Naomba ushauri: Mpangaji wangu msumbufu kulipa kodi nataka nifungie vitu vyake

Usimfanyie hivyo, mpe muda andikishiana nae kwa mjumbe kwamba hadi kufikia let say Disemba mosi ulipe pesa yangu laa nitafunga chumba na nitazuia vitu vyako hadi hapo utakapokuja kulipa pesa yangu.
Ngojea nijaribu kufanya hivyo boss,japo nipo mbali nae,hofu yangu hasije kuhama usiku
 
Busara ni kumpa notes alipe ama aondoke nyumba iwe wazi aje mwingine,ukiwa mwenye nyumba ndani ya miezi3 ukiona mtu hajalipa Basi ni vyema ukamtaka muachane tu maana hata Maisha hubadilika anaweza tafuta nyumba atayoimudu kwa muda huu, iwe ni nje ya mji kabisa ambazo kodi ni nafuu sana au maeneo kama mabibo, Manzese, Tandale ,kigogo,buguruni ama Mbagala anaweza pata chumba na sebule KWA 40000 tu na akajihifadhi na kujipanga upya.

Nenda KWA step pia maana naye ni binadamu na anahaki zake,ukikosea tu anaweza kukubadilikia na kukuhamza maana mtu akishmbuliwa na Tatzo la kodi hupatwa na stress sana,hata me pia
Nikweli,inabidi niendenae taratibu tu, ngojea nimuandikie NOTICE kwamba Hadi muda fulani awe amelipa,ikishindikana ntazuia vitu vyake
 
Dah sema wenye nyumba wanakuwaga wababe sana huwa wanaona wameyapatia maisha. Halafu watoto wao wakina kuwa wakubwa wanapitia madhila Yale Yale waliyopitia wapangaji wao. Kama unaweza msamehe tu nyumba hayiami utapata mpangaji mwingine.
mkuu nimemvumilia Sana, hila yote kwa yote inawezekana, maana Bora tu Banda langu hawezi ondokanalo, ikifeli nitamsamehe tu
 
Weka na mlinzi baada ya kumfukuza maana ukinifanyia mimi hivyo nakuja usiku navunja naiba vitu vyote alaf asubuhi naenda kukopa hiyo laki 6 yako nakuletea alaf nakudai vtu vyangu vyenye thaman ya 1.5M+ hapo ndo utauona moto
 
mzee kuwa makini sanaa....mjumbe ni bure tu mbele ya sheria ...

kuna kisa kama hiki kilitokea
jamaa alikuwa anadaiwa laki 4 na mwenye nyumba ,mwenye nyumba akamchukua mjumbe wakafunga nyumba ,yule mpangaji akasafiri zake wala hakuhaingaika na kitu chchte ,

badae mwenye nyumba akaona nyumba yake ipo tu watu wanakuja kuulizia nyumba lkn ndo hvyo kuna vitu vya jamaa...

akamwita mjumbe wakavunja na kuadika mali walizokuta ndani wakavipakia store ,wakapangisha nyumbaa....

eeeeeh hilo ndo likawa kosa kubwa kwao,

jamaa alivyorudi na kukuta ile hali hakuongea na mtu akanyoosha mahakamani na kufungua kesi ,na katika ile kesi alidai kulikuwa na fedha taslimu million 5 kwenye bahasha ambazo zilikiwa ndani ya nyumba..

mwenyenyumba na mjumbe waliipata kisawasawa ..walilipa million 6 na laki 3 kwa awamu 3 huku mahakama ikaweka amri ya kuvirejesha vitu vyake ndani na apewe muda wa mwezi mmoja (notice) ndo ahame ....

jamaa akabeba hela wala hakurudi kwenye hyo nyumba akasepa na kitita akaishiaa zake


KUWA MAKINI SANAA ..UKIKUTANA NA MTU ANAYEIJUA SHERIAA UTAIPATA VZR
Hiyo ni mahakama gani? mkataba unasemaje?
 
mzee kuwa makini sanaa....mjumbe ni bure tu mbele ya sheria ...

kuna kisa kama hiki kilitokea
jamaa alikuwa anadaiwa laki 4 na mwenye nyumba ,mwenye nyumba akamchukua mjumbe wakafunga nyumba ,yule mpangaji akasafiri zake wala hakuhaingaika na kitu chchte ,

badae mwenye nyumba akaona nyumba yake ipo tu watu wanakuja kuulizia nyumba lkn ndo hvyo kuna vitu vya jamaa...

akamwita mjumbe wakavunja na kuadika mali walizokuta ndani wakavipakia store ,wakapangisha nyumbaa....

eeeeeh hilo ndo likawa kosa kubwa kwao,

jamaa alivyorudi na kukuta ile hali hakuongea na mtu akanyoosha mahakamani na kufungua kesi ,na katika ile kesi alidai kulikuwa na fedha taslimu million 5 kwenye bahasha ambazo zilikiwa ndani ya nyumba..

mwenyenyumba na mjumbe waliipata kisawasawa ..walilipa million 6 na laki 3 kwa awamu 3 huku mahakama ikaweka amri ya kuvirejesha vitu vyake ndani na apewe muda wa mwezi mmoja (notice) ndo ahame ....

jamaa akabeba hela wala hakurudi kwenye hyo nyumba akasepa na kitita akaishiaa zake


