Naomba uniulize chochote kuhusu kufanikiwa katika Biashara na Ujasiriamali

Hutegemei kuziuza?
AKIJA MTEJA MZURI NAUZA, NAUZA KWA MILIONI 7 ZOTE KWA PAMOJA, ALAFU NI FURSA NZURI SANA KWA KUHIFADHIA VITUNGUU, YAANI KUNA ILE MIEZI WANAVUNA VINGI THEN UKAHIFADHI KWENYE CAGE ZILE UKAPIGA PESA KIPINDI CHA UHABA WA VITUNGUU MWEZNI WA NNE,TANO NA SITA MWANZONI
 
Mkuu kwa tarifa tu,miradi yangu nasimamia mwenyewe mara nyingi, mke wangu na kaka yangu ndio kazi yao kubwa, sipigwi kwenye cost,ila tu mradi unakua hauna manufaa, kwamfano nimelima vitunguu Ruaha kule kiasi cha ekatano, ofcoz ukungu ulipiga sana nimevuna gunia 60 hivi lakini hata mteja simpati now ni second week, nilifuga kuku nyumbani kwangu Kimara wa nyama mwenyewe bila kutegemea mfanya kazi nikakosa soko kabisaa mpaka nikauza kuku mmoja 2500 wanaofuga hawa viumbe wanajua hasara yake. ni vitu vingi sana vilivyonitia hasara,ninahitaji kitu ambacho nitafanya mwenyewe preferbly of professional nitakachofanya mwenyewe kuanzia saa tisa na nusu mpaka usiku na siku za weekeend
Fanya kununua mazao msimu wa mavuno kama mahindi, mpunga ,vutunguu na kuleta sokoni. Una angalia bei ikoje sokoni halafu unajumua shamba unaleta dar .
 
Fanya kununua mazao msimu wa mavuno kama mahindi, mpunga ,vutunguu na kuleta sokoni. Una angalia bei ikoje sokoni halafu unajumua shamba unaleta dar .
Asante sana mkuu kwa ushauri,ila naona uletaji mazao mjini inahitaji kidogo uwe na godown in case hujapata mteja wa kununua
 
Laki 3 kwa sasa haitakufikisha sehemu boss, kama ungekuwa na vifaa say feeders, drinkers nk ungeweza kuanza na japo broilers 50. Napo faida itakua kiduchu sana
nikitaka kupata faida nzuri kidogo, nianze na mtaji kiasii gani?
 
**Kutokuwa na taarifa sahihi - mtu anasikia biashara ya tikiti maji inalipa haswa, kesho anaingia shamba kulima tikiti, hajui chochote ye anawaza akivuna atapiga faida Milioni kadhaa.

**Mitaji ya kuunga unga - unakuta mtu ana mtaji mdogo lkn anataka afanye biashara kubwa ili apate faida kubwa, anaishia kuteketeza kile kdg alichonacho.

**Kutokujua principles za biashara kama uvumilivu - mtu anaanza biashara asubuhi anataka jioni aone faida. Au unakuta mtu kuyumbishwa kdg tu na upepo anaamua kuacha kabisa biashara.
Nimekuelewa hapa acha tu..
 
Mkuu kwa tarifa tu,miradi yangu nasimamia mwenyewe mara nyingi, mke wangu na kaka yangu ndio kazi yao kubwa, sipigwi kwenye cost,ila tu mradi unakua hauna manufaa, kwamfano nimelima vitunguu Ruaha kule kiasi cha ekatano, ofcoz ukungu ulipiga sana nimevuna gunia 60 hivi lakini hata mteja simpati now ni second week, nilifuga kuku nyumbani kwangu Kimara wa nyama mwenyewe bila kutegemea mfanya kazi nikakosa soko kabisaa mpaka nikauza kuku mmoja 2500 wanaofuga hawa viumbe wanajua hasara yake. ni vitu vingi sana vilivyonitia hasara,ninahitaji kitu ambacho nitafanya mwenyewe preferbly of professional nitakachofanya mwenyewe kuanzia saa tisa na nusu mpaka usiku na siku za weekeend
Kwanza pole sana

Mkuu kilicho kuangusha ni soko, ulianza miradi bila kuwa na soko la uhakika.

