Ushauri wenu ni muhimu sana.
Umri wangu ni miaka 50, nimeoa mke kanisani huu ni mwaka wa 25 naishi naye na tumejaliwa watoto wanne, wa kwanza na wapili wamemaliza tayari chuo kikuu na wa tatu yupo chuo kikuu mwaka wa pili. Wa nne kamaliza kidato cha 4 mwaka jana, katikati hapo miaka 18 iliyopita bahati mbaya nikajiingiza kwenye mahusiano na binti wa miaka 20 wakati huo na akapata ujauzito, nilipomwambia nimeoa ili aitoe mimba ile na kwa kuwa bado ni binti mdogo anaweza kupata wa kumwoa, alikataa katakata. Na mimi kwa kuogopa maana alinitamkia kuwa atajiua kama nitamlazimisha kutoa mimba na kuwa yupo tayari kuishi na mimi kama mke wa pili na ujauzito ule hawezi kutoa kamwe.
Niliendelea kumshawishi atoe, matokeo yake akakimbia akaenda kwao mpaka akajifungua huko.
Lakini kiufupi zaidi, alirudi tena na kunitafuta na kunitishia kumwambia mke wangu, hivi ninavyoandika ilibidi nirudishe nyuma majeshi na kuanza kuishi naye kama mke wa pili.
Nilimpangishia chumba na maisha yakaendelea, baada ya muda alipata mtoto wa pili, wote ni wa kike, baada ya muda nilianza kuwasomesha kuanzia chekechea mpaka sasa hivi wa kwanza anafanya mtihani wa form Six mwaka huu na wa pili anafanya wa form 4 mwaka huu na wote wamesoma shule za Private toka chekechea mpaka sasa hivi na kwa wastani kila mmoja alikuwa ananigharibu 2.5m hasa shule za msingi mpaka secondary. Hapo bado michango mbalimbali na usafiri, kwa maana walikuwa wanasoma mikoani.
Baada ya kumpata mtoto wa kwanza akiwa kwenye chumba cha kupanga, niliona sina budi watoto wangu na mimi binafsi niwe na uhuru maana maisha ndio yalishaanza hivyo, na mimi upendo tayari ulishaingia na kuona ni maisha kama maisha mengine.
Ndipo nilipoamua kununua viwanja, kama unakumbuka miaka ile ya 2000 nadhani kuanzia 2006 serikali ilipima viwanja 20,000 maeneo mbalimbali ya DSM, mimi nilichukua viwanja viwili, wakati ule nakumbuka kimoja nilinua 1,800,000 na kingine 1,300,000 ml. Ukubwa ni sq m 1200 na 1000. Kimoja kikubwa nikamjengea nyumba ya mgongo wa tembo, vyumba 2 na sebule katikati na choo kizuri cha nje, nikaacha eneo kubwa tu kwa ajili ya kujipanga na kujenga nyumba kubwa baadaye, kumbuka huo ni mwaka 2007 alipohamia hapo au tulipohamia hapo.
Baadaye nimfungulia biashara ya saloon, akafanya kama miaka 2 vibaka wakaingia nakuiba kila kiatu, nikaona isiwe shida nikamfungulia mghahawa ambao ulikuwa na vitu 16 na meza nne kubwa, bado na wenyewe haukufanya kazi vizuri, nikamfungulia grocery ya bia na kuweka kila aina ya kinywaji kwa kutumia viti na meza za mghahawa.
Nayo haikufanya kazi vizuri, nikamnunulia Hiace iliyotumika tayari kama dala dala.
Na yenyewe usimamizi ukawa mgumu.
DA NITAENDELEA, MAANA DA SIPO VIZURI KABISA KIAKILI NI NIMECHANGANYIKIWA SASA HIVI.
MUENDELEZO WA TUKIO HILI SOMA HAPA CHINI:
SEHEMU YA 2
SEHEMU YA 3
SEHEMU YA 4
SEHEMU YA 5
SEHEMU YA 6
SEHEMU YA 7
SEHEMU YA 8
SEHEMU YA 9
SEHEMU YA 10
SEHEMU YA 11
SEHEMU YA 12
SEHEMU YA 13
SEHEMU YA 14
SEHEMU YA 15
SEHEMU YA 16
SEHEMU YA 17
SEHEMU YA 18
SEHEMU YA 19
SEHEMU YA 20
SEHEMU YA 21
Umri wangu ni miaka 50, nimeoa mke kanisani huu ni mwaka wa 25 naishi naye na tumejaliwa watoto wanne, wa kwanza na wapili wamemaliza tayari chuo kikuu na wa tatu yupo chuo kikuu mwaka wa pili. Wa nne kamaliza kidato cha 4 mwaka jana, katikati hapo miaka 18 iliyopita bahati mbaya nikajiingiza kwenye mahusiano na binti wa miaka 20 wakati huo na akapata ujauzito, nilipomwambia nimeoa ili aitoe mimba ile na kwa kuwa bado ni binti mdogo anaweza kupata wa kumwoa, alikataa katakata. Na mimi kwa kuogopa maana alinitamkia kuwa atajiua kama nitamlazimisha kutoa mimba na kuwa yupo tayari kuishi na mimi kama mke wa pili na ujauzito ule hawezi kutoa kamwe.
Niliendelea kumshawishi atoe, matokeo yake akakimbia akaenda kwao mpaka akajifungua huko.
Lakini kiufupi zaidi, alirudi tena na kunitafuta na kunitishia kumwambia mke wangu, hivi ninavyoandika ilibidi nirudishe nyuma majeshi na kuanza kuishi naye kama mke wa pili.
Nilimpangishia chumba na maisha yakaendelea, baada ya muda alipata mtoto wa pili, wote ni wa kike, baada ya muda nilianza kuwasomesha kuanzia chekechea mpaka sasa hivi wa kwanza anafanya mtihani wa form Six mwaka huu na wa pili anafanya wa form 4 mwaka huu na wote wamesoma shule za Private toka chekechea mpaka sasa hivi na kwa wastani kila mmoja alikuwa ananigharibu 2.5m hasa shule za msingi mpaka secondary. Hapo bado michango mbalimbali na usafiri, kwa maana walikuwa wanasoma mikoani.
Baada ya kumpata mtoto wa kwanza akiwa kwenye chumba cha kupanga, niliona sina budi watoto wangu na mimi binafsi niwe na uhuru maana maisha ndio yalishaanza hivyo, na mimi upendo tayari ulishaingia na kuona ni maisha kama maisha mengine.
Ndipo nilipoamua kununua viwanja, kama unakumbuka miaka ile ya 2000 nadhani kuanzia 2006 serikali ilipima viwanja 20,000 maeneo mbalimbali ya DSM, mimi nilichukua viwanja viwili, wakati ule nakumbuka kimoja nilinua 1,800,000 na kingine 1,300,000 ml. Ukubwa ni sq m 1200 na 1000. Kimoja kikubwa nikamjengea nyumba ya mgongo wa tembo, vyumba 2 na sebule katikati na choo kizuri cha nje, nikaacha eneo kubwa tu kwa ajili ya kujipanga na kujenga nyumba kubwa baadaye, kumbuka huo ni mwaka 2007 alipohamia hapo au tulipohamia hapo.
Baadaye nimfungulia biashara ya saloon, akafanya kama miaka 2 vibaka wakaingia nakuiba kila kiatu, nikaona isiwe shida nikamfungulia mghahawa ambao ulikuwa na vitu 16 na meza nne kubwa, bado na wenyewe haukufanya kazi vizuri, nikamfungulia grocery ya bia na kuweka kila aina ya kinywaji kwa kutumia viti na meza za mghahawa.
Nayo haikufanya kazi vizuri, nikamnunulia Hiace iliyotumika tayari kama dala dala.
Na yenyewe usimamizi ukawa mgumu.
DA NITAENDELEA, MAANA DA SIPO VIZURI KABISA KIAKILI NI NIMECHANGANYIKIWA SASA HIVI.
MUENDELEZO WA TUKIO HILI SOMA HAPA CHINI:
SEHEMU YA 3
SEHEMU YA 4
SEHEMU YA 5
SEHEMU YA 6
SEHEMU YA 7
SEHEMU YA 8
SEHEMU YA 9
SEHEMU YA 10
SEHEMU YA 11
SEHEMU YA 12
SEHEMU YA 13
SEHEMU YA 14
SEHEMU YA 15
SEHEMU YA 16
SEHEMU YA 17
SEHEMU YA 18
SEHEMU YA 19
SEHEMU YA 20
SEHEMU YA 21