Naomba ufafanuzi kuhusu mitihani ya bodi NBMM/NBAA

TAECOLTD

JF-Expert Member
Mar 2, 2013
1,051
1,831
Habari za muda huu wandugu? Nimekuja kwenu na jambo moja kwa ushauri zaidi..nimekuwa naona watu wengi wakiongelea kwenda Advance School na wengine kwenda Certificate chuo lakini katika kupitia kwangu threads nyingi sijaona mtu akigusia suala la kukunja kona na kufanya mitihani ya bodi. Nimefuatilia zaidi na kufahamu kwa ufupi kuhusu bodi ya procurement iliyopo kurasini ambapo kutokana na vigezo vyao ni kuwa

1) Mwanafunzi aliyemaliza form four na ufaulu anaweza soma na kufanya mitihani ya bodi kwa kuanzia Basic Stage one na two ambapo akimaliza ni kama anakuwa sawa na aliyesoma certificate na anaruhusiwa na kutambuliwa na chuo chochote.

2) Mwanafunzi aliyemaliza form six na ufaulu anaweza soma na kufanya mitihani ya bodi kwa kuanzia foundation one na two ambapo akimaliza ni kama aliyesoma Diploma na anatambuliwa na vyuo vyote na anaweza kujiunga degree kokote

3) Mwanafunzi aliyemaliza degree anaweza kufanya mitihani ya bodi stage five ya mwisho kutegemeana na degree yake aliyosoma kisha akatunukiwa cheti cha bodi kama CPSP...

Sasa concern yangu ni namba mbili kwa Mwanafunzi wa form six. Kwanini haizungumziwi sana na je ninaweza kusoma hiyo mitihani na kusonga mbele na kama yupo aliyesoma hiyo foundation one na two afafanue changamoto na faida za kufanya mitihani hiyo?!
Asanteni na ninakaribisha michango yenu...!!!
 
Ni njia nzuri ila ndefu sana. Mitihani migumu alafu kama huna degree kupata exemption paper zinakuwa nyingi sana. Wenzako watamaliza chuo na kuja final stage wewe unasota tu. Kama una kichwa kizuri unaweza kumaliza ndani ya miaka mitatu lakini wachache sana wanaoweza ku clear professional exams zote kwa single sit kila level.
 
kwa ufahamu wangu mimi, NBMM/NBAA pale sio njia ya kupita, Ni bora uende ukasome chuo tu. kwasababu wanafunzi wengi wanaoenda hapo NBAA ni wale ambao tayari wana degree na wanatafuta kusomea, kufanya mitihani na kupata cheti cha certified public accounts CPA ambacho ni cheti muhimu sana kwa wahasibu. Kwa nilivyosikia kutoka kwa wadau wa accounts ni kwamba ukiwa na CPA hukosi kazi bank yeyote hapa Bongo.
 
kwa ufahamu wangu mimi, NBMM/NBAA pale sio njia ya kupita, Ni bora uende ukasome chuo tu. kwasababu wanafunzi wengi wanaoenda hapo NBAA ni wale ambao tayari wana degree na wanatafuta kusomea, kufanya mitihani na kupata cheti cha certified public accounts CPA ambacho ni cheti muhimu sana kwa wahasibu. Kwa nilivyosikia kutoka kwa wadau wa accounts ni kwamba ukiwa na CPA hukosi kazi bank yeyote hapa Bongo.
Ndugu swala sio kukosa au kupata ajira..hiyo CPA ni stage ya mwisho kwa accounting ila Kuna stages za mwanzo Kabisa ambapo wanaweza kusoma watu wa form four na six mpaka kufikia CPA kama kwa NBMM inavyoanzia Basic kisha Foundation na kisha Profession na mwisho wa stage anatunukiwa cheti Cha CPS, CPSP
 
Back
Top Bottom