Naomba ushauri: Kati ya Kluger V na Harrier ni gari ipi ni nzuri zaidi?

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,661
18,035
1594721183725.png

Kluger V
1594721221104.png

Harrier

Wakuu, nimejipanga kwa muda wa kutosha na sasa naona naweza kujipatia usafiri wangu wa kueleweka. Kuna gari hizi mbili zote nazipenda sana. Naomba kushauriwa na wenye uzoefu na uelewa mkubwa wa hizi gari mbili ni ipi wanaona ni nzuri zaidi? Suala la mafuta sio tatizo, lakini uimara wa gari na hadhi ya gari na gharama ya gari. Nimetenga bajeti ya milioni ishirini na tano mpaka thelathini kwa mchakato wote.

Karibuni tushauriane.


MAONI YALIYOTOLEWA NA WADAU:
Brother, I have been into both mess.
Kluger nyepesi, na haina matoleo tofauti tofauti kama Harrier. Kwa issue ya status hakuna wa kukuona outdated.

Fuel consumption zote zinaendana 6-8Km/lt.
Engine zote VVTI.

Harrier nzito na ipo comfortable kiasi chake kuzidi kidogo Kluger..

Generally both are good cars.
Cha msingi tafuta gari iliyotembea km chache na iliyo kwenye condition nzuri.
Make a budget of not more than 28M for Harrier and 24M for Kluger.
All the best.
---
Harrier (Lexus)
6c9e834b9c486246b0a32976c016ef81.jpg


Kluger V
f0c638ecda4daa9a678197f3f35335a4.jpg


Volvo xc90
50bb30c9b4d1dca9f53a951eaab9f3c9.jpg


Kazi kwako. Pia zingatia na umri wako. Ila kama umri umesogea kaa humu Toyota Fortuner
9e66bcfc126d59ba3860e0ef9e103e1d.jpg
---
Hongera kwa hatua uliyoifikia ya kununua gari. To clarify; binafsi sijawahi kumiliki haya magari, usiscroll down kwanza! Nisikilize, but nina experience na Kluger na nitakupa mtazamo wangu wa Toyota Harrier.

My cousin anatumia Toyota Kluger V, nilishaiendesha mara kibao tu, since yeye hata hawezi kuendesha ana dereva wake, so most of the time unalikuta home tu. And this is my review:

Toyota Kluger ni gari zuri, heshima mjini. Ndani lina nafasi kubwa, ukipata yenye sunroof utaenjoy maana zinakuwaga na bonge la sunroof. Speakers are loud enough, seats are high enough kukupa high visibility ya barabara. Though sidhani kama interior italingana na Harrier.

Mafuta linakula vizuri, 1l/10km, ila naona umesema mafuta sio issue. Acceleration is fine for a huge vehicle, mimi sio mtu wa speed so siwezi zungumzia kuhusu hilo. But lina hundle vizuri barabara zetu za Boko. Though at some point nahisi lipo chini sana, maybe its just me.

Nina doubt sana 4WD yake though kwa hapa Dar haitakuzingua unless wewe ni engineer wa REA. So expect it to take you anywhere. Barabarani linatulia mpaka raha. Vidimbwi havisikiki, wewe ni kunesanesa tu. At night, taa zake nazipa salute, stock lights. Overall handling yake imetrump Rav4 na Suzuki Escudo. Its an SUV that handles like a Sedan.

Conclusion:
Like I said Harrier sijawahi kuliendesha wala kulipanda. Zaidi nalionaga kwa majirani na barabarani, but I can tell you, kama wewe ni bishoo chukua tu Harrier, lile gari lina turn heads. Kwa looks Kluger haliiwezi Harrier. Kluger lina sura ngumu kama limao, Harrier limekaa kama Qatar Airways. Also, Harrier linaonekana liko juu in terms of ground clearance, so I think lita handle vizuri zaidi Barabara za vumbi.

Just to remind you unacompare Harrier latest kidogo na Kluger la zamani, so obviously Harrier litali trumplify Kluger. Mtazamo wangu kama hela sio ya mawazo chukua Harrier uongeze Instagram likes, ila kama unataka hizo extra 2-4m uweke heshima bar chukua Kluger.

Hope I answered your question. Enjoy your new car.

-callmeGhost
---
Kwa nijuavyo Harrier na Kluger:

Ni kitu kimoja, ukiwa na Kluger, jua kwamba ni sawa na una Harrier tu maana ni gari ile ile tu, ila wameitofautisha kwenye muundo wa nje tu pamoja na majina basi!

