Naomba tafsiri ya ndoto hii

Maana yake siku za hivi karibuni utaolewa na mganga wa kienyeji. Kwa hyo jipange mama. Ni mwendo wa kula kuku na mbuzi wa kafara kwa mrija.
 
Kama mwezi mmoja au miwili nyuma niliota nipo sehem na mwenzangu ambaye nahis alikua mwanaume ambaye cjui kama namjua au simjui ila ni kama vile alikua ananiongoza yaan anataka kunionyesha kitu ambacho aliniambia mie nikambishia kuwa hicho kitu hakiwezekan.

Kwahiyo akaniambia kama unabisha twende tukafika sehem kama kulikua nankitanda hivi akainama kidogo uvunguni mwa kitanda akanyanyuka na mie nikafanya vile vile sasa ile nanyanyuka pale uvunguni natembea hatua mbili kugeuka nyuma nikaona kuna mwanaume kavaa kilemba chekundu anatufuatilia kwa nyuma japo tumemuacha mbali kidogo lakn anaonyesha juhudi za kutukimbilia nikawa naogopa huku tunaendelea kutembea tukafika sehem kuna kama uwanja na watu wengi yule akajitokeza mtu mmoja akaniambia ukitaka huyo asiwafuatulie chukua mtama huu hapa mmwagie..

sasa nikachukua mtama ile namumwagia hiv akaukwepa japo ulimpata kidogo kwahivo tukaendelea kutembea na tukampiga chenga pale kwenye kundi la watu! Ila tumetembea mbele kidogo mara tena nikamuona huyo katokea manake katutafuta hadi katuona ndoto ikaishia hapo.

Siki ya pili yake tena nikaota mwanaume kavaa kilemba cheusi na yeye ananifuata aah sikumbuki ndoto yake ilikuaje lakin nakumbuka tu hapo kuwa alinifata.

Sasa umepita huo muda zaid ya mwezi mmoja leo tena nimeota watu wawil wale wale mmoja kavaa kilemba chekundu na mwingne cheusi eti wamekuja pembeni ya kitanda changu halafu wakanisujudia kkaa wananiomba kitu hivi...

Naombeni anayejua tafsir ya ndoto hii yenye muendelezo anisaidie maana hata sielew ni kina nan hao wanaonifuata?

Na kwanini wamefunga vilemba? Sioni sura zao vizuro lakin najua ni wanaume weusi na vilemba wamevifunga vizuri tu.

Msaada wenu tafadhali maana naogopa sana!
Unadalili ya kua mganga
 
Acha utani kie nauliza kweli ujue
Mambo ya ndoto mda mwingine huwa ni fikra tu na mawazo yako. Ila binafsi hua ninaota usiku kama kuna jambo baya litatokea kesho yake. Mfano kuna siku niliota nimesimama pembeni ya kaburi na watu wengi wamenizunguka wanalia. Ile naamka tu kesho yake asubuhi mjomba wangu akanipigia simu ananiambia rudi nyumbani kuna tatizo nilikua chuo alafu kesho yake kulikua na test. Nikamwambia mjomba siwez nina test kesho. Akaniambia nenda ni muhimu akakata simu. Mda huo huo bro nae akanipgia simu ananiambia rudi nyumban mzee amefariki. So kua makin nenda kanisan mueleze mchungaj uombewe.
 
Kuna baadhi ya ndoto unaota ukiwa hujashiba sawasawa, nyingine ukiwa umeshiba na kupitiliza, nyingine ukiwa na njaa na nyingine ukiwa na madeni lukuki...

Hizi ndoto lazima uwe mwangalifu sana.
 
Inabidi uwe makini na watu ambao utakuwa nao kimahusiano.. Usimkubalie mtu usiyemjua kiundani zaid utakubali mapepo...

Sina mengi ila ni hayo tuu nyota yako iko vyema watu wanataka kuitumia sasa njia ya kukupata ni kwa mahusiano
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom