Naomba ushauri kwenye tukio hili

cacashian01

Member
Mar 3, 2016
76
62
Habari wanajamvi.

Naomba msaada wa kufahamisHwa kisheria, nina Ndugu yangu alikua anafanya kazi kwenye mgahawa alikua anaaminika na Bosi wake pamoja na wafanyakazi wenzake,kwa pamoja wakaamua kuanzisha mchezo wakupeana Hela(upatu)ambapo yeye (Ndugu yangu) ndio aliyependekezwa na wenzake pamoja na bosi wake awe anaweka hela,

Waliendelea na mchezo na akawa anawakabidhi hela wale wanaopokea wakabaki watatu yani Bosi wake na wafanyakazi wengine wawili,na wakati huo mchezo ukiwa unaendelea Bosi akikwama anawaambia waazime hela kwa Ndugu yangu, na ndugu yangu alikua anaandika kila anachomkopesha bosi.

Sasa biashara ikawa sio nzuri Bosi akawasimamisha huku mchezo (upatu haujaisha) kwahiyo kwenye mahesabu Bosi anasema anadai Mil.1 wakati ndugu yangu kwenye hela alizo msainisha Bosi anatakiwa alipwe Laki 5 tu, na wingine wawili wanadai jumla ya laki . Sasa Bosi anamlazimisha Ndugu yangu alipe wakati wanaotakiwa kulipa kazi wamesimamishwa na yeye ndugu Yangu hadaiwi kwenye huo mchezo. Bosi anasema atampeleka polisi.

Msaada wenu afanyaje?
 
Mi sijaelewa hayo maelezo
Kiufupi ni kwamba walikua wanacheza mchezo wakupeana hela mwisho wasiku wakaachishwa kazi kabla mchezo haujaisha ni km upatu unatoa elfu 2 mbili leo ana pokea huyu kesho yule sasa kazi hamna na bosi anadai hela ambayo alikua naichukua na ilikua inaandikwa deni analojikopesha Bosi
 
Habari wanajamvi.

Naomba msaada wakufahamiswa kisheria,nina Ndugu yangu alikua anafanya kazi kwenye mgahawa alikua anaaminika na Bosi wake pamoja na wafanyakazi wenzake,kwa pamoja wakaamua kuanzisha mchezo wakupeana Hela(upatu)ambapo yeye (Ndugu yangu) ndio aliyependekezwa na wenzake pamoja na bosi wake awe anaweka hela.

Waliendelea na mchezo na akawa anawakabidhi hela wale wanaopokea wakabaki watatu yani Bosi wake na wafanyakazi wengine wawili, na wakati huo mchezo ukiwa unaendelea Bosi akikwama anawaambia waazime hela walizo kuwa wanachangisha za mchezo kwa Ndugu yangu.

Ndugu yangu alikua anaandika kila anachomkopesha bosi,sasa biashara ikawa sio nzuri Bosi akawasimamisha huku mchezo (upatu haujaisha) kwahiyo kwenye mahesabu Bosi anasema anadai Mil.1 wakati ndugu yangu kwenye hela alizo mkabidhisha bosi akikopa Bosi anatakiwa alipwe Laki 5 tu.

Wengine wawili wanadai jumla ya laki 8.sasa Bosi anamlazimisha Ndugu yangu alipe wakati wanaotakiwa kulipa kazi wamesimamishwa na yeye ndugu Yangu hadaiwi kwenye huo mchezo.Bosi anasema atampeleka polisi.

Msaada wenu afanyaje?
 
Kiufupi ni kwamba walikua wanacheza mchezo wakupeana hela mwisho wasiku wakaachishwa kazi kabla mchezo haujaisha ni km upatu unatoa elfu 2 mbili leo ana pokea huyu kesho yule sasa kazi hamna na bosi anadai hela ambayo alikua naichukua na ilikua inaandikwa deni analojikopesha Bosi
sasa si alipe yeye huyo bosi ..
 
Upatu ni kosa kisheria. Kwa mujibu wa sheria ya mikataba inaeleza kuwa mkataba wa kufanya kitu haramu basi mkataba huo ni haramu. Hapo hakuna jinai wala madai, mwambie akashtaki japo najua anaweza kutumia nguvu kuwahonga polisi lakini huyo ndugu yako awe ngangari kesi iende mahakamani.
 
Habari wanajamvi.

Naomba msaada wa kufahamisHwa kisheria, nina Ndugu yangu alikua anafanya kazi kwenye mgahawa alikua anaaminika na Bosi wake pamoja na wafanyakazi wenzake,kwa pamoja wakaamua kuanzisha mchezo wakupeana Hela(upatu)ambapo yeye (Ndugu yangu) ndio aliyependekezwa na wenzake pamoja na bosi wake awe anaweka hela,

Waliendelea na mchezo na akawa anawakabidhi hela wale wanaopokea wakabaki watatu yani Bosi wake na wafanyakazi wengine wawili,na wakati huo mchezo ukiwa unaendelea Bosi akikwama anawaambia waazime hela kwa Ndugu yangu, na ndugu yangu alikua anaandika kila anachomkopesha bosi.

Sasa biashara ikawa sio nzuri Bosi akawasimamisha huku mchezo (upatu haujaisha) kwahiyo kwenye mahesabu Bosi anasema anadai Mil.1 wakati ndugu yangu kwenye hela alizo msainisha Bosi anatakiwa alipwe Laki 5 tu, na wingine wawili wanadai jumla ya laki . Sasa Bosi anamlazimisha Ndugu yangu alipe wakati wanaotakiwa kulipa kazi wamesimamishwa na yeye ndugu Yangu hadaiwi kwenye huo mchezo. Bosi anasema atampeleka polisi.

Msaada wenu afanyaje?
Mueleze ndugu yako kuwa wote katika kundi lao walikuwa wanatenda jinai hivyo hakuna atakayesalimika .Rejea Kanuni ya Adhabu kifungu 171A Mpaka 171C .
 
Back
Top Bottom