Naomba Ushauri: Kati ya BMW 3 Series 2006 model na Subaru Legacy B4 Sports 2006 model

Cha ajabu kuna mtu noilimwona Dodoma na BMW M3 E90 pia jana nimeona 535i...truth be told,magari yote ya ulaya kabla ya 2012 hayana ubora wa kudumu kabisa kwasababu walikua wanakimbizana na Lexus technologies ambao waliweka vitu vingi sana kwnye magari yao mwanzoni mwa 2000's. Kuna jamaa anadai rafiki yake ana Lexus GS300 imeshavuka km 1,000,000 kwenye odometer na kuanza upya lakini haisumbui kabisa. Nakushauri uchukue Subaru BMW, Benz, na mwengine waachie wenyewe ila exception ni Range Rover. Model za 2012 na kuendelea wanadai ziko reliable sana kiasi cha kupewa nyota 9 kati ya 10
 
Daah yaani BMW unailinganisha na vitu vya kijinga?

hahaha Subaru Gari Ya Kijinga? you cant be serious, ingia online soma comments za subaru model yoyote ila halafu uangalie gari zipi zimekuwa rated highly in all time car with stability and safety katika miaka mbali mbali na model mbali mbali mara nyingi. BMW sio gar mbaya ila you cant write off Subaru just yet. by the way Subaru ni moja kati ya gar chache ambazo na uhakika wa kugusa more than 250K plus in Km na bado ingine haijaguswa

by the way kuanzia model za miaka ya tisini subaru gar zao zote ni AWD bila kujali model.

NARUDIA BMW NI GARI NZURI SANA, ILA IPE HESHIMA YAKE SUBBY
 
Nunua BMW tu kama una pesa za service na spare parts,,. Nina experience na vw aisee siwezi kumshauri mtu anunue. It's the worse car kuwahi kuimiliki manake taa ya check engine ilikua inawaka kila wiki na gari inashinda garage kuliko home. Usiombe DSG transmission ianze kusumbua, hainaga fix ni msiba. Kwa mtu anaetaka kununua vw beware,,.
Duh!
 
Ni vitu 3 ndivyo vinavyowafanya binadamu kuamua ktk manunuzi au machaguo yao ya vitu
1 Brand name
2 Models
3 Performance

Brand name kigezo kikubwa cha kuuza bidhaa au kitu ni brand name yake hii ndio inayoongoza kwa kuuza bidhaa mfano kwenye nguo,simu,viatu,etc kwenye magari watu wengi wananunua magari kwa kufata brand names mfano Tanganyika brand name tunayonunua sana ni TOYOTA mtu akinunua toyota anaona kama spare zitapatikana kwa wepesi sana kumbe sio ni mazoea tu na kwa kenya ni NISSAN

Models hii ndio kigezo cha pili cha kuuza bidhaa au kitu watu wananunua vitu sana kutokana na model ya hyo bidhaa mfano ww umechagua subaru legacy B 4 na BMW 3 series za mwaka 2006 japo zipo subaru na bmw nyingi na za model mbalimbali

Performance hii ni hatua ya tatu ktk ununuzi au kuuza kwa bidhaa au kitu hii mala nying waafrica hatuijali sana lakini kwa wenzetu wanaijali sana mfano leo unataka kununua kitu kwa matumizi gani na matumizi yako yataitaji Performance gani ya hyo ndo maana kwenye gari kuna aina ya Performance kwa matumizi yake

Sasa inategemea kwa ww unaangalia nini ktk kununua magari hayo
1 brand name kwa maswala ya BN BMW is best
2 Model zote ni sawa kwani zote ni sedan na mwaka 2006 So hapo ni 50/50

3 Performance sasa inategemeana unataka Performance ya upande gani
A Stability & Maneuverability BMW is best
B speed Subaru is best

the choice is urs
Yani jamaa unachambua hizi gari hadi raha.
Mi binafsi nilikuwa nafikiria kununua kati ya Audi A4 au A6, BMW 3 series na Subaru legacy b4.
Na mimi nimeshapata majibu sasa, kati ya hizo tatu legacy b4 ni chaguo sahihi zaidi.
Abarikiwe aliyeanzisha huu uzi na wachambuzi.

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
BMW The Best
2bf4223ef0508c1acf5443b8556b876b.jpg
 
kumbuka kuna heshima na perfomance plus features zake ...kwa upande wangu subaru yoyote ya kwanzia 2005 kuja juu sio ya kuwaza mara mbili....afu TRA kodi kidogo chee spea kibao achana na hayo magari ya ki germany
 
Katika magari ambayo mjapani kayatengeneza aina ya sedani yenye comfortability yenye wazifa wa magari ya ulaya ni Toyota Crown mengine ni kawaida tu labda yale yanayouzwa Ulaya na Marekani kwani mjapani anatengeza magari kwa ajiri ya masoko ya Ulaya na Marekani lakini majina yanatofautiana na majina ya huku lakini muonekeno wa gari ni sawa sawa

BMW 3 series na Subaru legacy b 4

FUEL CONSAMPTION

Magari mengi ya ulaya ulaji wake wa mafuta ni mdogo sana ila yanatumia umeme ktk ops zake nying tofauti na magari ya japani so ktk swala la mafuta BMW ni best kwani
BMW kama gari aina tatizo lolote ktk mfumo wa mafuta ni 15 km/1 liter na full tank yake ni 57 liter so unaweza kwenda Km 855 kwa full tank

Subaru legacy b 4 kama aina tatizo ktk mfumo wa mafuta ni 8.9 Km/1 liter na full tank yake ni 64 titer so unaweza kwenda Km 569.6 kwa full tank

So umeona matumizi ya mafuta BMW 3 series is the best


SPEED
bmw
Transmision =6 speed outo
Horsepower @ RPM = 215@6250
Torque @ RPM = 2750
0-60 time = 6.7 sec

subaru legacy b 4
Transmision= 6 speed outo or manual
Horsepower @ RPM = 243@6000
Torque @ RPM =3600
0-60 time= 4.5 sec

Note RPM ni revolutions per minute inapatikana kwenye dashbord na inakazi ya kuonyesha speed ya engine kwa dakika

So katika speed subaru legacy is best


SPARE PARTS
katika ulimwengu huu hofu ya kuogapa kununua gari kwa kuhofia spare ilishakwisha hofu iliyobaki ni kupata mafundi wazuri wa gari tu spare unaagiza leo baada ya siku 3 au 4 umeshaipata

KUDUMU

kudumu kwa gari inategemea utunzaji na matumizi yako pia barabara unazotumia pia na uendeshaji kwani nimegundua Tanganyika madereva ni wachache sana ila waendeshaji wa magari wapo wengi unaweza jiuliza watu wanaagiza gari za mpaka miaka ya 1990 japani au Ulaya lakini zinaonekana mpya ikifika huku ndo zinachakaa pia hali ya hewa Africa inatuangusha sana gari aipatani na joto


KUTULIA BARABARANI
kuna kutulia barabarani kwa aina mbili
1 Stability ya gari
2 Maneuverability ya gari

BMW ikikimbia na kufika speed kuanzia 100 inashuka chini na ni kama ilivyo benz na unaruhusiwa kukata kona kali hata ukiwa na top speed ya 80Kmh

Subaru inakimbia sana lakini ipo kama Toyota Altezza na unaruhusiwa kukata kona kali hata ukiwa top speed ya 50 kmh zaidi ya hapo do @ your own risk

yani umeelezea mpaka nime furahi safi sana mkuu your the best
 
Back
Top Bottom