naomba ufafanuzi wa haraka kuhusu kodi ya magari ....!

meningitis

JF-Expert Member
Nov 17, 2010
8,349
4,674
naomba nimnukuu ndugu mgimwa

Kuongeza kiwango cha Ushuru wa Bidhaa kwenye magari yasiyo ya uzalishaji (Non-Utility Motor Vehicles) ya umri wa zaidi ya miaka 10 kutoka asilimia 20 hadi asilimia 25. Hatua hii inalenga katika kupunguza uagizaji wa magari chakavu, kulinda mazingira na kupunguza ajali;

nimeshaagiza kigari changu cha mwaka 2002 sasa hiki kilichoongezeka ni kitu gani?

CIF 3600USD.
 
Kaka, hiyo maana yake hicho kigari chako, Pamoja na CIF 3600, kikifika tu bandarini lazima kiwekewe bei nyingine kwa mujibu wa bei za gari ya aina hiyo kwenye soko sasa hivi huko Japan. Halafu inapigwa 25% ya bei hiyo Kama kodi. Twafwa
 
Utalipa kodi ya kawaida,utajumlisha na dumping charge (uchakavu)ambao nadhani kuanzia trh 1/7 utakuwa 25% badala ya 20%,hatujuhi aina ya gari uliloagiza na CC zake ili upate makisio..na kitu kingine ni kwamba TRA wanaweza ku uplif hiyo CIF yako($3600)na kusababisha cost kuwa juu zaidi.kiufupi ni kwamba uchakavu peke yake wawezakuwa Tsh 1.8ml,weka details za gari ili upate makisio
 
Andaa 80% mkuu. Mi nilitaka kushindwa kutoa mwezi jana. Jamaa noma
 
Andaa 80% mkuu. Mi nilitaka kushindwa kutoa mwezi jana. Jamaa noma

Yani kwa sasa kama hujajipanga ni kazi sana wana uplift sana kuliko ata cost halisi ya bidhaa,nilitoa container langu wiki chache zilizopita,kuna baiskeli ndogo nilinunua $100 wao katika makisio yao wakasema $300,total cost ilipokuja wala sikuamini macho yangu
 
Valuation ya kodi za magari
Import Duty 25%
Vat 18%
Excise Duty cc O-2000 ni 5%
Cc 2001-> ni 10%
Kama imezidi miaka kumi toka ilipoundwa adhabu yake yaani Dumping fees ya sasa ni 20% mpya kuanzia Jully1 itakuwa 25%
 
Utalipa kodi ya kawaida,utajumlisha na dumping charge (uchakavu)ambao nadhani kuanzia trh 1/7 utakuwa 25% badala ya 20%,hatujuhi aina ya gari uliloagiza na CC zake ili upate makisio..na kitu kingine ni kwamba TRA wanaweza ku uplif hiyo CIF yako($3600)na kusababisha cost kuwa juu zaidi.kiufupi ni kwamba uchakavu peke yake wawezakuwa Tsh 1.8ml,weka details za gari ili upate makisio
mkuu gari yangu ni subaru 2000cc
 
Back
Top Bottom