Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dawa ya vidonda ni kupunguza mawazo / stress.Habari za muda huu wadau nimeteseka sana na vidonda vya tumbo sasa nataka ushauri hospitali gani niende naweza pata vipimo vizuri vikanisaidia,hapo mwanzo nilikuwa naenda hospital za kawaida kutokana na kipato ila kwa sasa nimekusanya pesa kama laki tisa kwa ajili ya kwenda kupata vipimo vya uhakika,Nitangulize shukran kwenu
Sent using Jamii Forums mobile app
Badilisha diet ya uchafu unaoingia tumboni.....acha mavyakula yenye Acid tumboni mwako punguza kula damu (nyama) kula matunda kwa sana na mboga mboga ndio kiwe chakula chako. Na unywe maji mengi sana.Habari za muda huu wadau nimeteseka sana na vidonda vya tumbo sasa nataka ushauri hospitali gani niende naweza pata vipimo vizuri vikanisaidia,hapo mwanzo nilikuwa naenda hospital za kawaida kutokana na kipato ila kwa sasa nimekusanya pesa kama laki tisa kwa ajili ya kwenda kupata vipimo vya uhakika,Nitangulize shukran kwenu
Sent using Jamii Forums mobile app
Naomba nije pm kwakona mimi nina hiyo shida,lakini kuna dawa ya kienyeji nilipewa imenisaidia sana tofauti na nilivyokuwa nikitumia dawa za hosptln.
Hiyo dawa nilipewa na msabato jirani angu
Fuata ushauri kupitia hii post. Hosp waweza kuandikiwa Heligo kit, ina dawa zenye combination nzuri. Ukifuata masharti yake utapona kabisa!VIDONDA VYA TUMBO NA TIBA YAKE
Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula ni mfumo unaohusika na umeng'enyaji wa chakula mpaka kuwa katika hali inayoweza kusharabiwa na mwili.
Sehemu kuu zinazohusika katika umeng'enyaji huo ni kinywa, umio 'Esophagus', mfuko wa tumbo 'Stomach', ini, mfuko wa nyongo, utumbo mwembamba 'Duedenum & Ileum', kongosho, utumbo mpana na puru 'Rectum'.
Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula hasa kuta za umio, tumbo na utumbo mwembamba hupata mmomonyoko ambao husababishwa na asidi inayotumika kumeng'enya chakula inaposhambulia kuta hizo. Kitaalamu hali hii hutambulika kama 'Peptic ulcers'.
stomach_ulcers
Vidonda vya mfumo wa umeng'anyaji chakula vikiwa kwenye tumbo tunaita vidonda vya tumbo 'Gastric ulcer', vikiwa katika duodenum tunaita 'Duodenal ulcer' na vikiwa katika esophagus tunaita 'Esophageal ulcer'
SABABU ZA VIDONDA VYA TUMBO
Bakteria aina ya Helicobacter pylori 'H.pylori' & Non-Steroidal Anti Inflammatory Drugs 'NSAIDs' ndio visababishi vikuu.
Bakteria H.pylori wanahusika sana kwa angalau nne ya tano ya vidonda vya tumbo 'Gastric ulcers' & 95% ya 'Duodenal ulcers' ambapo NSAIDs husababisha 20% ya 'Gastric ulcers' na 5% ya 'Duodenal ulcers'
Bakteria H.pylori husababisha kupitia vyakula na maji. Pia hupatikana kwenye mate ya binadamu hivyo inaweza kusambazwa mdomo kwa mdomo wakati mkila denda/kunyonyana midomo.
Bakteria H.pylori huishi kwenye kuta za utumbo na hutengeneza vimeng'enya 'Enzyme' iitwayo 'Urease' inayopunguza athari za asidi kwenye utumbo.
Utumbo hutaka kufidia kiasi cha asidi kinachopotea kwa kutengeneza zaidi na husababisha kukwangua kuta za utumbo.
Non-Steroidal Anti Inflammantory Drugs 'NSAIDs' ni dawa za kutuliza maumivu ya kichwa, maumivu ya hedhi, kushusha homa na kuondoa maumivu madogo madogo mfano Aspirin, Ibuprofen,Diclofenac & Meloxicam. Dawa hizi hupunguza uwezo wa kuta za tumbo na kufanya uwe rahisi kushambuliwa na asidi za tumboni hivyo kusababisha vidonda.
Chembe za urithi 'Genetics': Idadi kubwa ya watu wenye vidonda vya tumbo wana ndugu wa karibu wenye vidonda pia, hii huwafanya wataalamu kufikiria kuwa chembe za urithi zinahusika pia.
Uvutaji sigara/tumbaku: Wavutaji wa sigara wako katika hatari ya kupata vidonda vya tumbo ikilinganishwa na wasiovuta.
Matumizi ya pombe/vilevi: Walevi wako katika hatari zaidi ya kupata vidonda vya tumbo ikilinganishwa na wasiotumia vileo/pombe.
Msongo wa mawazo 'Mental stress': Msongo wa mawazo hausababishi vidonda moja kwa moja ila hufanya hali kuwa mbaya zaidi kwa wagonjwa.
DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
Maumivu ya tumbo na huwa makali zaidi pale asidi inapopita juu ya vidonda.
...Maumivu yanaweza anzia kwenye kitovu na kupanda juu hadi katikati ya kifua 'Epigastric pain'
...Maumivu yanaweza kuongezeka unapokuwa njaa. Pia yanaweza kuwa makali wakati wa usiku kwenye mida ya kulala, yanayoweza kupunguzwa kwa kula chakula kidogo.
Kushindwa kumeza vizuri chakula.
Chakula kukwama kama kinataka kurudi mdomoni.
Kujisikia vibaya baada ya kula.
Kupungua uzito.
Kukosa hamu ya kula.
DALILI HATARI
Kutapika damu.
Kupata choo kikubwa cheusi au chenye damu nzito.
Kichefuchefu & kutapika.
JINSI VIDONDA HUGUNDULIWA:-
Maelezo ya mgonjwa juu ya dalili alizonazo humsaidia daktari kuhisi kinachomsumbua mteja wake ni vidonda vya tumbo.
Ili kuthibitisha vidonda vipimo vifuatavyo hufanyika :-
Kupima damu 'Blood test'
Kuangalia bakteria aina ya H.pylori na kama mgonjwa amekuwa akitumia antibayotiki au dawa za vidonda Proton Pump Inhibitors 'PPIs' mfano Omeprazole vipimo vyake vya damu vitaonyesha majibu hasi 'Negative'
Kupima pumzi 'Breath test'
Mgonjwa hupewa anywe maji yenye atomi za kaboni zinazoweza kuvunjika, hii hufanya bakteria H.pylori kuvunjika na baada ya lisaa mgonjwa hutoa pumzi kwenye chombo kilichofunikwa kama mgonjwa ameambukizwa sampuli ya pumzi itaonyesha vipande vya kaboni kwenye kabonidioksaidi.
Kupima antijeni kwenye kinyesi 'Stool antigen test'
Kipimo hiki huangalia kama kuna bakteria H.pylori kwenye kinyesi. Vilevule kipimo hiki hutumika kuangalia ufanisi wa matibabu yaliyotolewa dhidi ya bakteria.
X-ray ya sehemu ya juu ya tumbo 'Upper gastrointestinal x-ray'
Picha huonyesha umio 'Esophagus', mfuko wa tumbo 'Stomach' na Dudenum. Mgonjwa humeza maji yenye 'Barium' ambayo hufanya vidonda kuonekana kirahisi kwa x-ray.
Kamera ya tumbo 'Endoscopy'. Mrija mrefu wenye kamera huingia tumboni na daktari huona vidonda kwenye skrini ya kompyuta 'Monitor'.
MATIBABU YA VIDONDA VYA TUMBO
Kama vidonda vitakuwa vimesababishwa na bakteria H.pylori dawa za kuua na kuondoa bakteria hutumiwa.
Kama vidonda vya tumbo vitakuwa vimesababishwa na 'NSAIDs' na hana maambukizi ya bakteria H.pylori atapaswa kutumia dawa Proton Pump Inhibitors 'PPIs'
Proton Pump Inhibitors 'PPIs' hufanya kazi kwa kuvunja/kuzuia kazi ya protini ziitwazo 'Proton Pump' ambazo huhusika katika utengenezaji wa asidi tumboni.
Matumizi ya NSAIDs kwa ajili ya kuondoa homa na maumivu yatalithiwa na dawa kama Paracetamol.
Matibabu yaliyozungumziwa hapo juu yanaweza kuchukua muda kabla ya kuanza kufanya kazi hivyo daktari anaweza kuongeza matibabu mengine kama vizuia asidi 'Antiacids' & 'Alginates' kwa ajili ya nafuu ya haraka.
Usitumie dawa hizi ndani ya lisaa moja baada ya kunywa PPIs mfano Omeprazole au H2-Receptor Antagonists mfano Cimetidine.
Matibabu kwa njia za asili, zipo dawa mbali mbali unazoweza tumia zikiwa kwenye mfumo wa unga au kimiminika
Kwa ushauri na tiba kwa maradhi mbali mbali wasiliana nasi.
what's app /call
+255 655 821 550
Sulayman Sangida
Sent using Jamii Forums mobile app
karibu
vp mkuu umepona now?Ni mwezi sasa tangu nimekutwa na huyo H. Pylori! Nashukuru naendelea na Dawa alizoniandikia Dr
chenga tupu babu!
sahivi natumia vitunguu swaumu, naona nafuu leo siku ya nne.chenga tupu babu!
hamna Kitu!
na mimi ndio nimeanza