Prodigy Oligarchy
JF-Expert Member
- Mar 21, 2020
- 571
- 643
Salaam,
Tuzidi kuchukua tahadhari dhidi ya Covid-19 , maana ipo na ni hatari.
Naomba niingie moja kwa moja katika mada husika;
Ni hivi, kuna ndugu yupo mkoa fulani ndani ya Tanzania. Ndugu huyu anamtoto mmoja tu, ambaye ni wa kike.
Umri wa msichana wake, ni chini ya miaka 22, lakini haishuki chini ya 20. Huyu binti elimu yake, karibia yote ya secondary alisoma shule ya bweni tena nje ya mkoa wao.
Kilichonifanya kuandika uzi huu wa kuomba msaada wa ushauri ni baada ya ndugu huyo hivi karibu kuwasiliana nami, kuniuliza ikiwa ninafahamu madaktari bingwa wa magonjwa ya wanawake.
Sikuwa na jibu la moja kwa moja juu ya swali lake, ndipo nilipomuuliza 'kulikoni' ?
akaanza kunielezea, kwamba kwa takriban mwaka na nusu binti yake , kila anapoingia kwenye period, basi huwa anakua ni mgonjwa wa taaban, hajiwezi kwa lolote kwa chochote, na anakua na maumivu makali mno ya tumbo, yaloyopitiliza na anakua anatapa-tapa kama vile anataka kufa kabisa.
Wamejaribu kumpeleka hospital kadhaa, lakini hakuna cha zaidi sana walichopata zaidi tu ya kumpa dawa za kutuliza (amenitajia dawa, nimesahau).
Akaongeza kwamba, kuna kipindi walimfanyia vipimo, wakabaini ana viuvimbe kidogo, lakini hawawezi kumfanyia upasuaji, akasema huenda akija kushika ujauzito na kujifungua basi na vyenyewe vitaisha.
Nilimuuliza huwa inachukua muda gani, akasema ni muda ambao anakua ndani ya siku zake, ila akimaliza au akiwa mwishoni mwishoni kukaribia kumaliza, huwa anakua sawa.
Sijui tu ni kwanini, lakini mawazo yangu yalienda mbali sana, mbali mno, nikawaza/nikahisi huenda pengine binti alishawahi kutoa ujauzito , na kinachomsumbua ni matokeo ya alichofanya kwa siri.?!
Nilikumbuka likizo fulani, ndugu alifanya tu mawasiliano namie, akaniambia 'fulani likizo hii hatokuja, kwa sabahu hatorudi nyumbani, anabakia shuleni' ilinishangaza kidogo na hata ndugu yangu huyo ambaye ndiye mzazi wake ilimshangaza pia lakini akajua huwenda anatulia ili apate muda wa kujisomea zaidi.
Na cha ajabu ni kwamba, ni kitu ambacho hakikuwahi kujirudia. Ninaambiwa, Aliporudi, afya yake haikuwa yule wa sikuzote, kuna muonekano fulani wa tofauti kidogo yupo nao, mwanzoni walihisi ni kwa sababu ya shule, ila haikuwahi kubadilika, hakuwahi kurudi kwenye muonekano wake wa kawaida kama alivyokua awali (anase,a mzazi wake)
Naomba wataalamu wa kada hii ya afya, haswa ambao wamebobea kwemye mambo haya ya afya ya uzazi especially kwa wanawake, mnisaidie ikiwa mawazo yangu yapo sahihi, na kama ndio ni hatua gani za kumsaidia zichukuliwe?
Nitashukuru kwa michango yenu itakayotoa mwanga mzuri wakuweza kumsaidia.
Ahsante.
P. Oligarchy.
Tuzidi kuchukua tahadhari dhidi ya Covid-19 , maana ipo na ni hatari.
Naomba niingie moja kwa moja katika mada husika;
Ni hivi, kuna ndugu yupo mkoa fulani ndani ya Tanzania. Ndugu huyu anamtoto mmoja tu, ambaye ni wa kike.
Umri wa msichana wake, ni chini ya miaka 22, lakini haishuki chini ya 20. Huyu binti elimu yake, karibia yote ya secondary alisoma shule ya bweni tena nje ya mkoa wao.
Kilichonifanya kuandika uzi huu wa kuomba msaada wa ushauri ni baada ya ndugu huyo hivi karibu kuwasiliana nami, kuniuliza ikiwa ninafahamu madaktari bingwa wa magonjwa ya wanawake.
Sikuwa na jibu la moja kwa moja juu ya swali lake, ndipo nilipomuuliza 'kulikoni' ?
akaanza kunielezea, kwamba kwa takriban mwaka na nusu binti yake , kila anapoingia kwenye period, basi huwa anakua ni mgonjwa wa taaban, hajiwezi kwa lolote kwa chochote, na anakua na maumivu makali mno ya tumbo, yaloyopitiliza na anakua anatapa-tapa kama vile anataka kufa kabisa.
Wamejaribu kumpeleka hospital kadhaa, lakini hakuna cha zaidi sana walichopata zaidi tu ya kumpa dawa za kutuliza (amenitajia dawa, nimesahau).
Akaongeza kwamba, kuna kipindi walimfanyia vipimo, wakabaini ana viuvimbe kidogo, lakini hawawezi kumfanyia upasuaji, akasema huenda akija kushika ujauzito na kujifungua basi na vyenyewe vitaisha.
Nilimuuliza huwa inachukua muda gani, akasema ni muda ambao anakua ndani ya siku zake, ila akimaliza au akiwa mwishoni mwishoni kukaribia kumaliza, huwa anakua sawa.
Sijui tu ni kwanini, lakini mawazo yangu yalienda mbali sana, mbali mno, nikawaza/nikahisi huenda pengine binti alishawahi kutoa ujauzito , na kinachomsumbua ni matokeo ya alichofanya kwa siri.?!
Nilikumbuka likizo fulani, ndugu alifanya tu mawasiliano namie, akaniambia 'fulani likizo hii hatokuja, kwa sabahu hatorudi nyumbani, anabakia shuleni' ilinishangaza kidogo na hata ndugu yangu huyo ambaye ndiye mzazi wake ilimshangaza pia lakini akajua huwenda anatulia ili apate muda wa kujisomea zaidi.
Na cha ajabu ni kwamba, ni kitu ambacho hakikuwahi kujirudia. Ninaambiwa, Aliporudi, afya yake haikuwa yule wa sikuzote, kuna muonekano fulani wa tofauti kidogo yupo nao, mwanzoni walihisi ni kwa sababu ya shule, ila haikuwahi kubadilika, hakuwahi kurudi kwenye muonekano wake wa kawaida kama alivyokua awali (anase,a mzazi wake)
Naomba wataalamu wa kada hii ya afya, haswa ambao wamebobea kwemye mambo haya ya afya ya uzazi especially kwa wanawake, mnisaidie ikiwa mawazo yangu yapo sahihi, na kama ndio ni hatua gani za kumsaidia zichukuliwe?
Nitashukuru kwa michango yenu itakayotoa mwanga mzuri wakuweza kumsaidia.
Ahsante.
P. Oligarchy.