KUWA MAKINI SANAA ..UKIKUTANA NA MTU ANAYEIJUA SHERIAA UTAIPATA VZR
Kosa alilofanya huyo nikufunga nyumba bila yakuwepo huyo mpangaji wake,

Kisheria nadhani wajumbe au mabalozi wanatambulika na mahakama katika suala la Ushaidi,
Kwaiyo boss unashauri njia gani ni nzuri labda
 
Weka na mlinzi baada ya kumfukuza maana ukinifanyia mimi hivyo nakuja usiku navunja naiba vitu vyote alaf asubuhi naenda kukopa hiyo laki 6 yako nakuletea alaf nakudai vtu vyangu vyenye thaman ya 1.5M+ hapo ndo utauona moto
ukija kuvunja unatengeneza kesi ya ujambazi Sasa 😎😂
 
Wakuu habari:

Unajua hizi nyumba za kupangisha zina matatizo Sana,mtu umetumia pesa kibao kuwekeza,Bado Tena unakuja kupangisha majitu ambayo hayajielewi.

Ni hivi, Kuna mpangaji wangu now anakaribia miaka miwili kama na nusu kwenye mabanda yangu, Sasa huyu tangu kipindi cha Corona ya kwanza hile mambo yake hayajakaa sawa, nilikuwa namdai milioni na laki mbili, alilipa laki nne Bado laki sita, Sasa saundi zimekuwa nyingi, mara subiri kidogo, mara week ijayo, mara mwisho wa mwezi ,

Sasa nilichofikiria huyu bwana mdogo labda nikuzuia vitu vyake vyote,na kufunga nyumba Hadi hapo atakaponilipa pesa yangu,

Sasa je nikiwa na mjumbe siinatosha kiushaidi kwenda kumtimua hili nifunge nyumba Hadi atakapolipa Deni!!?

Au wazee wenzangu mwashaurije katika hili, maana sitaki kutumia ubabe sheria itanibana
Una mkataba nae wa maandishi? Uliupitisha tra na unalipa Kodi? Kama mna makubaliano ya mdomo Bora uondoe kimyakimya maana anaweza kusema humdai na ukashindwa kuthibitisha.
 
Una mkataba nae wa maandishi? Uliupitisha tra na unalipa Kodi? Kama mna makubaliano ya mdomo Bora uondoe kimyakimya maana anaweza kusema humdai na ukashindwa kuthibitisha.
Yaan mkataba wa nyumba kupangisha upitishe Hadi TRA, nayeye akisema simdai si aonyeshe Ushaidi,


Nna Ushaidi wa kieletronic kuwa namdai na anafahamu
 
Sasa akianza kuhamisha vitu vya thamani mwezi ukifika akuachie masufuria.Hapo ni kumkazia sa hivi haina kusubiri,deni linazidi kuongezeka na uwezo hana.
hapo ndio hofu yangu,mnaandikishiana, usiku anahamisha vitu vya thamani anaacha masufulia tu anahama
 
Kuna jamaa yangu alipanga nyumba akakutana na mpangaji mtata ,miezi 6 ikapita bado anakwepa kulipa,akamwambia ondoka bado anasema ili niondoke lazima unipe notice . Mwenye nyumba alichofanya ni kumwita mjumbe mbele ya jamaa akasema nataka kurepair nyumba yangu aondoke ,mafundi wakaanza kutoa bati,chumba ikawa wazi kwa juu halafu akaacha hapo hapo ,mvua ikija au jua likiwaka watajua wenyewe au akiibiwa atajijua ..mbona aliondoka mwenyewe
Ahahah,Kama ni chumba kimoja kinajitegemea unaweza kufanya hivyo 😂
 
Nikweli,inabidi niendenae taratibu tu, ngojea nimuandikie NOTICE kwamba Hadi muda fulani awe amelipa,ikishindikana ntazuia vitu vya
Ni naona mpe notisi ya miezi mitatu

Deni mwambie ukiona ni haki yangu utanilipa ila ukiona siyo haki yangu basi kaa nayo .

Ili uweke mpangaji mwingine upate pesa.

Ukiendelea kung'ang'ana naye huyo ndugu unajichelewesha .
 
Kama uwezo hana mzee kua muungwana maisha yanabadilika sana ukute anawaza namna ya kumaliza deni lako ingekua uwezo upoo labda hapo ungewaza ufanye nini
kulipana hivo ni changamoto sana,hapo akimaliza deni ina maana miezi inakimbia pia na miezi inayokuja Mambo yale yale deni lingine linaanza
 
Ni naona mpe notisi ya miezi mitatu

Deni mwambie ukiona ni haki yangu utanilipa ila ukiona siyo haki yangu basi kaa nayo .

Ili uweke mpangaji mwingine upate pesa.

Ukiendelea kung'ang'ana naye huyo ndugu unajichelewesha .
umeongea point mkuu,

Ntalifanyia kazi, Baada ya kuandika notice, Kuna haja yakumpa then nikabakia na copy yake
 
Nenda taratibu. Ni wanadamu wanakwaza.

Mie nina wa kwangu namdai karibia kodi ya miezi 8. Nasikia anajinasibu kwa wenzie anasema
"YAANI NIACHE KUMLIPIA MWANANGU ADA, NIMLIPE HUYO BOYA, FALA KODI YAKE..."

Namvutia pumzi
Dah,aisee mtu Kama huyo inatakiwa kumfanyia tu umafia wa aina tofauti
 
Back
Top Bottom