Lakini kila kitu ni kile kile yaani. Kuanzia engine capacity & machenically etc

So, ni wewe tu uchague ni aina ya muundo unaouopenda. (I mean, muundo wa Harrier au Kluger)

By the way, okoa fedha nyingi kwa kununua gari yoyote unayohitaji kupitia ecarstanzania
Sisi ni waingizaji wa magari bora na kwa gharama nafuu kabisa.

Tupo Kinondoni, Ada Estate.

Email : ecarstanzania@gmail.com

Karibu


MREJESHO WA MDAU BAADA YA KUSOMA MAONI YA WANA JF
Mrejesho: Baada ya kupitia post nyingi humu na kwa kuzingatia ushauri wa family members tayari nimeshanunua Kluger V nyeusi: Cylinder 6, CC 3,000. Nimeshaitumia kwa zaidi ya miezi 5. Kwenye highway haitumii sana mafuta, japo huwezi kuilinganisha na utumiaji mafuta wa gari ndogo. Kwenye mizunguko ya mitaani na mjini hapo ulaji wake wa mafuta uko juu kidogo. Ila nimeipenda sana na sijajuta.

Nashukuru sana kwa michango yenu.
 
Wakuu, nimejipanga kwa muda wa kutosha na sasa naona naweza kujipatia usafiri wangu wa kueleweka. Kuna gari hizi mbili zote nazipenda sana. Naomba kushauriwa na wenye uzoefu na uelewa mkubwa wa hizi gari mbili ni ipi wanaona ni nzuri zaidi? Suala la mafuta sio tatizo, lakini uimara wa gari na hadhi ya gari na gharama ya gari. Nimetenga bajeti ya milioni ishirini na tano mpaka thelathini kwa mchakato wote.

Karibuni tushauriane.

Kluger nadhani huwa zina gia 4, so expect fuel consumption to be high. For me harrier ndio mpango mzima hasa zile zenye engine ya vvti
 
sina gari sijawai kumilika hata baiskeli ina hamuwezi kuamini ni magari machache sana sijawai kupanda.yaani machache . hizi lift hizi saa zingine ukute kuna watu wanaiba nyota yangu ya kumiliki gari wakinipa lift. kwanini nipande magari makali makali ya wenzangu na kuishia kupiga honi tu na kupungia watu? why?
 
Wakuu, nimejipanga kwa muda wa kutosha na sasa naona naweza kujipatia usafiri wangu wa kueleweka. Kuna gari hizi mbili zote nazipenda sana. Naomba kushauriwa na wenye uzoefu na uelewa mkubwa wa hizi gari mbili ni ipi wanaona ni nzuri zaidi? Suala la mafuta sio tatizo, lakini uimara wa gari na hadhi ya gari na gharama ya gari. Nimetenga bajeti ya milioni ishirini na tano mpaka thelathini kwa mchakato wote.

Karibuni tushauriane.
Usisahau kuweka taarifa zako za kifedha karibu, TRA watazihitaji
 
Wakuu, nimejipanga kwa muda wa kutosha na sasa naona naweza kujipatia usafiri wangu wa kueleweka. Kuna gari hizi mbili zote nazipenda sana. Naomba kushauriwa na wenye uzoefu na uelewa mkubwa wa hizi gari mbili ni ipi wanaona ni nzuri zaidi? Suala la mafuta sio tatizo, lakini uimara wa gari na hadhi ya gari na gharama ya gari. Nimetenga bajeti ya milioni ishirini na tano mpaka thelathini kwa mchakato wote.

Karibuni tushauriane.

Brother, I have been into both mess.
Kluger nyepesi, na haina matoleo tofauti tofauti kama Harrier. Kwa issue ya status hakuna wa kukuona outdated.

Fuel consumption zote zinaendana 6-8Km/lt.
Engine zote VVTI.

Harrier nzito na ipo comfortable kiasi chake kuzidi kidogo Kluger..

Generally both are good cars.
Cha msingi tafuta gari iliyotembea km chache na iliyo kwenye condition nzuri.
Make a budget of not more than 28M for Harrier and 24M for Kluger.
All the best.
 
Nina harrier, yangu naonaga ipo tofauti kidogo na harrier nyingine. Ya kwangu iko na automatic na manual gear anafanya kucontrol unachotaka. Kama mwezi hivi umepita nilitoka Dar saa 11 kwenda Kahama nilifika saa 10:30 kila mtu niliomwambia alikataa Harrier (Lexus) zinatembea sana kwa mpenda safari. Kluger kidogo ni zito. Sema consumption kidogo ni kubwa.
 
Back
Top Bottom