Naomba ushauri katika suala la elimu

haloo

JF-Expert Member
Aug 19, 2016
569
217
Habari wanajamvi

Mimi ni miongoni mwa wahitimu wa chuo kikuu mwaka huu katika fani ya elimu wa masomo Economics na Geography.na form six nilisoma kombi ya HGE yaani History,Geography na Economics.

Kutokana na matamko yalioyotokea siku chache zilizopita kuhusu serikali kutoa ajira kwa walimu wa sayansi tu.Nimetafakari sana nimeamua kurudi nyuma na kuamua kurudia mtihani wa form six lkn kwa kombi ya EGM kwa kuliongeza somo la Mathematics.Ili nisome diploma ya Elimu kwa Masomo ya Geograph na Mathematics ili niweze kupata ajira serikalini kwa sababu nikifiria niweze kujiajiri inashindikana sababu ya mtaji.

Na vile vile Matokeo yangu ya Form four ni mazuri sana masomo yoote nimefaulu ikiwemo na Yale yoote ya sayansi .Nimeamua kusoma EGM kwa sababu katk masomo hayo yoote ninamsingi nayo hususani Geography na Economic s na vile vile hata hilo la Mathematics ninamsingi kidogo wa BAM
 
Kwa hiyo naombeni ushauri hapo inawezekana ? Sababu nataka nitumie mwaka mmoja tu wa maandalizi INSHAALLAH
 
Kwa hyo advanced maths ya advnc kuisoma mwaka mmoja alf ukfaulu n kazz nguumu mno hasa ukizngatia gred za huyu mama !
 
Inawezekana lakini nadhani ni vyema ukafanya mpango wa kujiajiri kuliko kutegemea kuajiriwa na serikali.
Kwa mtu kama wewe wa HGE tena mwenye shahada ya elimu (Economics&Geography) bado una nafasi kubwa ya kuajiriwa hata shule binafsi ambako utapiga kazi kwa lengo la kupata mtaji.
Kwa mwezi huu kabla shule hazijafunguliwa jaribu kucheki shule binafsi utapata na imani.
 
shule binafsi nazo zina walimu wa kumwaga wa arts tena wana minywa mshaara hatali sasa wewe nakushauri hama tu hii nchi nenda south africa yapo maisha kijana
 
kwanza pole sana shule binasfi siku zote zina walimu wa kutosha pili kurudi kusoma mathematics lazima uwe na msingi mzuri wa hesabu bam sio kigezo cha kufanya uende pure nilisoma hesabu advance naijua shida yake kamahunamsingi mzuri narudia polesana kila la kheri.
 
Dah kuanza upya mkuu, huna ulilokosa we jiajir tu kwa maana chuo nilitaka nianze kuuza maji nikaamua nirud nyumban isiwe shida kwa maana elimu saiv ni kaa la moto
 
Kwa hyo advanced maths ya advnc kuisoma mwaka mmoja alf ukfaulu n kazz nguumu mno hasa ukizngatia gred za huyu mama !
hapo yeye atakuwa anasoma somo moja mkuu topics km 17 hv km atajitoa ataweza sasa asije mpaka anapofika chuo mwaka wa pili akaambiwa walimu wa math wamejaa sijui itakua (nimewaza tu)
 
hapo yeye atakuwa anasoma somo moja mkuu topics km 17 hv km atajitoa ataweza sasa asije mpaka anapofika chuo mwaka wa pili akaambiwa walimu wa math wamejaa sijui itakua (nimewaza tu)
Nia yangu ni kusoma diploma na sio degree harafu kuwa na msingi wa pure msingi ninao
 
kasome diploma ya biomedical engineer hutafikiria kuajiliwa mkuu vigezo uwe umefaulu fizikia kemia na biolojia vyema
 
Habari wanajamvi

Mimi ni miongoni mwa wahitimu wa chuo kikuu mwaka huu katika fani ya elimu wa masomo Economics na Geography.na form six nilisoma kombi ya HGE yaani History,Geography na Economics.

Kutokana na matamko yalioyotokea siku chache zilizopita kuhusu serikali kutoa ajira kwa walimu wa sayansi tu.Nimetafakari sana nimeamua kurudi nyuma na kuamua kurudia mtihani wa form six lkn kwa kombi ya EGM kwa kuliongeza somo la Mathematics.Ili nisome diploma ya Elimu kwa Masomo ya Geograph na Mathematics ili niweze kupata ajira serikalini kwa sababu nikifiria niweze kujiajiri inashindikana sababu ya mtaji.

Na vile vile Matokeo yangu ya Form four ni mazuri sana masomo yoote nimefaulu ikiwemo na Yale yoote ya sayansi .Nimeamua kusoma EGM kwa sababu katk masomo hayo yoote ninamsingi nayo hususani Geography na Economic s na vile vile hata hilo la Mathematics ninamsingi kidogo wa BAM
Mkuu nakushauro ufuate ushauri wa SODOKA, Utatoka tu kama unataka kusoma, sikushauri kurudi sekondari
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom