Naomba ushauri jinsi ya kuacha kuangalia filamu za ngono

Mr Mose

JF-Expert Member
Jun 11, 2016
368
524
Mimi ni kijana wa miaka 23,tatizo langu ni kwamba napenda sana kuangalia video za kikubwa yaani X videos.

Nipo addicted kiasi kwamba napoteza muda na pesa nyingi kununua bando. Natamani kuacha lakini nashindwa, nina miaka kama minne sasa naangalia karibia kila siku.

Naombeni ushauri nifanyaje kuacha.
 
Ukimaliza kuangalia naamini hakuna madhara unayoleta kwenye jamii kama vile kubaka watu na kuku. So kwa ushauri wangu uendelee tu kwa sababu ndio starehe yako uliyoichagua.

Ila kwa umri huo pia najua ni mwanachama wa CHAPUTA bila ubishi.

Nawasilisha mkuu usinielewe vibaya hayo ni mawazo yangu binafsi unaweza kuyafuata au kuyaacha ukuina yanakufaa au hayakufai.
 
Uza DVD weka King'amuzi, Uza Desk & Laptop, Achana na Smart Phone tafuta Nokia Ya Kawaida tu na Usiweke Memory Card, halafu jiangalie vipi utaacha au hutoacha.
 
Mr Mose, msaada pekee ni Yesu kristo tuu ndiye atakayekusaidia kuyabeba hayo matatizo yako yote, peke ako kwa kuamua tu hutoweza. Ukiendelee kufanya hivo utazid viwango kila siku na kuacha itakua ngumu zaidi kwako, mpokee yesu hutopata kazi.
 
Rudi kwenye misingi ya imani yako, hope unaamini kuwa kuna Mungu. Usijipe muda wa kuwa idle, jichanganye na marafiki wakiwemo wa jinsia tofauti or fanya sana mazoezi muda wote unapokuwa huna la kufanya. Jifunze kutumia internet kwa mambo ya msingi na upunguze kiasi cha data unachonunua kwa matumizi yako ya kawaida.
 
Mkuu ingia hapo kama sio mvivu wa kusoma nna uhakika itakusaidia kama mimi ilivonisaidia. Niliacha kabisa ila ilinichukua muda kama miezi sita.
 
Hii kitu nikama vile mtoto anavyokuwa kikojozi wakati ukifika mwenyewe ataacha, hata hii mambo yakuangalia picha za x na punyeto wakati ukifika mwenyewe utaacha lakini usifikiri kwa umri huo kuna ushauri utakusaidia kwa %100 , itakusaidia japo sio sana jichanganye na watu, usipendi kukaa ndani peke yako , kuwa katibu na mpenzi wako mara kwa mara
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom