Naomba ufafanuzi kuhusu rais kupewa uwenyekiti wa chama CCM

nyamalagala

JF-Expert Member
Jun 5, 2016
744
673
Natumai wana JF mu bukheri wa afya kwa kudra za maulana
Katiba ya JMT ya mwaka 1977 toleo la 2005 katika sura ya pili sehemu ya kwanza ibara ya 33-(2)Rais atakuwa mkuu wa nchi,kiongozi wa serikali na Amiri jeshi mkuu.

Nirejee kwenye mada.bila shaka kila mtu anaelewa tukio litakalotokea Tarehe 23/7/2016 katika jengo la CCM dodoma.Ni wazi kuwa mh JPM atashika hatamu kwenye nafasi ya juu ndani ya chama hicho.sisi sote tunamtambua JPM kuwa ndiye Rais halali wa Tanzania kwa mjibu wa mamlaka aliyopewa na katiba.Sasa najiuliza yeye kwenda huko Dodoma kwenye shughuli za chama chake ataenda katika mwonekano upi kati ya haya.

1_ataenda kama rais wa tanzania au kama mwana CCM wa kawaida?

2_atatumia gharama za serikali kwenda huko au za CCM?

3_Je,atapewa ulinzi kama apewao akiwa na kofia ya urais?

4_Je,ikitokea baada ya kukabidhiwa kijiti hicho kutoka kwa JK akahutubia kidogo atakuwa anaongea na watanzania wote kama Rais au atakuwa anawahutubia wana CCM?

5_kama kawaida yake kutoa matamko ya ghafla tamko lolote litakalotolewa litawahusu wanaCCM au watanzania wote,?

6_Je,atatumia gari maalum la Rais au magari ya chama?
Uzi huu si wa uchochezi bali ni kutaka kujua namna ya kupambanua mambo.Nini wananchi wasio wana CCM wafanye endapo garama na mali za taifa zitaonekana kutumika kwenye mambo ya chama?

Naamini humu JF kuna wajuvi wa mambo haya na nawaombeni mtufahamisheni mustakabali wa mambo haya.
Kama kuna mahali nimekosea naruhusu kusahihishwa.

Naomba kuwasilisha.

nyamalagala
 
Nchi ya ahadi.

Nasubiri kusikia ataahidi kitu gani na kama kuna kaburungutu katatolewa au la.
 
Natumai wana JF mu bukheri wa afya kwa kudra za maulana
Katiba ya JMT ya mwaka 1977 toleo la 2005 katika sura ya pili sehemu ya kwanza ibara ya 33-(2)Rais atakuwa mkuu wa nchi,kiongozi wa serikali na Amiri jeshi mkuu.

Nirejee kwenye mada.bila shaka kila mtu anaelewa tukio litakalotokea Tarehe 23/7/2016 katika jengo la CCM dodoma.Ni wazi kuwa mh JPM atashika hatamu kwenye nafasi ya juu ndani ya chama hicho.sisi sote tunamtambua JPM kuwa ndiye Rais halali wa Tanzania kwa mjibu wa mamlaka aliyopewa na katiba.Sasa najiuliza yeye kwenda huko Dodoma kwenye shughuli za chama chake ataenda katika mwonekano upi kati ya haya.

1_ataenda kama rais wa tanzania au kama mwana CCM wa kawaida?

2_atatumia gharama za serikali kwenda huko au za CCM?

3_Je,atapewa ulinzi kama apewao akiwa na kofia ya urais?

4_Je,ikitokea baada ya kukabidhiwa kijiti hicho kutoka kwa JK akahutubia kidogo atakuwa anaongea na watanzania wote kama Rais au atakuwa anawahutubia wana CCM?

5_kama kawaida yake kutoa matamko ya ghafla tamko lolote litakalotolewa litawahusu wanaCCM au watanzania wote,?

6_Je,atatumia gari maalum la Rais au magari ya chama?
Uzi huu si wa uchochezi bali ni kutaka kujua namna ya kupambanua mambo.Nini wananchi wasio wana CCM wafanye endapo garama na mali za taifa zitaonekana kutumika kwenye mambo ya chama?

Naamini humu JF kuna wajuvi wa mambo haya na nawaombeni mtufahamisheni mustakabali wa mambo haya.
Kama kuna mahali nimekosea naruhusu kusahihishwa.

Naomba kuwasilisha.

nyamalagala
 
Back
Top Bottom