Naomba ushauri kama Baba mpya. Je, ni malezi yapi mazuri kati ya malezi ya Kiafrika au ya Wazungu?

abdulhamis

JF-Expert Member
Aug 2, 2019
1,436
2,292
Habari wadau wa JamiForums,

Mara nyingi huwa napenda ku-share mambo ili niweze kupata mawazo kutoka katika akili tofauti tofauti ili nipate majibu mengi tofauti na jibu ambalo huwa ndio limejibiwa na wengi basi huwa naliangalia na mimi tena kwa umakini then nalifuata.

Mimi ni kijana mwenyewe umri wa miaka 27 nimebahatika kupata mtoto mmoja nampenda sana na mimi kama Baba nataka nijitaidi kuwa Baba bora kwa Mtoto wangu kwa kusimamia kila kitu.

Nimekuja kwenu kuwauliza fikra zenu juu ya Malezi ya mtoto yatakayo kua Mazur kwa kwa afya yake ya mwili mpaka akili.

Kuna malezi aina mbili tuliyo nayo.

Moja ni malezi ya wazazi wa Kiafrika ambayo yana sifa nyingi sana nzuri na mbaya na malezi haya ndio niliyolelewa hata mimi moja ya mambo ambayo yalikuwa ni msingi katika malezi ya mtoto na ilikuwa lazima afuate zikiwemo sheria za kama mkubwa hakosei mtoto kwa wazazi hakui, mtoto haombwi msamaha, na mtoto hayupo huru kufanya jambo kisiri bila wazazi kujua

Malezi ya wenzetu wazungu kwanza mtoto anakua free Sana, mtoto akitaka kufanya kitu kwa wazazi anaomba ushauri tu na wala sio ruhusa pia mtoto akifiksha miaka 18 basi wazaz mkimuingilia kwenye mambo yake anaweza hata akawashtaki.

Pia mimi kama Baba kumwambia Mtoto wangu nakupenda ni sawa au kumuomba radhi mtoto wangu.
 
Kama hujajua nini wajibu wako wewe kama mzazi hadi sasa, unategemea ushauri wa malezi ya mwanao tokea watu wengine, na JF, uyumbishwe yumbishwe humu kama dera la Msomali niseme pole.

Parental insticts siku zote ndiyo zinatupa muongozo! Ukichanganya na mazingira na saikolojia. Ndiyo maana mtoto wa kisukuma aliyekulia Bariadi, Busanda, Misungwi, Ibadakuli, Dar, Mtwara, California, London, kuna vitu watafanana na kuna vitu watatofautiana.

Kila la heri katika safari ya malezi!

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
kwa mtt wa kike ili usiingiliwe,na kuanza kuletewa viboyfriend vyake Hadi sabuleni kwako,vikimutenda anakuja kushtaki kwako baba yake,na ukimkemea anatishia kunywa sumu akidai unamnyima Uhuru na unamnyanyasa!!,mkuu kwa kuwa ni ke mlee kwa malezi ya kiafrika,hutojuta kabisaaaa.
 
Mkuu kwa vile tayari ua idea na ufahamu wa aina zote mili za malezi hayo, basi ni wewe ufanye tathmii ya faida a hasara za aia hizo mbili za malezi!

Lakini anza kwanza kwa kujiangalia wewe mwenyewe kwa malezi ulopewa je ni nini faida yake na nini umekikosa?

Zaidi ya yote, malezi ya mtoto ni lazima pia yazigatie mazingira atakayokuja kuishi, kama utampa mtoto za Kitanzania wakati unajua ataishi Ulaya and viceversa is true, basi hapo utakuwa unamzidishia mtoto mzigo wa maisha magumu maana maisha tunayoishi sisi hivi sasa ni mepesi, lakini watakayoishi watoto wetu ni ghari zaidi! Fikiria mwaka 1990 laki 5 unapata kiwanja poa tu, vipi leo?
 
Baba mpya, hakuna formula ya malezi, mchanganyie mambo ya kale na ya kisasa, hiyo itampa asili yake pamoja na usasa. Mfundishe dini na kamwe asimuache Mungu
ukimchanganyia atakuwa chotara wa maadili mkuu,halafu atakuwa ni mtu ambaye Hana msimamo wa maamuzi.
 
Hongera sana chief,moja ya njia bora sana ya malezi kwa watoto ni mzazi kupenda kujifunza.
Wote tumetoka katika familia,so kuna namna tulipitia ambayo ilikuwa njema au ngumu,kupitia huko yapo ya kuchukua in positive/negative way.
Baba bora ni yule anayeweza kuwa kiongozi kupitia maisha yake mwenyewe anayoishi. Jua yakupasayo na yatende kwa ukamilifu.
 
Malezi yako wewe mwenyewe yanamtosha hakuna namna ambayo malezi ya watoto wa jamii fulani kuwa na malezi yanayofanana,Kwa sababu kila familia ina taratibu zake na tabia zake ni tofauti na familia nyingine, Hivyo lea wanao kutokana na mazingira yaliyopo.
 
Back
Top Bottom