Naomba ufafanuzi juu ya sanitizer na hand wash

Jskinondo

Member
Jan 9, 2020
36
34
Kama kichwa kinavyo ongea, kutokana na janga la Corona virus pandemic, watu wana shauriwa kunawamikono kwa maji tiririka na sabuni.

Lakini siku hizi wengine wanaona kunawa maji kila wakati ni usumbufu kwahiyo hutumia sanitizer kama mbadala wa kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni.

Njia zote hizi bado zina maswali ambayo wananchi wengi hawajapata ufafanuzi mzuri.

Hii imepelekea wengine kuamini ukinawa mikono kwa maji tiririka na sababu au kupaka hand sanitizer ni suruhisho la kuviua virus vya Corona.

Binafsi hii sintofahamu bado inanichanganya kama inavo wachanganya baadhi ya watu.

Mfano 1: kwa upande wa matumizi ya sanitizer; bado sina uhakika kama nikipaka sanitizer mikononi inaweza kuviua virusi vya corona.

Najiuliza hili swali na ningependa nipate ufafanjzi sababu sanitizer bei yake ipo juu na inatakiwa itumike mara kwa mara unapo interact na mtu au watu endapo nitapata uhakika kuwa inaweza kuua corona virus na bacteria nitajitahidi kutumia.

Mfano: 2 kwa upande wa kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni: bado sijafaham ni sabuni zipi zina faa kutumika na zipi hazifai kutumika kunawa mikono.

Hili limepelekea sabuni zote kutumika mtaani.

Najiuliza swali hii sababu tulio wengi uchumi wetu ni mdogo wengine pesa ya kula tu ni ya kuunga unga.

Mambo yote haya yanafanyika sababu ya kukosa elimu juu ya matumizi sahihi ya hizi vitu.

Kama ilivyo kwenye wiki ya nyungu kabla ya wataalam wa tiba asilia hawajatoa mchanganyiko sahihi wa kujifukiza, wapo walio kwisha changanya miti zaidi ya sita na waliwafukiza hadi watoto chini ya miaka 3.

Ni vema hili nalo likatolewa ufafanuzi kusudi watu wasifanye mambo kwa kubahatisha.

Naamini hapa Jf tuna madaktari bingwa ambao wanaweza kutoa elimi kwa niaba ya wengine.

#Stay home# stay safe.
 
Umemalizia vizuri sana, fuata maelekezo ya wataalam. Siyo ya ccm. Jihadhari nao Sana, sasa hivi ajenda zao zimebaki mbili tu. Uhujumu uchumi na ubeberu, yale mambo ya uzalendo na kukusanya mapato wamepiga chini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maji Tiririka na Sabuni ni Bora na Ndio Chaguo La Kwanza.

Ila kama mazingira hayaruhusu kuweka MAJI maeneo kama BANKS, MALLS, Kwenye MAGARI au MAJI YANAPATIKANA KWA SHIDA KWA BAADHI ya maeneo.

Hapo Hand Sanitizers zinakuwa CHAGUO LA PILI.
 
Sanitizer zina ethanol ama ethyl alcohol ya 98%, pia kuna peroxide ndani yake na glycerol kuongeza tu thickness na viscosity alcohol ya kiwango hicho na peroxide vinauwezo wa kuvunja protein coat ya virus wengi na hata bacteria, hivyo kwa sanitizer iliyotengenezwa kwa ubora unaofaa unaweza kabisa kuua virusi mikononi mwako

Sabuni zenyewe zina sulfate (hydrophilic), katika ile long chain ya fatty acid (hydrophobic) ukiangalia hizi zote kazi kubwa ni kutoa kitu chochote ambacho kimejishika katika surface, ila kazi kubwa ya sabuni siyo kukiua kirusi bali ni kukiondoa mikononi mwako kwa urahisi..

Nafikiri utaona vyote vina kazi sawa ila mbinu tofauti...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sanitizer zina ethanol ama ethyl alcohol ya 98%, pia kuna peroxide ndani yake na glycerol kuongeza tu thickness na viscosity alcohol ya kiwango hicho na peroxide vinauwezo wa kuvunja protein coat ya virus wengi na hata bacteria, hivyo kwa sanitizer iliyotengenezwa kwa ubora unaofaa unaweza kabisa kuua virusi mikononi mwako...
Ahsante kiongozi, vip kuhusu sabuni naweza kutumia sabuni yoyote haina shidah?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa mkuu,hata sabuni ya kipande na ya unga zinafaa kutumika au vip
Maji Tiririka na Sabuni ni Bora na Ndio Chaguo La Kwanza.

Ila kama mazingira hayaruhusu kuweka MAJI maeneo kama BANKS, MALLS, Kwenye MAGARI au MAJI YANAPATIKANA KWA SHIDA KWA BAADHI ya maeneo.

