Naomba tuongee UHALISIA kuhusu biashara ya Real Estate kutumia mfano HAI

Rufaro

JF-Expert Member
May 7, 2022
222
340
Nashukuru kwa makaribisho mazuri.!

Naomba moja kwa moja niende kwenye mada husika.

Naamini asilimia kubwa pengine tupo katika biashara either iwe kubwa au wastani au ndogo. Sasa najua wengi wetu tumekuwa tunasikia baadhi ya wafanyabiashara wanakuambia kuwa mfano alianza na pea moja ya viatu na sasa ana kiwanda cha viatu, mwingine anakuambia nilianza na kubrash viatu (shoeshine) na sasa anamiliki makampuni ya kuuza juisi au mabasi. Hili jambo limekuwa linanipa ukakasi sana.

Basi naomba leo tujadiliane kwa pamoja kuhusu hili na pia tuanze na mfano hai na naamini kupitia maandishi haya wengine pia wataweza kuokota chochote kitu kitakachowasaidia nao pia katika safari yao kibiashara. Ni ndoto za kila mfanyabiashara haswa ndogondogo kwamba anachofanya kitakuwa kikubwa na sio kuishia chini.

Mfano hai wangu ni huu, je nitawezaje kuifanya biashara ya real estate yenye nyumba moja tu ya kupangisha ya familia yenye kuingiza Tsh. 450,000/- kwa miezi mitatu, kuifanya kuwa biashara kubwa ambayo ntakuwa namiliki nyumba za kukodisha(renting) za kukaa na apartments pia na majengo mengi ya kukodisha kama frem za kufanyia biashara? Karibuni tushirikiane kwa pamoja, najua kwenye jumuiya hii ya JamiiForums kuna wafanya biashara wakubwa na wazoefu, na washauri wazuri na hata wanaofanya hii real estate.

Thread hii itakuwa muendelezo....

Asanteni
 
*Kupandisha thamani
Kama nyumb haina maji & umeme unaviweka vinaongeza thaman hii inajumuisha muonekano mzma wa nyumba inayopangishwa rangi,floor nk
* Formalize biashara
Achana na uswahili andaa mikataba na wapangaji kisheria itakusaidia kupata wateja formal +bima ya nyumb
* Usitake return mapema sana
 
*kupandisha thamani
Kama nyumb haina maji& umeme unaviweka vinaongeza thaman hii inajumuisha muonekano mzma wa nyumba inayopangishwa rangi,floor nk
* formalize biashara
Achana na uswahili andaa mikataba na wapangaji kisheria itakusaidia kupata wateja formal +bima ya nyumb
*usitake return mapema sana

Asante mkuu kwa ushauri, ila..

*Nyumba ina maji na umeme !

* Floor naweza kusema bado tiles.

*Rangi pia iko okey.

*Mikataba ipo kisheria kabisa huwa nafanya hivyo huwa sikabidhi kienyeji kabisa.

*Bima bado.
 
Nenda katumie hiyo nyumba kukopa benk, then njoo Nungwi pub tuipangie matumizi hiyo pesa. Kufa kupo maisha ni hayahaya hakuna maisha mengine
mkuu nyumba bado hati haijatoka, na hata ingekuwepo, benki gani wangenipa mkopo bila usumbufu na delays zisizoisha , nina mifano hai kwa ninaowajua wamesumbuliwa na walitumia hati lakin hawajapata.
 
Uza nyumba iliyopo; kanunue viwanja, na ujenge nyumba ndogo ndogo za wapangaji
Asante mkuu kwa ushauri, ila naomba niulize nipate ufafanuzi wako, tuende katka uhalisia.

Nyumba hii hadi kukamilika nimetumia milioni 70, kwa ushaur wako naweza kuuza kwa shilingi ngapi, na kiasi hiko kinunue viwanja vingapi, kwa bei isiyozidi kias gani, na ramani ya nyumba hizo ndogo unazosemea ndugu za wapangaji zitakua za vyumba vingapi? Na nyumba hizo zitakua ngapi? Na kodi yake isizidi kiasi gani?
 
Kupangisha kwaajili ya makazi itakuchelewesha..kama uko site nzuri toboa fremi za biashara..ama igeuze iwe gest house.

#MaendeleoHayanaChama
 
Biashara ya Real estate Africa ni tricky sana badala ya kufikiria nyumba ya kupangisha kawaida fikiria zaidi kuwa na small modern units mfano unit moja yenye sebule open kitchen na chumba cha kulala master kama square meter 40 mpaka 45 Kwenye compound moja unaweza kupata units 10 kwenye eneo la square meter 1000
 
Kupangisha kwaajili ya makazi itakuchelewesha..kama uko site nzuri toboa fremi za biashara..ama igeuze iwe gest house.

#MaendeleoHayanaChama
Asante mkuu kwa ushauri, ila site ilivyokaa nikisema fremu itakua ngumu sababu site haiko vizuri, hata atakayepangisha business yake haitoonekana labda kama atakua na wateja wake special wa simu, pia nikisema gesti house, Je itakuwa sahihi gesti kuwa katika mazingira ya nyumba za watu na watoto?
 
Back
Top Bottom