Titicomb
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 11,290
- 17,734
Wakuu habari?
Kwanza nimpongeze sana DC Sabaya jinsi alivyo weka juhudi kuwasaidia watu waliolalamika kulaghaiwa na kampuni ya Q-Net wilayani kwake.
Katika mazungumzo yake na waalimu akawauliza "bado tu hamjajifunza jinsi taasisi ya DESI ilivyofumuliwa na Rais Magufuli?"
Chanzo: Youtube channel ya Jamiiforums.
Kwa kumbukumbu zangu DESI ilisimamishwa kufanya kazi zake na viongozi wake kushitakiwa wakati wa Waziri mkuu Mh.Mizengo Pinda na raisi akiwa Mh. Jakaya Kikwete.
Mh.Pinda ndiyo alisimamia zoezi hilo.
Kwa vile mimi binadamu huenda nimesahau naomba kukumbushwa sakata la DESI lilishughulikiwa wakati wa raisi gani?
Kama nipo sahihi ilikuwa kipindi cha Mh.Kikwete basi naomba niweke rekodi sawa kama nilivyo eleza.
Wakati mwingine kama viongozi wetu au wanasiasa wanataka kutoa sifa au kukumbushia taarifa kama hizi basi wajizuie kutaja majina ya viongozi au muda husika endapo hawana uhakika wa nani alihusika.
Yakifanyika makosa kama haya mnawapa nafasi wakosoaji wenu kuthibitisha mnasema uongo sana au mnasifia sana kupita uhalisia kiasi cha kumfanya anaye sifiwa aonekane mpenda sifa kupitiliza kumbe hajawatuma.
Ilitosha kusema 'hamjajifunza jinsi DESI ilivyo fumuliwa na serikali' bila kumtaja mheshimiwa raisi.
Mwisho DC Sabaya nakupongeza sana kwa juhudi ulizofanya hadi kuwatafuta watu wa BRELA hapo hapo kwenye kikao wakupe uthibisho wa usajili wa Q-Net.
Pia naomba niwaulize jeshi la polisi na vyombo vingine vya kusimamia sheria kwanini mnasubiri mambo kama haya yaje kushughulikiwa na viongozi wakubwa wa kisiasa?
Hamkupata malalamiko ya wananchi juu ya Q-Net na hii biashara yao yenye kutia mashaka?
Kwanza nimpongeze sana DC Sabaya jinsi alivyo weka juhudi kuwasaidia watu waliolalamika kulaghaiwa na kampuni ya Q-Net wilayani kwake.
Katika mazungumzo yake na waalimu akawauliza "bado tu hamjajifunza jinsi taasisi ya DESI ilivyofumuliwa na Rais Magufuli?"
Chanzo: Youtube channel ya Jamiiforums.
Kwa kumbukumbu zangu DESI ilisimamishwa kufanya kazi zake na viongozi wake kushitakiwa wakati wa Waziri mkuu Mh.Mizengo Pinda na raisi akiwa Mh. Jakaya Kikwete.
Mh.Pinda ndiyo alisimamia zoezi hilo.
Kwa vile mimi binadamu huenda nimesahau naomba kukumbushwa sakata la DESI lilishughulikiwa wakati wa raisi gani?
Kama nipo sahihi ilikuwa kipindi cha Mh.Kikwete basi naomba niweke rekodi sawa kama nilivyo eleza.
Wakati mwingine kama viongozi wetu au wanasiasa wanataka kutoa sifa au kukumbushia taarifa kama hizi basi wajizuie kutaja majina ya viongozi au muda husika endapo hawana uhakika wa nani alihusika.
Yakifanyika makosa kama haya mnawapa nafasi wakosoaji wenu kuthibitisha mnasema uongo sana au mnasifia sana kupita uhalisia kiasi cha kumfanya anaye sifiwa aonekane mpenda sifa kupitiliza kumbe hajawatuma.
Ilitosha kusema 'hamjajifunza jinsi DESI ilivyo fumuliwa na serikali' bila kumtaja mheshimiwa raisi.
Mwisho DC Sabaya nakupongeza sana kwa juhudi ulizofanya hadi kuwatafuta watu wa BRELA hapo hapo kwenye kikao wakupe uthibisho wa usajili wa Q-Net.
Pia naomba niwaulize jeshi la polisi na vyombo vingine vya kusimamia sheria kwanini mnasubiri mambo kama haya yaje kushughulikiwa na viongozi wakubwa wa kisiasa?
Hamkupata malalamiko ya wananchi juu ya Q-Net na hii biashara yao yenye kutia mashaka?