Hapo Hand Sanitizers zinakuwa CHAGUO LA PILI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama kichwa kinavyo ongea, kutokana na janga la Corona virus pandemic, watu wana shauriwa kunawamikono kwa maji tiririka na sabuni.

Lakini siku hizi wengine wanaona kunawa maji kila wakati ni usumbufu kwahiyo hutumia sanitizer kama mbadala wa kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni.

Njia zote hizi bado zina maswali ambayo wananchi wengi hawajapata ufafanuzi mzuri.

Hii imepelekea wengine kuamini ukinawa mikono kwa maji tiririka na sababu au kupaka hand sanitizer ni suruhisho la kuviua virus vya Corona.

Binafsi hii sintofahamu bado inanichanganya kama inavo wachanganya baadhi ya watu.

Mfano 1: kwa upande wa matumizi ya sanitizer; bado sina uhakika kama nikipaka sanitizer mikononi inaweza kuviua virusi vya corona.

Najiuliza hili swali na ningependa nipate ufafanjzi sababu sanitizer bei yake ipo juu na inatakiwa itumike mara kwa mara unapo interact na mtu au watu endapo nitapata uhakika kuwa inaweza kuua corona virus na bacteria nitajitahidi kutumia.

Mfano: 2 kwa upande wa kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni: bado sijafaham ni sabuni zipi zina faa kutumika na zipi hazifai kutumika kunawa mikono.

Hili limepelekea sabuni zote kutumika mtaani.

Najiuliza swali hii sababu tulio wengi uchumi wetu ni mdogo wengine pesa ya kula tu ni ya kuunga unga.

Mambo yote haya yanafanyika sababu ya kukosa elimu juu ya matumizi sahihi ya hizi vitu.

Kama ilivyo kwenye wiki ya nyungu kabla ya wataalam wa tiba asilia hawajatoa mchanganyiko sahihi wa kujifukiza, wapo walio kwisha changanya miti zaidi ya sita na waliwafukiza hadi watoto chini ya miaka 3.

Ni vema hili nalo likatolewa ufafanuzi kusudi watu wasifanye mambo kwa kubahatisha.

Naamini hapa Jf tuna madaktari bingwa ambao wanaweza kutoa elimi kwa niaba ya wengine.

#Stay home# stay safe.
Ukipaka sanitizer mikononi inaua virusi na hata backeria. Sanitizer ya alcohol iwe angalau 70% ethanol au methanol.

Sabuni za kawaida hazitaua virusi ila kuna aina ya subuni zenye antimicrobial action kama vile detol hii inaweza kuua virus na bacteria. Detol inaweza pia kutumika kama sanitizer.

Ila detol hubaki kwenye mikono yako kwa muda mrefu na hivyo huweza kuendelea kuua hata bacteria wazuri walioko chini zaidi kwenye ngozi yako na kufanya ngozi yako iwe nyembamba(thinning of skin). Hili laweza kuwa tatizo kwani ngozi yako yaweza kuwa laini mno na kushambuliwa na bacteria/fungus kirahisi endapo utatumia detol kila mara kwa muda mrefu.

Uzuri wa sanitizer zinazotumia alcohol in kwamba zinaua vimelea vya juu ya ngozi na mara moja sanitizer hizo huvukishwa (evaporate) bila kukuacha na harufu au madhara ndani ya ngozi.

Ni vizuri ukawa na kichupa cha sanitizer ya alcohol na kutembea nacho mfukoni hasa kwa wale wanaopanda mabasi au kushika sehemu zinazoshikwa na watu wengi kama milango, ATM, n.k, tumia mara baada ya kushika vitu hivyo.

Ukiosha mikono kwa sabuni za kawaida sharti ujikaushe na upake sanitizer, kuosha mikono peke yake haiui virusi.
 
"Sanitizer" na sabuni + maji tiririka vyote viwili ni Sanitizers, vinafanya kazi moja. Vyote viwili ni antiseptics.
Sanitizer yenye alcohol huuwa viruses na bacteria. Sabuni + maji tiririka huondoa bacteria na viruses kwenye ngozi au surface yoyote mechanically, bila kuviuza ingawa baadhi vinaweza kufa.
For fast action, tumia Sanitizer yenye 70% ethanol au methanol. Glycerine huongezwa ili ngozi isikakamae na kuwa ngumu maana alcohol peke yake inafanya ngozi ikakamae.
Sanitizer inatakasa ngozi, kama ambavyo sabuni + maji tiririka vinafanya. Hamna sababu ya kupaka sanitizer baada ya kunawa na sabuni + maji tiririka.
Mimi napendelea kupaka zanitizer kuliko maji tiririka + sabuni.
Sabuni yoyote inafaa, ila labda medicated soap inafaa zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom