Naomba ushauri au msaada wa kisheria kuokoa hawa watoto

dumbi

JF-Expert Member
Jan 15, 2018
989
1,523
Habari zenu wakuu?

Nina dada yangu alizaa watoto wawili na mwanaume wa nchi fulani ya jirani hapa Africa na walifunga ndoa halali. Lakini badae wakaja kutengana na watoto akabaki nao mama yao, jamaa anahudumia kila kitu aliwajengea nyumba na shule wanasoma hizi za english medium.

Tatizo lilipo na kuwaomba ushauri ni kwamba huyu dada hana muda wa kuangalia hawa watoto, yeye akitoka asubuh kurudi usiku hajui watoto wameshindaje hapo nyumbani, hii imepelekea watoto kutokuwa na maendeleo mazuri shuleni mfano huyu mkubwa alitakiwa awe form 2 lakin yupo la sita amerudishwarudishwa.

Juzi juzi nilikuwa nao yule mkubwa akaniambia mjomba mimi nataka nikae na wewe sitaki kurud kwa mama muda mwingi tunakaa na njaa mpaka mama arudi usiku ndio tunakula na mengine mengi ameniambia.

Kibaya zaidi huyu mdogo amekuwa ana tabia za kike kike juzi kati nilipata kesi kwamba watoto wenzie wanamwingilia, mama yake alivyosikia hivyo alimpiga na marungu mpaka akawa hawezi kutembea na hii sio mara ya kwanza kumpiga manake ni mtundu sana mama anajua kupiga tu.

Mimi nilienda nikaongea nae mtoto kweli akakubali lakin anadai ni mara 2 tu. Huyu dada tumemshauri watoto waje waishi kwangu lakin yeye hataki, tena anatukana matusi mengi sana ukimgusia swala la watoto wakati anaona wanamshinda.

Baba yao ndio aliniomba zamani sana nikae na watoto lakini kwasabu dada ni mtata nilikataa sasa nimeamua niwachukue tatizo mama yao hataki je nifanyeje ili niweze kuchukua hawa watoto?
 
Duu fanya fasta mkuu kabla hujachelewa! Mwambie baba wa watoto awachukue,kwa muda then awalete kwako.
Yeye hayupo nchi hii mwanzo kabisa alitaka kuwachukua baraza la wazee wakampa ushindi sister sasa anasema kwa sasa hawezi mpaka wamalize shule manake shule zao huko hawafunsish english wala kiswahili sasa itakuwa ngumu shule.
 
Yeye hayupo nchi hii mwanzo kabisa alitaka kuwachukua baraza la wazee wakampa ushindi sister sasa anasema kwa sasa hawezi mpaka wamalize shule manake shule zao huko hawafunsish english wala kiswahili sasa itakuwa ngumu shule.
Huwezi kuwasiliana na hilo baraza la wazee na kuwaeleza hayo? wazazi wenu vp? Nionavyo ni wewe wa kuwaokoa ankles zako! Una mawili, kuwaokoa katika jahazi au kuwazamisha katika jahazi la machoko.

Pambana jombaaa.
 
Jaribu hii, mtafute shemeji yako wa sasa (anayempa utamu sister wako) uyajenge nae atakusaidia kuwaokoa wajomba zako.
 
Huwezi kuwasiliana na hilo baraza la wazee na kuwaeleza hayo? wazazi wenu vp? Nionavyo ni wewe wa kuwaokoa ankles zako! Una mawili, kuwaokoa katika jahazi au kuwazamisha katika jahazi la machoko.
Wazazi tushasahau kitambo,halafu ni mtu ambae haeshimu mtu anapayuka mahali popote na mtu yeyote haangalii umri.
 
Huwezi kuwasiliana na hilo baraza la wazee na kuwaeleza hayo? wazazi wenu vp? Nionavyo ni wewe wa kuwaokoa ankles zako!.. una mawili...kuwaokoa katika jahazi au kuwazamisha katika jahazi la machoko....

Pambana jombaaa.
Na hili la baraza ni zamani wakat watoto wadogo kwa sasa bado sijaenda popote.
 
fanya ufanyavyo uokoe hao watoto hasa huyo wakiume jaman ataharibikiwa hadi tumbo limeniuma aisee na nakuombea Mungu akusaidie katika harakati hiyo.
 
Shida wa Dada wanaweza child support ili maisha yaende bila kujali maendeleo ya makuzi ya watoto.
Hicho ndio ninachoona jamaa kasema yupo tayar ampe m 1 kama mtaji wa maisha yake atoe watoto,bado hatujamwambia lakin naona atakataa manake hawezi kujishuulisha kwakifupi anamdomo hata kwenye biashara.
 
Habari zenu wakuu?

Nina dada yangu alizaa watoto wawili na mwanaume wa nchi fulani ya jirani hapa Africa na walifunga ndoa halali. Lakini badae wakaja kutengana na watoto akabaki nao mama yao, jamaa anahudumia kila kitu aliwajengea nyumba na shule wanasoma hizi za english medium...
Mkuu nikupongeze sana kwa moyo huo wa huruma na upendo,jinsi unavyowapigania watoto wa dada yako na kuwa na uchungu nao hata kutafuta mbinu mbalimbali za kuwanusuru hao watoto,Mungu akubariki sana na kila la kheri.
 
Back
Top Bottom