Habari za usiku?
Nguruwe wangu mmoja alipoteza hamu ya kula. Baada ya siku moja tulimtoa zizini tukamweka nje ambako hakuna sakafu.
Aliendelea kukataa chakula chochote. Hakutaka kunywa maji. Alitumia muda mwingi kufukua na kuchimba kwa pua yake.
Alikuwa na nguvu nyingi za kufukua. Alipokuwa akichoka analala. Tulihisi ni homa ya nguruwe lakini hakuwa na homa, hakutapika, hakuharisha.
Baada ya siku tano tangu kuona dalili tulimchinja ili kufanya uchunguzi wa tatizo alilokuwa nalo. Daktari alibaini alikuwa amevimba na kuoza ini mojawapo. Hakuwa na tatizo jingine.
Leo nimeona nguruwe wengine wawili wenye hali hiyo. Hao na wengine waliosalia amewadunga vetoxy.
Naomba msaada wenu wadau.
Nguruwe wangu mmoja alipoteza hamu ya kula. Baada ya siku moja tulimtoa zizini tukamweka nje ambako hakuna sakafu.
Aliendelea kukataa chakula chochote. Hakutaka kunywa maji. Alitumia muda mwingi kufukua na kuchimba kwa pua yake.
Alikuwa na nguvu nyingi za kufukua. Alipokuwa akichoka analala. Tulihisi ni homa ya nguruwe lakini hakuwa na homa, hakutapika, hakuharisha.
Baada ya siku tano tangu kuona dalili tulimchinja ili kufanya uchunguzi wa tatizo alilokuwa nalo. Daktari alibaini alikuwa amevimba na kuoza ini mojawapo. Hakuwa na tatizo jingine.
Leo nimeona nguruwe wengine wawili wenye hali hiyo. Hao na wengine waliosalia amewadunga vetoxy.
Naomba msaada wenu wadau.