Wengi huwa tunafeli hapo na hata hizi taarifa tunazopeana kwenye mitandao kuhusu ufagaji na kilimo utakuta tuna ongelea zaidi gharama na faida lakini Mara chache mno watu wataongelea soko kwa undani.

Rudi tena kwenye miradi mkuu Ila Safari hii anza kwanza kulijua soko vizuri la kitunguu na kuku. Uzuri mkuu Ontario kajitolea kuunganisha watu na soko la uhakika la kuku.

Kingine kwenye kilimo jifunze ni wakati gani soko linakuwa limejaa zao husika kwa maana wakulima wengi wanakuwa wanavuna na wakati gani zao linakuwa halipatikani kwahiyo wewe hakikisha unalima ili uvune kipindi ambacho zao husika (kitunguu) halipo kwa wingi sokoni. Ila hapa nitoe angalizo, Mara nyingi kulima ili uje kuvuna kipindi ambacho kitunguu kipo kichache sokoni huwa kuna Changamoto sababu Mara nyingi huwa ni msimu ambao Hali ya hewa hairuhusu kitunguu kustawi Kama wewe ulivyo kumbwa na ukungu Ina maana ulilima kipindi ambacho sio favorable kwa kitunguu, kwahiyo kipindi hili inabidi uwe na uangalizi wa Hali ya juu mnoo, ukifanikiwa kuvuna hata gunia 60 kwa ekari kipindi hiki umetusua


Kila la kheri

Aluta continua
Mapambano yanaendelea
 
Hongera kwa mafanikio mkuu ONTARIO nilikuwa na uliza kama ulishawah kufanya kilimo cha greenhouse na experience yako ikoje katika ulimaji wa mboga mboga!
 
1. Kupanua uzalishaji wa Bidhaa maana yake ni kua bidhaa unazozalisha ni chache kuliko mahitaji ya clients wako. Kama bado unastruggle kupata clients, njia 1 na rahisi ni kuadd new features kwenye product yako ambayo wengine hawana, hata aina ya packaging pekee inaweza kukutofautisha, pia kuangeza quantity kwa bei ile ile.

Unajua kwenye biashara kitu cha kwanza kbs ni kuWin people's hearts, then ukitoka hapo ndio uanze kufikiria kutengeneza faida. Kama hauna consistent clients hauwezi kutoa products zako hivyo hauwezi kutengeneza faida. Kwahiyo uwe tayari kuingia gharama za kuwavutia wateja ambayo wazungu wanaita 'client acquisition'.

2. Mimi nahisi kwa products zako soko la ndani lenyewe ni kubwa sana, nahisi bado haujafanya utafiti wa kutosha. Lkn again sio mbaya kuingia kwenye soko la nje kama upo tayari.

Mimi mwaka jana nilivuna vitunguu November, lkn soko la bongo lilikuwa ovyo mno mno. Ukienda Kkoo na Buguruni bei ni elfu 70-80 wakati kipindi kama hiko mwaka 2015 bei ilikua 180k. So nilichokifanya ni kuuza Kenya, nilienda kwa bus hadi Nairobi, nikakutana na madalali wakanipa dira na kila kitu. Baadae nilivuna na kuuza mzigo wangu Garissa krb na mpaka wa Somalia kusini mwa kenya mbapo niliuze kwa bei mara 3 ya iliyokuepo bongo.

Mkuu naomba kupata taarifa hasa vibali na namna ya kupitisha mzigo boarder na connection za kuuza kitunguu huko kenya.
 
Kwanza pole sana

Mkuu kilicho kuangusha ni soko, ulianza miradi bila kuwa na soko la uhakika.

Wengi huwa tunafeli hapo na hata hizi taarifa tunazopeana kwenye mitandao kuhusu ufagaji na kilimo utakuta tuna ongelea zaidi gharama na faida lakini Mara chache mno watu wataongelea soko kwa undani.

Rudi tena kwenye miradi mkuu Ila Safari hii anza kwanza kulijua soko vizuri la kitunguu na kuku. Uzuri mkuu Ontario kajitolea kuunganisha watu na soko la uhakika la kuku.

Kingine kwenye kilimo jifunze ni wakati gani soko linakuwa limejaa zao husika kwa maana wakulima wengi wanakuwa wanavuna na wakati gani zao linakuwa halipatikani kwahiyo wewe hakikisha unalima ili uvune kipindi ambacho zao husika (kitunguu) halipo kwa wingi sokoni. Ila hapa nitoe angalizo, Mara nyingi kulima ili uje kuvuna kipindi ambacho kitunguu kipo kichache sokoni huwa kuna Changamoto sababu Mara nyingi huwa ni msimu ambao Hali ya hewa hairuhusu kitunguu kustawi Kama wewe ulivyo kumbwa na ukungu Ina maana ulilima kipindi ambacho sio favorable kwa kitunguu, kwahiyo kipindi hili inabidi uwe na uangalizi wa Hali ya juu mnoo, ukifanikiwa kuvuna hata gunia 60 kwa ekari kipindi hiki umetusua


Kila la kheri

Aluta continua
Mapambano yanaendelea
Asante mkuu kwa ushauri wako
 
Alishakataa hiyo kitu! Ukipitia comments za mwanzo kuna Jamaa aliomba hiyo formula!
Mwenyewe natamani hata akipatikana mtu wa uhakika nimlipe anifundishe

Mimi niko kwenye hii biashara ya kuku wa nyama na kweli vile vyakula vya makampuni bei imekua mbaya sana. Nina formula tatu mpaka saiv ambazo zote nimeanza kuzifanyia majaribio. Nimelipia kuzitengeneza na zinanipa majibu tofauti tofauti. Hii ya mwisho majibu ntayapata mwez July mapema. Naanza kuwalisha weekend hii.

Ikikamilika nitawapatieni hio formula hata kwa kuchangia kidogo.
Ila mpaka sasa hivi mfuko wa dukani ni 70,000 na mimi ninapochanganya natumia 50,000
 
Mkuu kwa tarifa tu,miradi yangu nasimamia mwenyewe mara nyingi, mke wangu na kaka yangu ndio kazi yao kubwa, sipigwi kwenye cost,ila tu mradi unakua hauna manufaa, kwamfano nimelima vitunguu Ruaha kule kiasi cha ekatano, ofcoz ukungu ulipiga sana nimevuna gunia 60 hivi lakini hata mteja simpati now ni second week, nilifuga kuku nyumbani kwangu Kimara wa nyama mwenyewe bila kutegemea mfanya kazi nikakosa soko kabisaa mpaka nikauza kuku mmoja 2500 wanaofuga hawa viumbe wanajua hasara yake. ni vitu vingi sana vilivyonitia hasara,ninahitaji kitu ambacho nitafanya mwenyewe preferbly of professional nitakachofanya mwenyewe kuanzia saa tisa na nusu mpaka usiku na siku za weekeend


Mkuu kwenye hio ya kuku wa nyama naweza kukusaidia. Biashara yake tatizo inahitaji connection kupata masoko. Fahamiana na wafugaji wengine. Mimi nna mwaka mmoja toka nianze nilianza na kuku 100 sasa hivi wako 600.

Tulichofanya sisi ni kushikilia masoko na tunakua tunapokezana kuagiza vifaranga kwa interval ukiwa na soko la kuku100 kila siku manaake ni kwamba mimi kuku wangu ndani ya siku 34wanakua wameisha wakati huo mtu mwingine anakamatia lile soko mi naagiza vifaranga(mwanzoni nilikua naona aibu hata kwenda kwenye vile vikao lwakua ni wamama tu ) ila nilipofanikiwa kuingia katika hio club raha msatarehe.

Nilipojaribu mara ya kwanza ilibaki kidogo wanidodee na mimi nilikaa nao hadi wiki 7 na wanaendelea kula tu. Nusura niache ila nikarudia pamoja na kuzunguka zunguka kupata masoko mambo mazuri.

Kwa maana hiyo kama mimi binafsi ningekua na mtaji nina uwezo wa kutoa kuku 100 kila siku(Faida ni zaid ya 150,000) na ukiwa na kuku wa kila umri manaake uweze kuchinja kuku 3000 kwa mwezi fikiria faida yake.

Ishu inakuwaga pale unapouza ukimaliza uanze kukuza upya ukirud soko limekabwa na wengine na ni muda wa kutoa kuku....hapo ndo nilikua natembea naongea peke yangu kama chizi. Huku nilipo tunauza 7000
 
93 Reactions
Reply
Back
Top Bottom