Naomba nafasi ya kazi unayoona inafaa kwa CV yangu, nina uzoefu

be unique

JF-Expert Member
Oct 12, 2016
2,374
2,273
Habari wakuu,heshima kwenu nyote,

Kama kichwa kinavyoeleza hapo juu,ombi kuu ni kuomba nafasi ya kazi, nafahamu hapa kuna watu mbalimbali na wenye nafasi tofauti tofauti na katika wengi waswahili tunasema haliharibiki jambo.

Kwanza nianze na kusema sehemu niliyokuwa nafanya kazi nafasi yangu ilichukuliwa na mtu mwingine baada ya kutokuwa kazini kwa muda mrefu kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu,hapa nawatoa shaka wale wataodhani nimefukuzwa au kufanya jambo lolote sehemu ya awali katika kazi.

ELIMU
Elimu yangu ni ngazi ya diploma ya manunuzi na ugavi (procurement and supply)

SKILLS
Driving.. driving licence with classes of vehicles A, A2, B, C, C2, C3, D, E and certficate from VETA.

EXPERIENCE
  • Ass.Store Supervisor at Export Trading Group
  • ass.Store Officer at Tanzania Ports Authority

In all level of experience is more than 3 years.

AREAS OF COMPETITION:
  • Stores supervising
  • Clearing and forwarding
  • Procuring and supply
  • Driving

And other area through my experience and education background.

Nitashukuru sana kama nikipata nafasi kupitia wana JF wenzangu, Nawakaribisha PM.

Shukrani
 
Uliajiriwa bandarini TPA Dar es salaam? hiyo ajira ya serikali imeishaje kimasikhara hivyo?
 
Uliajiriwa bandarini TPA Dar es Salaam? Hiyo ajira ya serikali imeishaje kimasikhara hivyo?

Sio ajira rasmi mkuu,kuna utaratibu wa vibarua pale, unafanya kazi zile zile za professional lakini unakuwa katika nafasi ya kibarua.

Kutokana na wingi wa watu nafasi inakuwa ngumu kupata kama ulipotea kwa muda mrefu.
 
Sio ajira rasmi mkuu,kuna utaratibu wa vibarua pale,unafanya kazi zile zile za professional lakini unakuwa katika nafasi ya kibarua.
Kutokana na wingi wa watu nafasi inakuwa ngumu kupata kama ulipotea kwa muda mrefu.
nasikia vibarua tu mle mnakula mpaka laki 9.

sasa jiajiri mkuu mambo ya ajira haya utapasuka
 
nasikia vibarua tu mle mnakula mpaka laki 9.

sasa jiajiri mkuu mambo ya ajira haya utapasuka

Kibarua kwa shift ni 9000/=, na hili uione pesa ni kupata nafasi kila siku yakufanya kazi tofauti na hapo ni maumivu mkuu.
 
Habari, nina diploma ya ugavi na udhoefu wa mikopo, individual and groups (microfinance) nahitaji kazi yoyote kwa sasa,nikipata usimamizi na utendaji kwenye biashara yako nitakuingizia faida sana, nina management skills kubwa sana na uaminifu mkubwa sana
0712605935
Nipo DSM
26,yrs
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom