto nyingine kwani hao watoto ndo kampani yake kuu, upweke atakaojisikia ukiwatoa si wa nchi hii.

Kama binadamu, dukuduku fulani linajaa kila siku kifuani kwamba mtoto asiye wangu anafaidi vyangu huku wangu akihangaika, inafikia kipindi mpaka unamuota binti yako kwa mawazo. Hisia za kukosa baraka kwa Mungu kwa hili zinaanza kukujia kichwani maana unaona kama unamuonea huyu mtoto!!

Mawazo yenu wadau katika hili.......
 
Kaka unajua kuna siku huyo mtoto ataangusha glasi na utampiga nusu kumuua au kumchoma vidole kumbe ni unataka kutoa huo uchungu wa kuona anakula vyako bure bure?

Mama zetu hua hawaombi vikubwa. Lakini chochote utachomtumia anaweza figure out namna ya kufanya walio nyumbani waridhike. Kama kweli shule ya kwa bibi ina ufaulu mzuri si umpeleke na huyu uliyenaye nyumbani ili naye afaulu?

Mimi nafikiri una shida ya ubinafsi na mapenzi kwa wakati mmoja. Now kabla havijakuchanganyia drop huyo mdada na mwanae chukua bibi, mwanao na mtoto wa kaka ishi nao.

Au drop huyo binti kisha nenda kaishi kwa bibi kama concern yako ni kufaulu.

Ushauri wangu umezingatia matukio ya wazazi wanaochoma moto watoto wa kambo au hata kuwaabuse sexually.
 
Kama ni mm, naiacha situation iendelee ilivyo. Mtoto wa kambo, kwa kuwa ulimpenda mama yake na ulimuoa ukijua kabisa anaye, mtunze tu. Yote ya Mungu, huenda akakufaa baadaye , huwezijua.

Kuhusu watoto hao wawili, kwa point moja tu kuwa WANAMPA KAMPANI KUMBWA MAMA, nitawaacha huko huko na kutuma ninachoweza kuwasaidia huko huko.
 
Mchukue bibi yao na watoto kaa nao town hakika hata kama kipato chako kitaongezeka hakika hyo damu isiyoyako usitegemee msaada hapo wa baadae
Nakanusha mstari wako wa mwisho. Mapenzi unayomuonesha mtoto wa kambo ndiyo yanayoamua mapenzi yake kwako pia akiwa mkubwa.

Ninao ushahidi wa binti aliyelelewa na mama yake wa kambo huko Sikonge - Tabora. Leo huyo mdads ni mtumishi wa umma na anapeleka sehemu ya mshahara wake kila mwezi nyumbani.
 
Kaka unajua kuna siku huyo mtoto ataangusha glasi na utampiga nusu kumuua au kumchoma vidole kumbe ni unataka kutoa huo uchungu wa kuona anakula vyako bure bure?

Mama zetu hua hawaombi vikubwa. Lakini chochote utachomtumia anaweza figure out namna ya kufanya walio nyumbani waridhike. Kama kweli shule ya kwa bibi ina ufaulu mzuri si umpeleke na huyu uliyenaye nyumbani ili naye afaulu?

Mimi nafikiri una shida ya ubinafsi na mapenzi kwa wakati mmoja. Now kabla havijakuchanganyia drop huyo mdada na mwanae chukua bibi, mwanao na mtoto wa kaka ishi nao.

Au drop huyo binti kisha nenda kaishi kwa bibi kama concern yako ni kufaulu.

Ushauri wangu umezingatia matukio ya wazazi wanaochoma moto watoto wa kambo au hata kuwaabuse sexually.
Siungi mkono wazo la kumdrop mdada (mke), unalenga kuvunja mji sasa na sio lengo la yy kuomba ushauri hapa.

Issue ya kumpeleka mtoto wa kambo kwa bibi (sio bibi yake kivyovyote) mke hawezi kuliafiki.
 
Moja wapo la jambo la kipuuzi kufanywa na mwanaume ni kumjali sana mtoto yeyote asiyekuwa wa kwake kuliko hata jinsi anavyomjali mtoto ambaye ni damu yake.

Na kwa bahati mbaya sana ndicho kitu ambacho wanaume wengi waliooa wanawake ambao tayari wamekwisha zalishwa wanakifanya.

Sent from my M100 using JamiiForums mobile app
 
Siungi mkono wazo la kumdrop mdada (mke), unalenga kuvunja mji sasa na sio lengo la yy kuomba ushauri hapa.

Issue ya kumpeleka mtoto wa kambo kwa bibi (sio bibi yake kivyovyote) mke hawezi kuliafiki.

Yaani kabisa amwambie mke wake eti amtoe mtoto wake hapo nyumbani, kisha jamaa ndio amlete mtoto wake ndio waishi naye hapo nyumbani

Wewe....weweee!!! Nimejaribu ku-imagine huo moto utakao Waka hapo nimeshindwa kupata picha.

Hiyo ni sawa na kuwaambia CCM waunde tume huru ya uchaguzi wataona ni heri tu wasishiriki kabisa uchaguzi..... Hivyo hivyo pia kwa single mother kumtenganisha na mwanae ilihali huyo mwanae ndio sababu kuu iliyomfanya aingie kwenye ndoa, ataona ni heri tu hiyo ndoa ife.

Sent from my M100 using JamiiForums mobile app
 
Siungi mkono wazo la kumdrop mdada (mke), unalenga kuvunja mji sasa na sio lengo la yy kuomba ushauri hapa.

Issue ya kumpeleka mtoto wa kambo kwa bibi (sio bibi yake kivyovyote) mke hawezi kuliafiki.
Ishu ya kwanza nimeshaijibu.

Ya pili. Kukataa au kukubali kutategemea huyu mwanamke ana urafiki gani na bibi
 
Sasa twende sawa.
1. Ni haki yake huyo mtoto wa mkeo kula vizuri na kupata mahitaji yote muhimu.
2. Ni wajibu wako kuhakikisha kwamba mwanao na yule wa kaka yako wanapata mahitaji yote ya msingi ikiwa ni pamoja na milo mitatu kwa siku. Uwe unanunua angalau mahindi gunia 3 na mchele gunia 1, maharage kilo 50, dagaa ndoo 3, mafuta ya kula lita 20, jaza gas, na mkaa walau gunia 1. Kisha unamwachia mamako angalau laki 2 za kubadilisha mboga na matumizi madogo madogo. Watoto wape walau buku 5 kila mmoja kila week.

Ukishindwa hivyo chukua bibi na watoto 2 leta nyumbani muishi wote 6. Bado si familia kubwa kihivyo.
Mwisho uache roho ya ubaguzi na upendeleo. Wote hao watano unawajibu wa kuhakikisha wanaishi kwa furaha na amani kwa kadri iwezekanavyo.
Kila la kheri!
 
Hii mbona simple sana?

Fanya yafuatayo:

Kwanza, hakikisha maisha mnayoishi nyie na mkeo ndiyo wanayoishi mama yako na hao watoto kule kijijini, hata kama isiwe sawa kwa 100% lkn angalau yaendane kwa 100%/90. Hakikisha kama wao wamelala njaa leo, basi kesho wao wale na nyie iwe zamu yenu kulala njaa.

Pili, huyo mwanao wa kambo pia ana baba yake, kama bado anamtambua basi amhudumie kwenye zile huduma za msingi kama ada za shule, nguo n.k. Kama bado anamtambua basi si vibaya akaja akamchukua kwani damu yake na kila mtu abebe mzigo wake. Najua utasema mama yake atakataa lkn kwenye maisha kuna muda lazima ufanye maamuzi magumu for your better future.

Tatu, tambua kwamba maamuzi yoyote utakayoyachukua lazima kuna upande utaumia. Hivyo pima mwenyewe ukifanya uamuzi upi utaleta maumivu madogo kwa upande husika kuliko kutochukua maamuzi leo kisha uje ujute maisha yako yote. Lkn lazima ufanye maamuzi kwani ni bora maumivu madogo ya leo kuliko maumivu for the rest of your life.


Kazi kwako mkuu.

Unforgetable
 
Ishu yako mbn ndogo sana mfano mm chabro nilioa mke wangu mwaka 2001 nilimkuta na mtoto wa miaka 3 mm nikamzalisha watoto 6 jumla tunao watoto 7 tunaishi vzr tuu na mtoto wa mke wangu nimemuingiza Jeshini dogo private saizi ananikumbuka vibaya mno na ananiheshimu sana mana nilikuwa nawalea na kuwa treat wote vzr nilikuwa sina upendeleo linapokuja swala la mtoto kakosea yani natia stick vibaya mno cjali awe wangu au co wangu napiga tu, mtoto wangu wa kwanza saizi yupo form 6 kwaiyo mzee yy alikataa kuingia jeshini anasema anataka asome awe doctor mzee mpende mtoto wako wa kambo atakusaidia badae mm uyu janja ananikubali vibaya mno ananipa tuu ela ya bia.....
 
Back
Top Bottom